INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Wednesday, January 28, 2015

JADA AMSUMBUA MAMA YAKE WA KAMBO ODAMA

Maisha ya Odama na mume wake Hemed HB yako matatani kutokana na mtoto wao JADA ambaye hataki kuona Odama akiishi vizuri na baba yake, Odama ambaye ni mama wa kambo wa JADA anateswa na  vituko vya mwanae JADA ambavyo vinamsababishia matatizo katika maisha yake. Ukitaka kujua mengi basi usikose kujipatia filamu yako mpya ya JADA inayotoka 19.02.2015.

Odama (kshoto) na mwane Jada ambaye anaonekana kuwa bize na kompyuta na anashindwa kumsikiliza mama yake wa kambo


PROF. LIPUMBA NA BAADHI YA WANACHAMA WAKE WAKAMATWA NA POLISI


Prof. Lipumba akihutubia.

TAARIFA zilizotufikia ni kwamba Mwenyekiti wa CUF, Prof Ibrahim Lipumba na wanachama wake wamekamatwa na kupigwa na Jeshi la Polisi.


Wananchi wakiwa eneo la tukio.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeeleza kushtushwa na tukio hilo la kupigwa na kukamatwa Mwenyekiti Mwenza wa UKAWA Prof. Lipumba.

Uongozi wa juu wa Chadema pamoja na mawakili wa chama hicho wameelekea Kituo Kikuu cha Polisi, Dar kwa ajili ya tukio hilo walilofanyiwa viongozi hao wa CUF na wanachama.


Polisi wakiwatawanya wananchi baada ya kuandamana.

Juhudi za Mtandao huu kumpata Kaimu wa Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda Suleiman Kova, Afande Sirro zinaendelea baada ya kumpigia simu hapo awali na kuomba kupigiwa baadaye kutokana na kikao alichokuwa nacho.

DOTNATA AMWAGA CHOZI ‘LOKESHENI’

Stori: Mwandishi wetu/Risasi Mchanganyiko
MKONGWE wa filamu Bongo, Illuminata Posh maarufu kama Dotnata, amesema alitoa machozi wakati akirekodi sinema inayohusu unyanyasaji wanaofanyiwa watoto wadogo, hasa alipobaini ukweli kuwa wanakosa mtetezi hata wa kuweza kuhisi mateso wanayokutana nayo.


Mkongwe wa filamu Bongo, Illuminata Posh 'Dotnata'.

“Watoto wanapata mateso sana kutoka kwa jamii inayowazunguka, wakipoteza wazazi au familia ikifarakana, wanaoumia zaidi ni wao kwani huingia mitaani na kuwa ombaomba, wanajiingiza kwenye wizi, ukahaba na ushoga. Wanafanya haya yote ili wapate mlo tu kwani hawana akili yoyote ya maisha yao ya mbele, jamii inapaswa kubadilika na kujadili vyanzo vya watoto wa mitaani badala ya kufikiri kuhusu misaada katika vituo vyao,” alisema Dotnata.

Filamu iliyomtoa machozi ni C.P.U ambayo yeye ameigiza kama wakala wa kuwauza wasichana kwenye madanguro ikiwahusisha wasanii wengine kama Kulwa Kikumba ‘Dude’, Richard Mshanga ‘Mzee Masinde’, Hashim Kambi ‘Ramsey’, Sauda Simba, Subira Wahure, Steve Sandhu, Nkwabi Juma, Mohamed Funga Funga ‘Mzee Jengua’ Mobby Mpambala na chipukizi kibao.a

VIVA ATAMBA MIMBA YAKE KUWA KAMA YA AUNTY

Musa Mateja/Uwazi
MSANII wa filamu Bongo, Viva ametamba kwamba mimba aliyokuwa nayo ni ya miezi sawa kama ya msanii mwenzake wa filamu, Aunty Ezekiel.


Msanii wa filamu Bongo, Viva akiwa na Aunt Ezekiel.

Akizungumza na safu hii akiwa katika tamasha moja lililofanyika katika Viwanja vya Leaders, Kinondoni, jijini Dar mwishoni mwa wiki iliyopita, Viva akiwa ameongozana na Aunty huku muda mwingi wakionekana kutambiana mimba zao, alisema huku akimgeukia mwandishi wetu:

“Kwanza nafurahi kuwa na mimba kipindi kimoja na Aunty. Mimba yangu ni kubwa na inazidi hata ya Aunty kwani ina zaidi ya miezi minne sasa, si unaiona.”

WILL SMITH, JADA KUSHEREHEKEA MIAKA 20 YA UHUSIANO WAO FEBRUARI 2015



Will Smith akiwa na familia yake.

STAA wa filamu Will Smith na mkewe Jada Pinkett wanataraji kusherehekea miaka 20 katika uhusiano wao mbali na kuwa wanandoa hao walisherehekea miaka 17 ya ndoa yao Desemba 31, mwaka jana.


Will Smith na mkewe Jada Pinkett.

Jada mwenye umri wa miaka 43, aliandika katika ukurasa wake wa Facebook kuhusu uhusiano wake na Will huku akielezea matunda ya mahusiano hayo wakiwemo watoto wao
Willow na Jaden Smith na jinsi walivyoweza kudumu katika upendo na kuvumiliana.

Aliandika hivi: Desemba 31, mwaka jana, nilisherehekea miaka 17 ya ndoa. Mwezi Februari mwaka huu nitatimiza miaka 20 tangu nilipoamua kuanza maisha na Will. Nimejifunza kuwa muungano wa watu wawili ni muujiza wa kweli na watoto ndiyo matunda ya muujiza huo.

Kwa jinsi ninavyoendelea kuupanda mlima huu wa upendo na muungano, ninahamasika kuona yote ambayo yeye na mimi tumetengeneza tukiwa kileleni mwa mlima huo. Aliandika Jada katika sehemu ya ujumbe huo.

Monday, January 26, 2015

ODAMA ASHINDA SHINDANO MSANII BORA KATIKA KIPINDI CHA FILAMU ZETU - REDIO UHURU 95.7 FM

Siku ya leo mwigizaji wa filamu Tanzania na mkurugenzai wa J-Film 4 Life, Jeniffer Kyaka (Odama) aliweza kupata mualiko wa kufika katika redio wa UHURU iliyopo maeneo ya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam Tanzania kufanya mahojiano juu ya ushindi alioupata katika kipindi cha Filamu Zetu kinachoendeshwa na mtangazaji wa redio hiyo Mama Abdul.

Kipindi hicho kilikuwa kinapambanisha waigizaji bora Tanzania ambapo Odama alipambanishwa na mwigizaji mwenzake Irene Paul. Wasikilizaji wa redio Uhuru waliweza kupiga simu na wengine kutuma meseja za kupiga kura kwa yule msanii waliona ni bora kwao. Hatiamye Jeniffer Kyaka (Odama) aliweza kuchukua ushindi

Mtangazaji wa Redio Uhuru katika kipindi cha filamu Zetu Mama Abdul (kushoto) akisoma historia ya msaanii wa filamu nchini Kenya, na kulia ni Odama akifuatilia historia hiyo.

Odama alimshukuru Mungu kwa ushindi alioupata na pia kwa wale wote waliompigia kura kwa njia ya simu. Ni kitu ambacho hakutegemea kabisa kuwa ataibuka mshindi wa shindano hilo kabambe. Aliwashukuru sana watangazaji wa redio hiyo na uongozi mzima kwa kumpa heshima ya kufanya mpambano huu mkali. Radio Uhuru ni moja ya redio bora Tanzania kwa kazi za wasanii na ndio maana wameamua kuanzisha kipindi cha Filamu Zetu.

Jeniffer Kyaka (Odama) na Mama Abdul (kulia)

Wadau waliweza kuuuliza maswali juu ya malengo yake ya baadae, naye Odama aliweza kufunguka na kuwaeleza kwa sasa yuko katika maandalizi ya kufungua kituo kwaajili ya kuinua vipaji vya wasanii wadogo ili waweze kujulikana kama yeye alivyojulikana na jamii ya Tanzania

Mtangazaji wa Redio Uhuru katika kipindi cha filamu Zetu Mama Abdul (kushoto) akisoma historia ya msaanii wa filamu nchini Kenya, na kulia ni Odama akifuatilia historia hiyo.
Wengine walitaka kujua idadi ya filamu ambazo amecheza, naye alisema mpaka sasa amecheza filamu zaidi ya 20 na hivi sasa ametoa filamu mpya inayoenda kwa jina la JADA ambayo itakuwa sokoni tarehe 19.02.2015 kwahiyo wadau wakae mkao wa kula kujipatia filamu mpya. Katika filamu hiyo wataweza kuona mtoto anayeishi na mama wa kambo anavyosumbua familia na kusababisha malumbano na kuvunjika kwa amani ndani ya familia.
Mtangazaji wa Redio Uhuru katika kipindi cha filamu Zetu Mama Abdul (kushoto) akisoma historia ya msaanii wa filamu nchini Kenya, na kulia ni Odama akifuatilia historia hiyo.
 Baadhi ya wadau walitaka kujua siri kubwa ya Odama kutokuwa na skendo mbaya kama baadhi ya wasanii wenzake, naye alisema, hii ni kutokana na jinsi yeye alivyojiwekea katika maisha yake kuwa atajitahidi sana kuishi kama Jeniffer Kyaka na sio kuishi yale maisha ambayo anaigiza katika filamu. Hii imemsaidia sana Odama na ndio maana mpaka leo jamii inamtambua Odama kama mwigizaji asiye na skendo. Pia malezi aliyolelewa na wazazi wake ambayo ni wacha Mungu na hapendi kuona anawaangusha wazazi wake kwa skendo.
 Jenifer Kyaka (Odama)
Wadau waliweza kupiga maswali mengi sana na hasa juu ya waigizaji wa filamu kuvaa mavazi ya ajabu katika jamii inayowazunguka kama wanavyofanya katika filamu zao, naye Odama alisema, hiyo ni tabia ya mtu na sio kitu kingine, kama mtu amezoea tabia hiyo ataendelea kuwa hivyo. Pia aliwaomba watu wasiwachukulie wasanii kama wote wana tabia mbaya kutokana na wanavyoona katika filamu zao bali watambue ya kuwa kile wanachofanya ni kuwakilisha vitu vinavyotokea katika maisha ya watu mitaani.
 Mama Abdul (kushoto) na Jeniffer Kyaka (Odama)
 Odama
  Odama
 Odama na mmoja wa watangazaji wa kipindi cha Filamu Zetu
  Odama
  Odama
 Mtangazaji wa Filamu Zetu - Redio Uhuru Mama Abdul

  Odama
  Odama
 Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Rumafrica (www.rumaafrica.blogspot.com), Mtangazaji wa Filamu Zetu Mama Abdul, Odama
 Mkurungenzi wa Rumafrica, RuleaSanga (kulia) na mtangazi wa kipindi cha nyimbo za tarabu redio Uhuru
 Mkurungenzi wa J-Film 4 Life, Odama (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa redio Uhuru, Angel A. Akilimali (kulia)
 Mkurungenzi wa J-Film 4 Life, Jeniffer Kyaka -Odama (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa redio Uhuru, Angel A. Akilimali (kulia)
 Kaimu Mkurugenzi wa redio Uhuru, Angel A. Akilimali
  Mkurungenzi wa J-Film 4 Life, Jeniffer Kyaka -Odama
  Mkurungenzi wa J-Film 4 Life, Jeniffer Kyaka -Odama
 Mkurungenzi wa J-Film 4 Life, Jeniffer Kyaka -Odama (kushoto) akikabidhiwa zawadi ya kalenda ya CCM na Kaimu Mkurugenzi wa redio Uhuru, Angel A. Akilimali (kulia)

ULIFIKA WAKATI WA KUPIGA PICHA ZA PAMOJA
Baadi ya wafanyakazi na watangazaji wa redio Uhuru waliweza kupiga picha za kumbukumbu na Odama na ilikuwa kama hivi"-

 Mtangazaji wa redio Uhuru kipindi cha Burudani Ambiance Shtuka, Cecy Jerry aka Mama Cecy au Mwasii Kitoko (kushoto) akiwa na Jeniffer Kyaka (Odama)
Mtangazaji wa redio Uhuru kipindi cha Burudani Ambiance Shtuka, Cecy Jerry aka Mama Cecy au Mwasii Kitoko (kulia) akiwa na Jeniffer Kyaka (Odama)
  Mtangazaji wa redio Uhuru kipindi cha Burudani Ambiance Shtuka, Cecy Jerry aka Mama Cecy au Mwasii Kitoko (kulia) akiwa na Jeniffer Kyaka (Odama)
Mtangazaji wa redio Uhuru kipindi cha Burudani Ambiance Shtuka, Cecy Jerry aka Mama Cecy au Mwasii Kitoko (kulia) akiwa na Jeniffer Kyaka (Odama)
 Mtangazaji wa redio Uhuru Scolastica Salim (kulia) akiwa na Odama
 Mtangazaji Neema Mwangomo (kulia) na Jennifer Kyaka (Odama)
  Mtangazaji Neema Mwangomo (kulia) na Jennifer Kyaka (Odama)
 Mtangazaji wa redio Uhuru kipindi cha Hello Tanzania, Sheila Simba (kulia)  na Jennifer Kyaka (Odama)
  Mtangazaji wa redio Uhuru kipindi cha Hello Tanzania, Sheila Simba (kulia) na Jennifer Kyaka (Odama)
 Mtangazaji wa redio Uhuru, FurahaLuhuembe (kulia) na Jennifer Kyaka (Odama)
 Mtangazaji wa redio Uhuru, FurahaLuhuembe (kulia) na Jennifer Kyaka (Odama)

Sunday, January 25, 2015

KIFO CHA MFALME ABDULLAH: NI UKUMBUSHO TOSHA MALI SI LOLOTE MBELE YA MUNGU!



Aliyebebwa na kisha kulazwa hapa ni Mfalme Abdullah wa Saudia. Aliswaliwa na kuzikwa huko Riyadh mapema wiki hii.
Kuna mengi tunajifunza kwa kifo cha Mfalme huyu wa Duniani, Allah ampe kheri na jazaa huko akhera , ameen.

Mfalme ambaye alikua na utajiri usomithilika, alikua na nguvu za kusema kile nataka hiki sitaki, alikua na uwezo mkubwa, lakini yote haya ulifika muda ikawa ni mwisho wake. Mwisho wa maamuzi. Hata akivuliwa nguo alositiriwa hana uwezo wa kukemea au kujisitiri tena.


Je, umauti hauwi sababu ya sisi kurudi kwa Mola wetu? Ewe mwenye mamlaka ya ulipo, kipi kinakupa kibri na jeuri hata unamkufuru Mungu muumba wa mbingu na ardhi, alokuumba wewe tokea tone la manii?
Mfalme amezikwa na ulimwengu umeshuhudia mazishi yake yalivyokua yakawaida kabisa, kaburi lake pia ni la kawaida mno, kaburi kama ulionavyo halijajengewa na halitajengewa.


Kaburini ni wewe na Malaika wa Allah tuu. Hapo ni matendo yako mema ndio yatakayokupa unafuu sana. Jaalia wewe ndie ulielazwa pale, jee una matendo gani ya kukuepusha na adhabu za Allah. Jee uliyoyafanya juu ya mgongo wa ardhi yatakueka mbali au kukukurubisha na moto wa Jahannam?


Hakika mauti ni glasi yenye kinywaji na kila nafsi itakunywa kinywaji hicho, hakika mauti ni mawaidha, tunatakiwa tuwaidhike nayo. Hakika mauti ni mlango, na kila mtu ataupita mlango huo. Kiukweli mauti ina majina mengi sana. Na kila jina linajitosheleza nalo. Tudumisheni matendo mema ili Allah S.W atulipe mema.

ENZI Z UHAI WAKE ALIHESHIMIKA NA VIONGOZI WAKUBWA WA DUNIA



...akiwa na Rais wa Marekani, Barack Obama


...akisalimiana na Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron


...akiongea na Rais wa Syria, Bashar al-Assad Allah anatwambia...

"Mali zoote mulizonazo ni mali zangu, na Pepo ni Pepo yangu, na nyinyi ni waja wangu, enyi waja wangu, inunueni Pepo yangu kwa mali zangu"
Je, nini tupewe kama Allah anataka tuinunue Pepo yake kwa mali zake?