INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, September 30, 2013

VIDEO – ANOTHER NOLLYWOOD STAR JIM IYKE CAPTURED AT SCOAN LIVE!

Making a surprise appearance in The SCOAN, Nollywood superstar Jim Iyke entered quietly and unannounced, joining worshippers from around the world as they listened to the inspiring message from renowned Prophet T.B. Joshua.



As The SCOAN’s Wise Men moved through the congregation in prayer, the lightning of God located Iyke and he was no longer able to control himself. Lunging towards one of the Wise Man as if to attack him, an evil spirit that had been tormenting the life of Jim Iyke manifested! The congregation in the auditorium and the overflow congregations shouted in surprise as they began to witness the deliverance of a m
Jim Iyke, born James Ikechukwu Esomugha, is currently one of the highest paid actors in the Nigerian movie industry and cultivated the name “Nollywood bad boy” for himself. As one of the most successful actors in Nollywood, he has starred in over 150 films to date. He has launched his own film production unit, “Untamed Productions” and his own music label, “Untamed Records” with his very own album, “Who Am I?” He is also founder of “Jim Iyke Foundation”, contributing funds to children of the less privileged and children with physical challenges.

Among his movie awards are: The Teenage Choice Award, Best Actor In Nigerian Entertainment Award, African Achievement Award, Best Actor of the Year (Mode Men Award 2010), Sexiest Man In Nigeria 2008, Best African Actor (NET Awards).

The evil spirit that had tormented the life of Jim Iyke for so many years began to manifest, confessing that it was the cause of Iyke’s setback and disappointment. It confessed that it was the reason he could never marry, stating that it would not allow him to love anyone. It continued confessing that Iyke was the biggest and that it was only God’s grace that had kept him. As the evil spirit inside him struggled to attack the Wise Man, the supremacy of the Holy Spirit continued to overpower it.

The deliverance continued but the battle was not against flesh and blood; it was against the spiritual entities that had been causing crisis in his life, family, health, career and future.

To the jubilation of the congregation, the name of Jesus Christ prevailed over the evil spirit and Jim Iyke received his freedom. Overwhelmed with what had just happened, Iyke immediately knelt in God’s presence, appreciating His Creator for his miraculous deliverance.

The humility demonstrated by Jim Iyke in submitting himself to the power of God should prompt others in his industry to make the same life-saving choice.

Friday, September 27, 2013

YAFAHAMU MAJINA YA ASILI YA BAADHI YA MASTAR WA BONGO MOVIES ......






KWA kawaida binadamu yeyote huzaliwa na kubatizwa jina ambalo hulitumia katika masomo na hata kazi yake.
Tofauti na ilivyo katika fani nyingine, wasanii wamekuwa wakijibatiza majina ya ziada (a.k.a). Mbaya zaidi, majina hayo huwa yanaanza kama utani lakini inafika wakati msanii husika

analizoea jina hilo jipya na kulifanya kuwa kama rasmi. Leo Amani linakuletea orodha ya baadhi ya mastaa ambao majina waliyopewa na wazazi wao ‘yamekufa’, hawayatumii kabisa: LULU

Jina lake halisi ni Elizabeth Michael, Lulu lilizoeleka kupitia tasnia ya uigizaji. Alianza kulitumia wakati alipojiunga na Kundi la Sanaa la Kaole.

Hadi leo hii, siyo rahisi kabisa mtu kutokea na kumuita jina la Elizabeth, wengi wanamfahamu kwa jina la Lulu.
RAY
Ray ndiyo jina ambalo limezoeleka na wengi. Vincent Kigosi alilopewa na wazazi wake ni kama limekufa. Kwa zaidi ya miaka kumi sasa tangu alipokuwa kwenye Kundi la Sanaa la Kaole hadi sasa.
Jina la Ray ndiyo watu wanalolifahamu zaidi ingawa hivi karibuni baadhi ya wasanii wenzake wamekuwa wakijaribu kumuita Vincent ili kurudisha uhai wa jina hilo.

JOHARI
Jina lake halisi ni Blandina Chagula. Johari lilizaliwa kwenye Tamthiliya iliyobeba taito ya jina hilo. Akiwa katika Kundi la Kaole, alianza kujiita Blandy, baadaye alibadilisha jina hilo na kuwa Johari walipoingiza tamthiliya hiyo ambayo pia ilizaa filamu.
“Kuna wakati huwa najuta kutumia jina la a.k.a ambalo limefunika kabisa jina langu la asili,” anasema Johari.

DK. CHENI
Ameanza gemu kitambo, tangu Kundi la Splended. Jina alilopewa na wazazi wake ni Mahsein Awadhi, kwa sasa limekufa. Hakuna anayelitumia, hata yeye mwenyewe.
Jina hilo lilizaliwa baada ya mazoea yake ya kupenda kuvaa cheni kubwa kwenye michezo iliyokuwa ikirushwa Runingani, kwa sasa wengi wanashindwa hata kulitamka jina lake.

ODAMA
Jina lake halisi ni Jenniffer Kyaka, limekufa kabisa kwa sasa. Wengi wanamfahamu kama Odama jina ambalo alilipata kwenye filamu iliyoitwa Odama miaka sita iliyopita
Tangu ilipotoka filamu hiyo hadi leo, jina la Odama limegeuka kuwa ndiyo la asili.

BATULI
Jina alilopewa na wazazi wake ni Yobnesh Yusuf lakini wengi hawalijui. Alianzia kuigiza katika Kundi la Kaole. Alianza kujiita Nesh, baadaye akabadilisha na kujiita Batuli baada ya kucheza filamu ya ‘Fake Smile’ ya marehemu Steven Kanumba.
Toka hapo, watu wote wakamfahamu kupitia jina la Batuli, wachache sana wanaolijua jina la Yobnesh, zaidi ni ndugu zake wa karibu.

JB
Majina mengi ya a.k.a ameitwa. Aliitwa Bonge la Bwana, Mtumishi, Eric Ford na mwisho jina la JB likasimama katika akili za watu.
Mwenyewe anasema jina la JB analipenda sana, kuna wakati hata yeye huwa anasahau kabisa kama anaitwa Jacob.


NORA
Jina lake halisi ni Nuru Nassoro. Takriban miaka kumi iliyopita baada ya kujiunga na Kundi la Kaole, jina la Nuru limekufa kabisa.
Familia yake nzima wanatumia jina la Nora na si Nuru tena, amelikubali na analipenda kutoka moyoni mwake.

RICHIE RICHIE
Huyu naye ni msanii wa muda mrefu, jina lake halisi ni Single Mtambalike. Wengi hawalifahamu jina lake halisi.
Wanamuita Richie Richie utadhani ndiyo alilopewa na wazazi wake, jina hilo alipewa takriban miaka kumi na tano iliyopita akiwa na Kundi la Nyota Ensembles.

CATHY
Huyu anaitwa Sabrina Rupia, Cathy lilikuja katika michezo kipindi hicho akiwa katika Kundi la Nyota Ensembles. Limeendelezwa hadi leo na kipo kizazi ambacho hakilifahamu kabisa jina la Sabrina zaidi ya Cathy.

RAYUU SASA YUKO MAHUTUTI KITANDANI MARA BAADA YA KUCHOROPOA MIMBA KIENYEJI










Hivi karibuni zilienea habari za chini chini kuwa muigizaji wa filamu nchini maarufu kwa jina la Rayuu zikidai kuwa ametoa mimba kienyeji na sasa yuko kitandani angali akiuguza maumivu...

Habari hizo zilimfikia mpekuzi wetu wa kitengo maalumu cha UMBEA na kuamua kumtafuta Rayuu ili atoe ufafanuzi wa issue hiyo.

Katika utetezi wake, mrembo huyo alizikana taarifa hizo na kudai kuwa yeye hana historia ya kuchoropoa mimba..

Inatoka: Vituko vya Ntaa

KUMBE AUNT EZEKIEL NA KANUMBA WAMETOKA MBALI......

Kanumba akipewa busu zamani, katika moja ya picha alizowahi igiza na Aunty Ezekiel.

Kanumba na Aunty Ezekiel, katika pozi kweye moja ya filamu walizowahi cheza kala ya kifo cha Kanumba

Kanumba

Aunty Ezekiel

Wednesday, September 25, 2013

MANAIKI SANGA NA IRINE UWOYA WALETA GUMZO KUBWA JIONEEE



Wasanii Manaiki Sanga na Irene Uwoya wakiwa kwenye picha za mahaba huku Uwoya akigida bieeeee hadi kuche.



Na Mwandishi Wetu


Mtandao hatari wa habari wa Xdeejayz kwa mara nyingine umekuwa wa kwanza kunasa picha za wasanii mastaa toka kiwanda cha bongo movie Manaiki Sanga na Irine Uwoya zikiwaonesha wakiwa kwenye mahaba mazito huku Irine akiwa ho kwa kiraji “pombe”.

Habari makini toka chanzo chetu makini ambacho ni rafiki wa karibu na Irine Uwoya kilisema Irine na Manaiki kwa sasa wako kwenye mahusiano ya karibu kiasi cha kuzua minong’ono kwa kudhani huenda wanamahusiano ya upande wa pili.

Hata hivyo chanzo hicho kiliendelea kusema kwa picha hizo zinadaiwa kupigwa katika viunga vya Club Maisha ambako walienda kula bata usiku kucha na hapo inaonekana ni asubuhi.

Aidha xdeejayz ilifanya juhudi za kuwatafuta wasanii hao ili kuweka bayana kuhusu picha zao hizo za mahaba na Uwoya ndiye aliyeanza kuvutiwa waya lakini hata hivyo simu yake iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa na alivyopigiwa Manaiki Sanga na baada ya mwandishi wetu kujitambulisha na chombo cha habari anachotoka hali ilikuwa tofauti kidogo kwani msanii huyo alianza kumporomoshea matusi makubwa mwandishi wetu huku akiituhumu blog hii kuongoza kumchafua kwa kuanika mambo yake ya siri hadharani.

Mtandao hatari wa habari wa Xdeejayz kwa mara nyingine umekuwa wa kwanza kunasa picha za wasanii mastaa toka kiwanda cha bongo movie Manaiki Sanga na Irine Uwoya zikiwaonesha wakiwa kwenye mahaba mazito huku Irine akiwa ho kwa kiraji “pombe”.
Habari makini toka chanzo chetu makini ambacho ni rafiki wa karibu na Irine Uwoya kilisema Irine na Manaiki kwa sasa wako kwenye mahusiano ya karibu kiasi cha kuzua minong’ono kwa kudhani huenda wanamahusiano ya upande wa pili.

Hata hivyo chanzo hicho kiliendelea kusema kwa picha hizo zinadaiwa kupigwa katika viunga vya Club Maisha ambako walienda kula bata usiku kucha na hapo inaonekana ni asubuhi.
Aidha xdeejayz ilifanya juhudi za kuwatafuta wasanii hao ili kuweka bayana kuhusu picha zao hizo za mahaba na Uwoya ndiye aliyeanza kuvutiwa waya lakini hata hivyo simu yake iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa na alivyopigiwa Manaiki Sanga na baada ya mwandishi wetu kujitambulisha na chombo cha habari anachotoka hali ilikuwa tofauti kidogo kwani msanii huyo alianza kumporomoshea matusi makubwa mwandishi wetu huku akiituhumu blog hii kuongoza kumchafua kwa kuanika mambo yake ya siri hadharani.

Friday, September 13, 2013

FILAMU YA JICHO LANGU IS COMMING SOON..JIPANGE SASA KUJIPATIA COPY YAKO...!!

 Unaweza kujiuliza mambo mengi sana juu ya mane haya...JICHO LANGU. Hii ni filamu ilkiyoandaliwa na Mtanzania wenu Jennifer Kyaka (Odama) katika kampuni yake ya J-Film 4 Life iliyopo hapa jijini Dar es Salaam, Kinondoni.

J-Film 4 Life inakuhimiza kuipanga kithabiti kuhakikisha unajipatia copy yako mmapema na uweze kusikia na kuona kile kinacvhoitwa JICHO LANGU. Filamu imebeba mambo mbalimbali yahusuyo jamii kwa lego zima la kuelimisha, kuadibisha, kufundisha, kuburudisha pia kuhakikisha wewe Mtazanaji unafuata yale mema yaliyoonyeshwa katika fialmu hii.

BAADA YA "FOOLISH AGE" KUANZA KUFANYA VIZURI ...MASTAA WA BONGO WAMTUMIA LULU MCHAEL VITISHO









KUFANIKIWA kwa uzinduzi wa filamu ya Foolish Age ya msanii Elizabeth Michael ‘Lulu’ uliofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, kumemfanya kinda huyo anayetingisha katika tasnia hiyo kupata vitisho kutoka kwa mastaa wenzake.

Habari kutoka vyanzo mbalimbali ndani ya fani hiyo zinasema katika uzinduzi huo, msanii huyo alifunika na kuonyesha dalili zote za kuwazima mastaa wenzake ambao kwa muda mrefu wamekuwa juu.
Taarifa hizo zinasema staa huyo wa Bongo Muvi anatafutwa kwa kila namna, usiku na mchana ili kuhakikisha nyota yake inafifia.
Madai hayo yamekuja zaidi baada ya uzinduzi huo kufana kwani pamoja na mambo mengine, hata jinsi alivyokuwa amejipanga kwa walinzi wake, lilikuwa ni jambo kubwa ambalo linafanana na inavyotokea katika shughuli za mastaa mbalimbali wa majuu.
Mwandishi wa gazeti hili aliamua kufunga safari hadi maskani kwao pande za Tegeta, lakini msanii huyo hakupenda paparazi afike kwao hivyo mazungumzo yao kufanyika kama ifuatavyo kwa njia ya simu ya kiganjani.

Mwandishi: Mambo vipi Lulu?

Lulu:
Salama tuu za kwako?

Mwandishi: Salama, vipi umesikia vitisho vyako kutoka kwa mastaa wa Bongo Muvi wanaodai kuwa umekuja kuwapita kisanii?

Lulu: Hapana sijasiki, lakini kama wanatoa vitisho lazima wakubaliane na ukweli kwamba lazima awepo wa kwanza na wa mwisho, wakaze buti.

Mwandishi: Umejipangaje kukabiliana na hilo?

Lulu: Najipanga kufanya kazi mimi kama mimi na wao wafanye kama wao, wakijifanya kuwa kama mimi haiwezi kuwa hivyo, mbona mastaa wa ughaibuni kama Beyonce na Rihanna wako tofauti? Lazima awepo wa kwanza mpaka wa 10 hatuwezi kulingana.

Mwandishi: Kuna lolote la kuongeza juu ya hilo ama wito kwa wasanii?

Lulu: Wajipange kufanya kazi kwa nguvu zote, wasifanye kama mimi wafanye kama wao,

Mwandishi: Asante Lulu nakutakia siku njema

Lulu: Ok, sawa kazi njema

SOURCE: GPL

Monday, September 9, 2013

MAPYA NDANI YA SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA...MSANII WA BONGO MOVIE 'AISHA BUI' AFUNGWA BLAZIL,MCHUMBA WA PENDO WA MAISHA PLUS AKAMATWA CHINA NA MBWANA MATUMLA AKAMATWA NCHINI HISPANIA.

 HABARI INATOKOA KATIKA BLOGU YA VITUKO VYA MTAA



Kwa wiki iliyopita, tuilipekenyua maeneo yote muhimu na kukumbana na mambo mapya kuhusu habari za ‘unga’ huku taarifa zikionesha kuwa, hali katika viwanja vye ndege duniani kote ni tete.

MNIGERIA ALIYEKAMATWA NA ‘UNGA’ ALITAHADHARISHWA MAGOMENI
Anthonie Ojo, raia wa Nigeria aliyekamatwa Septemba 4, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar (JNIA), akijaribu kusafirisha kete 99 za unga na ndege ya Shirika la Ethiopian Airways alinaswa.
Mwanamke huyo aliyevalia baibui akidai anakwenda kuhiji Maka, anadaiwa aliununua mzigo huo Magomeni-Mapipa jijini Dar. Aliziweka kete hizo kwenye makopo yaliyokuwa na poda ya Johnson.
Kwa mujibu wa uchunguzi wetu, wenyeji waliomuuzia unga mwanamke huyo walimtahadharisha kuhusu hali ya ulinzi iliyopo sasa JNIA hasa baada ya Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe kushikia bango udhibiti wa unga lakini mtuhumiwa huyo alidaiwa kusema atapita kwa anavyojua yeye.


MTANZANIA AFA DUBAI AKIWA NA UNGA TUMBONI
Ukiachilia mbali tukio la mwanamke huyo, habari zilizolifikia juzi zilidai kwamba Mbongo aliyejulikana kwa jina moja la Chambuso amefariki dunia katika Jiji la Dubai, Falme za Kiarabu kutokana na unga alioubeba tumboni kuyeyuka kabla ya kufika kwenye kituo husika.
Habari za uhakika kutoka chanzo chetu jijini Dar zinasema kuwa marehemu Chambuso alikuwa na ‘mlinzi’ wake ndani ya Ndege ya Emirate huku akiwa hamjui.
Ikazidi kudaiwa kuwa, baada ya kushuka jijini Dubai, hali ya Chambuso ilianza kubadilika akilalamikia zaidi maumivu ya tumbo, ndipo ‘mlinzi’ huyo alipombeba na kumpeleka hospitali (haikutajwa jina).
“Baada ya kufariki dunia, jamaa (mlinzi) alijiweka mbele akitaka kufanya maarifa kwa madaktari ili tumbo la jamaa lipasuliwe atoe mzigo. Akashtukiwa, akakimbia na mpaka sasa maiti hiyo iko chini ya ulinzi wa serikali,” kilisema chanzo



Tuachane na kifo cha Chambuso huko Dubai. Septemba 2, mwaka huu zilitufikia taarifa kwamba, mchumba wa mwigizaji Pendo Mushi ‘Pendo wa Maisha Plus’ aliyejulikana kwa jina moja la Tasha amedakwa na unga nchini China.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, Tasha alikamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Beijing nchini humo akiwa na unga aina ya heroin (kiasi na thamani hakikutajwa).
Ili kupata uhakika wa madai hayo, juzi Ijumaa Wikienda lilimtafuta Pendo kwa njia ya simu ya mkononi na kumuuliza kuhusu madai hayo ambapo alikiri.
“Yeah, ishu ni kweli. Mimi nilizipata hizo taarifa kutoka kule nikawaambia ndugu zake. Kwa mujibu wa mtu wake aliyekuwa naye kule (China) jamaa (Tasha) ameshapandishwa kortini,” alisema Pendo huku akisema uchumba wake na Tasha ulishakufa.

AISHA BUI ETI KAFUNGWA BRAZIL!

Wiki mbili sasa, mapaparazi wetu wamekuwa wakifuatilia kwa undani kuhusu kusambaa kwa madai kwamba, staa wa filamu za Kibongo, Aisha Bui eti kafungwa miaka 5 jela katika gereza moja nchini Brazil baada ya kukamatwa na madawa ya kulevya kwenye kibegi.
Kwa mujibu wa madai ya habari hizo, eti Aisha alidakwa kwenye uwanja wa ndege wa jijini Brasilia akirejea Bongo kupitia Dubai.
Septemba 2 na 5, mwaka huu, waandishi wetu walifika nyumbani kwa baba wa Aisha, Kigamboni, Dar kutaka kujua ukweli.
Septemba 2, mtu aliyekutwa nyumbani hapo alisema Aisha yupo Brazil lakini hakuna mawasiliano naye na alikwenda siku chache kabla ya Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, Julai mwaka huu.
Septemba 5, hakukutwa mtu ila majirani walielekeza eneo analopatikana mzee huyo ambapo ni ufukweni. Hata hivyo, sehemu hiyo hakupatikana na waandiishi waliacha namba zao za simu.
Jioni, mzee Bui alizipata namba zilizoachwa, saa 9:00 usiku wa kuamkia Septemba 6 alimpigia simu mwandishi wetu na kumvurumishia matusi huku akisema akome kumfuatafuata akidai yeye hana mawasiliano na binti yake tangu mwaka 2007.
Mzee huyo alikwenda mbele zaidi kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu (SMS) kwenye simu ya paparazi akitumia lugha ya Kiarabu ambapo kwa mujibu wa wataalam wa lugha hiyo ni dua ya kumwombea mabaya mwandishi huyo.

NZOWA AMZUNGUMZIA
Ili kwenda mbele zaidi, mapaparazi wetu walikwenda ofisini kwa Kamanda wa Kikosi Maalum cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa ili kutaka kujua kama amesikia lolote kuhusu Aisha Bui.
Alisema: Eee, kuna habari kama hiyo lakini si rasmi kwangu, bado nafuatilia Brazil ikiwa tayari nitawajulisha tu.
tulimtafuta Aisha kwenye mitandao, hasa Facebook, Instagram na Twitter bila mafanikio.tumemwachia ujumbe kwa kuamini kwamba akirudi hewani ataukuta na kujibu lakini wapi!

UZUSHI WA MBWANA MATUMLA KUNASWA NA UNGA HISPANIA WAWASHANGAZA WENGI


  Wiki iliyopita ilihitimika kwa redio moja kutangaza habari kwamba mmoja wa wanafamilia ya mzee Matumla, Mbwana Matumla amenaswa na unga nchini Hispania na kuwashangaza wengi.
Watu waliozungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki walisema kwamba walishangaa kusikia habari hiyo huku wakiwa wanamwona Mbwana mitaani.
“Sasa huyu kakamatwa Hispania huku tukiwa tunamwona mitaani, maana yake nini jamani? Alihoji msomaji wetu mmoja na kuongeza kwamba, yeye alikutana na bondia huyo siku tano nyuma.
Ijumaa Wikienda lilimsaka Mbwana kwa njia ya simu yake ya mkononi bila mafanikio, lakini lilipomtafuta kaka mtu, Rashid Matumla, Jumamosi iliyopita alisema Mbwana amejaa tele nyumbani kwake, Gongo la Mboto, Dar.

Friday, September 6, 2013

POLE SANA AUNT EZEKIELI KWA KUTOBOLEWA NA CHUPA CLUB



INASIKITISHA! Staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson ‘Gwantwa’ yupo hatarini kukatwa mkono kutokana na jeraha la chupa alilolipata hivi karibuni.
Tukio la Aunt kupigwa chupa na mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Yvonne nje ya Club Bilicanas, Posta jijini Dar, lilitokea Agosti 26, mwaka huu wakati staa huyo alipokwenda kujiachia na mshosti zake.
Baada ya kupigwa chupa siku hiyo, Aunt alikimbizwa katika Hospitali ya Aga Khan lakini bahati mbaya alikosa daktari wa kumtibu hivyo akalazimika kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Dk. Mvungi, Kinondoni ambapo alishonwa nyuzi sita pamoja na dawa za kukausha kidonda.

ALIKATISHA DOZI
Kwa mujibu wa chanzo makini, Aunt ni muoga wa dawa na wakati kidonda kikiwa bado hakijapona vizuri aliacha kumeza dawa alizopewa.
Chanzo hicho kilisema tatizo la staa huyo kukatisha dozi lilisababisha kidonda kishindwe kupona na badala yake kikaanza kutengeneza usaha na taratibu mkono ukaanza kuoza.
“Mkono ulifikia hatua ukaanza kuoza kwani licha ya kushonwa lakini kilibadilika rangi ndipo alirudi hospitali.

 ASAFISHWA UPYA
Imeelezwa kuwa mapema wiki hii, Aunt alirudi tena katika Hospitali ya Dk. Mvungi na kusafishwa upya kidonda baada ya madaktari kugundua tatizo lilizidi kuongezeka.

MKONO ULIANZA KUOZA
Kwa mujibu wa nesi wa hospitali hiyo aliyeomba hifadhi ya jina lake, hali ya Aunt ilimshtua daktari, akamwambia aombe Mungu kwani kidonda kilichimbika sana na tatizo kama hilo huweza kusababisha mtu kukatwa mkono.
“Iligundulika mkono ulikuwa unaoza, daktari alimwambia amuombe Mungu kwani hatua iliyokuwa imefikia ni mbaya hivyo asipokuwa makini tatizo hilo litamfanya akatwe mkono,” alisema nesi huyo.

CHANZO CHA UGOMVI NI NINI?
Licha ya kuhusishwa na ugomvi wa kimapenzi baina yake na mpenzi wa Yvonne anayejulikana kwa jina la Joff, Aunt alisema ugomvi wao uliisha zamani na kila mmoja ana maisha yake.
“Yale mambo yalipita, yeye ana maisha yake na mimi nina yangu,” alisema Aunt.
Wakati huohuo, taarifa ambazo Amani limezipata kuhusu mtuhumiwa wa Aunt, Yvonne ambaye alifikishwa katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar siku ya tukio, anahaha kukwepa kifungo kwani uchunguzi ukikamilika atapelekwa mahakamani kisha gerezani.

inatoka Vituko vya Mtaa.

HUYU NDO TAPELI ALIE PONEA KIPIGO KIZITO KATIKA UZINDUZI WA FILAMU MPYA YA LULU "FOOLISH AGE"




Tapeli (katikati) akiwa anatolewa nje ya Ukumbi wa Mlimani City wakati wa uzinduzi wa Filamu ya Elizabeth Michael aka LULU mara baada ya kukamatwa akijaribu kutapeli katika moja ya Baa iliyokuwa ikitoa huduma kwa wakazi wa jiji waliofika kwaajili ya Kutazama uzinduzi wa Filamu ya Lulu mwishoni mwa wiki

Kijana ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja (katikati) akiwa amebebwa mzobemzobe na baadhi ya wafanyakazi wa Baa iliyokuwa ikitoa huduma ndani ya Ukumbi wa Mlimani city mara baada ya kukamatwa akitaka kufanya utapeli ndani ya baa hiyo iliyokuwa ikihudumia watu mbalimbali waliofika katika Ukumbi wa Mlimani City kwaajili ya Kushuhudia Uzinduzi wa Filamu ya Lulu iitwayo FOOLISH AGE uzinduzi uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City Mwishoni Mwa wiki

Baadhi ya Wafanyakazi na walinzi wakijaribu kumnusuru kijana huyo asipokee kichapo kutoka kwa wakazi wa jiji waliofika katika uzinduzi huo, huku mmoja wa wafanyakazi wa baa hiyo akitaka kupewa maelezo juu ya tukio zima ambalo kijana huyo alipokuwa akitaka kutapeli

Hapa sasa malezo yakiendelea huku akiwa kakamatwa haswa ili asiweze kuwachoropoka

Baadhi ya walinzi waliokuwepo katika uzinduzi huo wakiwa makini kuhakikisha amani inaendelea kuwepo na mtuhumiwa huyo anafikishwa kwenye ombo husika