INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, March 3, 2014

WEMA SEPETU AFANYA SHINDANO LA KUSAKA VIPAJI VYA KUIGIZA KWA WATOTO ENEO LA LEADERS JIJINI DAR LEO



Msanii wa Bongo Movie, Wema Sepetu na pia alikuwa ni jaji wa shindano la kusaka vipaji kwa watoto waliokuwa na umri kuanzia miaka minne(4) mpaka kumi na tano (15) akizungumza na mshiriki wa shindano hilo la kusaka vipaji kwa wanaojua kuigiza. Shindano hili limefanyika leo kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam na kuwapata watoto watatu waliokuwa wanaitajika.

Jaji Wema Sepetu akiwa na Jaji mwenzake Aunt Ezekiel walipokuwa wanawafanyia usahili watoto waliofika kwenye shindano la kusaka vipaji vya watoto wanaoweza kuigiza.

Msanii wa Bongo Movie, Wema Sepetu akicheza muziki na mmoja wa washiriki wa shindano la kusaka vipaji lililofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders.


ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI

Director wa shindano la kusaka vipaji, Adam akizungumza jambo

Msanii wa Bongo movie na aliyekuwa Jaji, Wema Sepetu akizungumza na mtoto aliyekuwa anashiriki kwenye shindano la kusaka vipaji kwa watoto wenye miaka minne mpaka miaka 14.

Baadi ya washiriki waliofika wakiwa na wazazi wao kwenye shindano la kusaka vipaji vya watoto wanaojua kuigiza.

Mmoja wa watoto akiigiza kwa kulia mbele ya majaji (hawapo Pichani) katika shindano la kusaka vipaji vya kuigiza lililofanyika leo kwenye viwanja vya leaders Club.


Msanii wa bongo movie akiiigiza na mmoja wa washiriki wa shindano hilo la kusaka vipaji vya watoto kwani alileta hisia kali kwa kuigiza vizuri

Palikuwa hapatoshi kwenye Stage maana watoto walikuwa wanafanya ya kwao


Msanii wa Bongo Movie, Aunt Ezekiel akiigiza na mmoja wa watoto waliokuwa kwenye shindano la kusaka vipaji.


Nae Adam (Kushoto) akuwa mbali maana hata yeye aliamua kuigiza na mmoja wa washiriki waliofika kwenye shindano hili

Wema Sepetu akiigiza na mmoja wa washiriki wa shindano la kusaka vipaji vya kuigiza

Baadhi ya washiriki wakiwa na wazazi wao




Hawa ndio watoto waliofanikiwa kuingia nusu fainali

Hawa watoto watatu ndio waliofanikiwa kushinda shindano hili mbalo liikuwa linahitaji watoto watatu

Sunday, March 2, 2014

KWANINI UKOSE TAMASHA HILI SIKU YA LEO..MESS JACOB CHENGULA KUZINDUA ALBAMU YAKE YA MUNGU HABADILIKI UBUNGO PLAZA

Jumapili ya leo ni balaa katika ukumbi wa kujidai UBUNGO PLAZA. Watu wa Mungu kukusanyika pamoja kumtukuza Mungu ambapo Mess Jacob Chengula atakuwa anazindua albamu yake ya Mungu Habadiliki. Njoo uone kazi ya Mungu na utabarikiwa sana na uimbaji wa leo

MHUSIKA WA TAMASHA
 Mess Jacob Chengula wa Mungu Habadiliki

ALBAMU INAYOZINDULIWA
Albamu ya Mungu Habadiliki ya Mess Jacob Chengula

ENEO LA UZINDUZI NI UBUNGO PLAZA

Katika hotel ya Blue Pearl

MGENI RASMI WA TAMASHA HILI

Mgeni rasmi ni Naibu Waziri wa mawasiliano Tanzania Mh Januari Makamba

WAIMBAJI WATAKAIMBA SIKU YA LEO JUMAPILI UBUNGO PLAZA

Rose Muhando

Masanja Mkandamizaji

Atosha Kissava

Bony Mwaitege

Upendo Nkone

Silas Mbise

Neema Gasper

Edson Mwasabwite

Madamu Ruti

Faraja Ntaboba

Bahati Bukuku

Mwanamapinduzi

Stella Joel


Enock

Miriamu Lukindo

Joshua Makondeko

VIINGILIO
VIP



VITI VYA KAWAIDA


WATOTO


TANGAZO LIMETENGENEZWA NA RUMAFRICA



Tembelea
www.messchengula.blogspot.com
www.rumaafrica.blogspot.com

FULSA KWENU MASHABIKI WA WEMA SEPETU..!! TAZAMA ALICHOKITANGAZA HAPA..!!

Mlete mwanao mwenye kipaji cha kuigiza acheze na Wema Sepetu, Aunt Ezekiel na Hemed Suleyman kwenye Movie mpya ya FAMILY..


Saturday, March 1, 2014

ILE FILAMU MLIYOKUWA MKISUBIRI YA JICHO LANGU ITAKUWA SOKONI TAREHE 31.03.2014. JIPATIE NAKALA YAKO

Anza mwezi Aprili na burudani kupitia  filamu mpya ya JICHO LANGU kutoka katika kampuni ya J-Film 4 Life. Tarehe 31.03.2014 ikifika jisogeze taratibu katika duka lililo karibu nawe ujipatie nakala yako ya JICHO LANGU.Ndani ya filamu hii utajifunza mengi kupitia mwigizaji maarufu nchini Tanzania Jennifer Kyaka (ODAMA) na wasanii wenzake. Hakika JICHO LANGU itakufungua mambo mengi ambayo ulikuwa hujui na hujawahi kuyaona yakitokea katika jamii yetu.

Saturday, February 22, 2014

WATU WAMUUA MCHEKESHAJI KING MAJUTO ANGALI HAI....HUU HAPA USHAIDI

JAMANI tunaombwa tunapotumiwa messege tujifunze kuisoma mpaka mwisho na sio kusoma juu tu nakuanza kuwapigia watu simu kuwapa habari zisizo za kweli.


Hivi karibuni kumekuwa na uzushi kuwa Msanii nguli wa vichekesho hapa nchini mzee King Majuto eti amefariki, Kwakweli sisi wasanii tulipata tabu sana kwa kupigiwa simu na kuulizwa eti kuna nini kimetokea huko?.. Mzee Majuto yupo?.. Mbona tunasikia kafa? Ukimuuliza mtu nani kakwambia eti nimetumiwa messege?.. Jamani tumechoka na uzushi huu jamani kwanza mzee majuto ni msanii mkubwa haiwezekani akafa ikapita wiki TV na Radio zisitangaze eti messege ndio ziungurume tuuuuuuuu...! tena kibaya zaidi messege yenyewe imetungwa na mtu tu hamna cha filamu ya majuto yenye matukio hayo wala nini.. HEBU cheki upuuzi wenyewe huu hapa chini..





King Majuto

Hamza King Majuto

MTOTO wa Mzee King Majuto ameongea kwa uchungu sana na kwa hasira sana kupitia kitendo hicho cha watu wanaoutumia muda wao kuandaa messege za ajabu za kuwazushia watu kifo aliiambia masainyotambofu kuwa swala la baba yake kuzushiwa kifo kwa kisingizio kwamba matukio hayo ni katika filamu mpya ya King Majuto huo ni uzushu mtupu.

Aliongeza kusema kuwa filamu za Baba yake zilizopo mbioni kutoka niWHY THIS ROOM, CHUNGU KIMOJA, RCO n.k. Hio iliyoandikwa katika messege ya kumzushia Baba yake kifo yeye haitambui kabisa ukweli ndio huo na Mzee Majuto yuko hai na afya nyema anaendelea na shughuli zake za sanaa kama kawaida.
HII HAPA CHINI NI MESSEGE YA MTOTO WA MAJUTO ALIOMTUMIA MWANDISHI WA WEBSITE YA Masai Nyotambofu.




Masainyotambofu

Wednesday, January 22, 2014

ENTERTAINER SET FREE FROM SMOKING AND DRINKING

Nigerian popular comedian Owen Eru, commonly known as Owen Tee, came with his wife to The SCOAN to testify of God’s miraculous deliverance through the medium of the Anointing Water. He testified that he had been living a life of smoking and alcoholism, drinking up to two crates of beer a day. He spent so much money on the two vices that he was not able to save any to afford a wedding. As a consequence, his wife’s relatives were hesitant at the idea of allowing their daughter to marry him. His wife, then his girlfriend, tried to talk him out of the two bad habits, but failed. He also tried on his own to stop through prayer and fasting but the moment he broke his fasting, he would find himself perched on the stool, drinking and smoking.


COMEDIAN OWEN TEE & FAMILY
Desperate to save their relationship and her future husband’s life, Eru’s girlfriend came to The SCOAN and received the Anointing Water. She took it home and told him that they should pray together in Jesus’ name for God’s breakthrough in their lives. After ministering the Anointing Water in prayer, they both noticed a change in their lives. Mr Eru did not smoke the following day. When he remembered that a day had passed without even a single stick, he decided to try drinking beer to see what would happen. To his surprise, the very smell and taste of alcohol suddenly became awful and disgusting. His urge for alcohol and cigarettes had completely left him. No longer wasting money on the bad habits, he was able to save money for their wedding. Jesus had broken his addiction and offered him a new life he had desperately aspired for.

“My friends have tried to tempt me with crates of beer and failed. They now buy me water. I have become a professional water drinker,” said the comedian, jokingly. His former girlfriend, now his wife, sat next to him in the church, displaying their beautiful newborn baby, a result of the glorious union God performed after his deliverance from smoking and drinking, over one year ago!

Thursday, January 2, 2014

JAZBA YATAWALA KATIKA MKUTANO WA BONGO MOVIE NA TRA...HIVI NDIVYO ILIVYOKUA

JAZBA baab’kubwa imeibuka katika mkutano wa wasanii wa filamu za Bongo ‘Bongo Movies’ na Bongo Fleva ulioandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kushirikiana na chombo cha kusimamia haki za wasanii nchini, Cosota.

Jacob Steven ‘JB’.

Tukio hilo lilijiri Jumatatu iliyopita ndani ya Ukumbi wa Vijana Social, Kinondoni, Dar ambapo mastaa wa filamu, Jacob Steven ‘JB’ na Issa Mussa ‘Cluod 112’ waliihoji Cosota juu ya tatizo la wizi wa kazi za wasanii ndipo ‘kiliponuka’ baada ya kutoridhishwa na majibu.


Issa Mussa ‘Cluod 112’.

Hali hiyo ilisababisha baadhi ya wasanii, wakiwemo JB na Cloud kutoka kikaoni na kuendelea na mambo yao mengine huku wawakilishi wa TRA wakiendelea na kikao na kufafanua mipango yao

Thursday, December 26, 2013

HATIMAYE CHUCK NORRIS AJIBU MAPIGO YA VAN DAMME KWA KUTENGENEZA TANGAZO LA KUSIMAMA JUU YA NDEGE 2 LENYE MFANO WA MTI WA CHRISMAS



Mara ya kwanza muigizaji mkongwe Jean-Claud 'Van Damme' alipotengeneza tangazo la Volvo kusimama katikati ya magari mawili makubwa ya Volvo juu ya side mirrors,mguu wa kushoto ukiwa kwenye gari moja na wa kulia kwenye lingine habari iliwashangaza watu wengi sana huku wengi wakijiuliza maswali.

VIN DIESEL ATANGAZA RASMI TAREHE YA KUACHIA FILAMU MPYA 'FAST AND FURIOUS 7'

Baada ya kusimamisha shughuli za maandalizi ya muendelezo wa saba ya Filamu ya Fast and Furious kutokana na kifo cha muigizaji 'Paul Walker aliyefariki mwishoni mwa mwezi uliopita kwa ajali ya gari.

Leo Desemba 23 Muigizaji na mkuu wa filamu ya Fast na Furious,Vin Diesel ametangaza rasmi tarehe ya kutoka kwa muendelezo wa saba wa filamu hiyo yenye mafanikio makubwa.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Diesel ameweka picha akiwa na Paul Walker na kuandika kuwa hiyo ilikuwa scene yao ya mwisho kuwa na staa huyo na kutangaza rasmi kuwa Fast and Furious sehemu ya 7 itatoka April 10 mwaka 2015.
“The last scene we filmed together…

There was a unique sense of completion, of pride we shared… in the film we were now completing… the magic captured… and, in just how far we've come… Fast and Furious 7 will be released… April 10th 2015! P.s. He'd want you to know first…,” ameandika Diesel.

Tuesday, December 17, 2013

BIFU KATI YA HEMED NA MLELA GUMZO JIJINI DAR



Hemed (kushoto) akimtishia bastola Mlela

Hemed na Mlela wakiwa wamelazwa hospitalini baada ya kuumizana huku mama yao akiwaangalia kwa huzuni


Kasha la filamu mpya ya bifu la kina Mlela na PHD inayotarajiwa kuingia mtaani keshokutwa Jumatano. LILE bifu lililowahi kufukuta kwa kasi mithiri ya moto wa kifuu baina ya ‘tozi’ wawili ndani ya tasnia ya filamu, Hemed Suleiman ‘PhD’ na Yusuf Godfrey Willard Mlela ‘Mlela’ linadaiwa kuibuka upya na kuzidisha uhasama baina ya wasanii hao. Aidha, alisema bifu hilo lilidhihirika hivi karibuni wakati wawili hao walipokutanishwa kuigiza filamu moja, kwani mara kwa mara walijikuta wakifanya kweli kwenye baadhi ya vipande vya ugomvi na mapigano jambo lililompa wakati mgumu muongozaji wa filamu hiyo inayotarajiwa kuingia sokoni kuanzia Desemba 18 mwaka huu iliyopewa jina la I Know You. “Walikuwa na muda mrefu sana bila kukutana, tukadhani bifu lao halipo tena, lakini hivi karibuni walikutana kwenye filamu iliyoandaliwa na Mtitu Game 1st Quality, wakawa wanafanya kweli kwenye baadhi ya sehemu za majibizano na mapigano huku wakifanyiana fujo mbalimbali huku kupigana vijembe vya wazi,” alisema rafiki huyo. “Ni kweli tulikuwa na utofauti, ule mvutano wa zamani bado ulikuwepo, kila mmoja hakutaka kuwa dhaifu kwa mwenzake, utaona baadhi ya vipande tulivyofanya kweli,” alisema Mlela ambapo simu ya Hemed iliita bila kupokelewa licha ya mwandishi wetu kuipiga mara kwa mara. Naye Meneja matayarishi wa Kampuni ya Game st Quality Ltd, Noel Amani ‘Futo’ alisema filamu ya I know You iliwapa wakati mgumu sana kutokana na bifu la wasanii hao kuonekana waziwazi. “Walitumbua sana, kuna wakati walifokeana kweli, kukunjiana ngumi hata hivyo kuna baadhi ya vipande walivyofanya kweli tumelazimika kuviacha ili kuleta uhalisia zaidi. Kila mmoja anaamini yuko juu ya mwenzake,” alisema Futo.

Wednesday, December 4, 2013

MTUNIS:WHO'S BAD NDIO FILAMU YANGU YA KUFUNGIA MWAKA 2013

Mtayarishaji na Muigizaji wa filamu Nice Mohamed ‘Mtunis’amesema kwamba filamu yake ya Who’s Bad itakuwa kazi yake ya kufungia mwaka kwa kuzima kazi nyingine za filamu zilizoingia pamoja na filamu hiyo ambayo inafanya vizuri sokoni baada ya kuingia mitaani hivi karibuni.

“Kama ambavyo wengi wamenizoea ninapotoa kazi inakuwa ni bora na lazima ikimbize sokoni, sinema yangu ya Who’s Bad itafunga mwaka kama kazi bora nakuwa makini sana katika utengenezaji wa filamu na ndio kilichofanyika katika filamu hiyo wasanii wamekamua sana na kuonyesho uwezo wa hali ya juu,”anasema Nice.

Filamu hiyo imeshirikisha wasanii kama Patcho Mwamba na washiriki wengine wanaofanya vizuri katika tasnia ya filamu, Mtunis amekuwa akifanya vizuri katika tasnia ya filamu Bongo kazi alizofanya ni kama Bar mead, Who’s Bad,Clinic Love na kusambazwa na kampuni ya Steps Entertainment.