INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Sunday, January 25, 2015

EDGA LUNGU ASHINDA URAIS ZAMBIA





Edga Lungu.

MGOMBEA wa Chama cha Patriotic Front, Edga Lungu ameshinda uchaguzi wa urais nchini Zambia.
Tume ya uchaguzi nchini humo imesema kuwa Lungu amepata asilimia 48 ya kura zilizopigwa.

Alikabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa mgombea wa upinzani Hakainde Hichilema.
Wagombea wote wawili walikuwa wameahidi kuboresha mifumo ya elimu na kubuni nafasi za ajira. Uchaguzi huo uliandaliwa kufuatia kifo cha rais Michael Sata aliyefariki dunia mwezi Oktoba mwaka jana

Saturday, January 24, 2015

ODAMA: ANGALIA TRAILER YA FILAMU YANGU MPYA YA JADA

Kwa
mara ya kuanza unagalia trailer ya filamu yangu ya JADA kwa kupitia
blogu yako pendwa ya Odama One. Ninawashukuru watu wote walioshirikiana
nami kumaliza zoezi la kushuti filamu yangu ya JADA ambayo ninauhakika
asilimia 100 ujumbe uliomo ndani ya filamu hii utaenda kubadilisha
maisha yako wewe.

Jeniffer Kyaka (Odama)
na mwane Jason

Filamu
yangu hii imetengezwa na kampuni yangu ya J-FILM 4 LIFE iliyopo
Kinondoni Biafra Dar es Salaam Tanzania. Katika filamu hii utaona
mabadiliko makubwa sana ya ubora (quality) katika picha, sauti, effects
na jinsi gani ujumbe ulivyomzito.

Siku ya tarehe 19.02.2015
filamu yangu itakuwa sokoni, kwahiyo unaombwa sana kama mdau wangu
kujipatia filamu hii na usikose kumjulisha na ndugu au jamaa yako wa
karibu juu ya ujio huu wa JADA.

Katika filamu hii utaweza kuona
jinsi gani mtoto anayeishi na mama wa kambo anavyokuwa mtukutu na kukosa
heshima ndani ya nyumba. Anashinda kumheshimu mama yake wa kambo
kutokana na kudekezwa  kwa baba yake. Nisikumalizie uhondo wa filamu hii
ila kwa sasa angalia trailer hili na baaada hapo kajipatie filamu yako
sokoni





Wednesday, January 21, 2015

MAMBO AMBAYO HUKUYAJUA KUHUSU STAA WA NOLLYWOOD ALIYEFARIKI, MUNA OBIEKWE


KIFO cha staa wa Nollwood, Muna Obiekwe kimezua gumzo kwa watu wengi nchini Nigeria na wengine ambao wanafuatilia tasnia ya filamu nchini Nigeria, sasa kuna mambo kadhaa ambayo yawezekana ulikuwa huyajui kuhusu staa huyo aliyefariki kutokana na matatizo ya figo.

Staa wa Nollwood, Muna Obiekwe enzi za uhai wake.

Alikuwa muoga wa waandishi wa habari
Muna hakuwa tayari kujitokeza hadharani kuomba kuchangishiwa fedha kwa kuwa alikuwa muoga wa kuonekana kwa waandishi wa habari na alipenda maisha yake binafsi yasijulikane.

Muna alikuwa mlevi
Inaelezwa kuwa alikuwa akinywa pombe sana licha ya kuwa daktari alimkataza kufanya hivyo. Alikuwa akijihudumia mwenyewe bila msaada wa watu wengine, lakini baadaye siku za mwisho za uhai wake alipata msaada mkubwa kutoka kwa Patience Ozokwor na Kanayo O.

Alimfuata Ibinabo Fiberesima
Licha ya kuwa alikuwa mtu aaibu sana, siku za mwisho za uhai wake aliwasiliana na muigizaji wa kike wa Nollywood, Ibinabo Fiberesima lakini hakuwa na msaada kwa kuwa alifariki siku chache baadaye.

Muna alijua tatizo lake siku nyingi
Alijua tatizo hilo siku nyingi lakini inaelezwa kuwa alijua atalitatua kimya kimya, aliyapuuzia maumivu aliyokuwa akiyasikia.

Muna alikuwa na mke na watoto wawili
Wengi hawakujua lakini alikuwa ni baba wa familia na mwenye watoto wawili.

ANGALIA FILAMU HII ALIYOSHIRIKI


Monday, January 19, 2015

TAARIFA: FILAMU YA MPYA YA JADA YA JENNIFER KYAKA (ODAMA) KUTOKA J-FILM 4 LIFE KUSAMBAA MITAANI SASA

Kampuni ya J-Film 4 Life ya mwanadada Jeniffer Kyaka (Odama) itaachia filamu mpya ya JADA siku ya terehe 19.02.2015. Kama tunavyomjua mwigizaji maarufu nchini Tanzania Odama ambaye kwa sasa ameamua kutoa filamu yake ya JADA kama zawadi kwako mdau wa filamu Tanzania ili uweze kuburudika na kujifunza mengi kutoka kwa mwigizaji huyu,

Katika filamu hii utaweza kuona jinsi gani mtoto anayeishi na mama wa kambo anavyoweza kuharibu ndoa ndani ya nyumba kwa vituko na udanganyifu. Mbali na hilo utaona mambo mengi sana ambayo yatakufanya wewe uweze kuwa na muonekano mpya kifikra na kimtazamo. Filamu hii itakubadilisha sana na kukuweka katika ulimwengu mwingine na uliouzoea. Hebu itazame sasa.

Pia unaweza kumuunga mkono na kuinua karama yake hii aliyopewa na mwenyezi Mungu ya uigizaji kwa kununua filamu zake zilizopo madukani kama zinavyooneka kwenye tangazo lililotengezwa na Rumafrica (+255 715 851523 www.rumaafrica.blogspot.com) hapo chini na hasa hii filamu mpya ya JADA.



ANGALIA PICHA ZA BEHIND THE SCENE ZA FILAMU YA JADA
Picha zimepigwa na Rumafrica +255 715 851 523 | www.rumaafrica.blogspot.com
























Rulea Sanga (kulia) na Wastara



























ANGALIA MATUKIO MENGINE KWA KUBONYZA "READ MORE" HAPO CHINI KIDOGO