INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Tuesday, May 31, 2016

Lazima Nimzalie Harmonize: Wolper

Jacqueline Wolper amenyanyua kinywa chake na kusema; “lazima nimzalie Harmonize (Rajabu Abdulhan, staa wa Bongo Fleva), kwa kuwa nimeridhika naye.”

Sijutii Kutembelea Bajaji: Wema Sepetu

STAA mwenye nyota ya kipekee Bongo, Wema Sepetu amewafungukia wanaomsema vibaya kuwa siku hizi kafulia mpaka anatembelea usafiri aina ya Bajaj na kudai kuwa hayo ni maisha yake binafsi ambayo hayamhusu mtu yeyote.
Akizungumza na gazeti hili juzikati, Wema alisema kuwa anashangazwa sana na watu ambao wanafuatilia maisha yake kila kona kwa kuwa yeye ni binadamu kama walivyo wengine na maisha yote anastahili kuishi.

Sikumuimbia Jokate Wimbo Wa Aje: Ali Kiba

Alikiba amesema Aje si wimbo aliomuimbia Jokate wala msichana yeyote bali aliimba kwaajili ya mashabiki wake.
“Sijamuimbia mtu yeyote kwa kweli, mi nimeimba kwa ajili ya mashabiki wangu, kwanza sijawahi kumuimbia mtu kabisa, sijawahi, so ni kwa ajili ya mashabiki wangu,” Kiba alikiambia kipindi cha Friday Night Live cha EATV.

Picha: Harmonize Amtambulisha Wolper Kwa Wazazi Wake Huko Mtwara.

Ijumaa iliyopita Harmonize alikuwa Mtwara kwenye show, hata hivyo alitumia nafasi hiyo kwenda kumtambulisha mpenzi wake mpya Jacqueleine Wolper kwa wazazi wake. Angalia picha...

Wednesday, May 25, 2016

Aunty Ezekiel Aelezea Maumivu Aliyopata Wakati Wa Kujifungua Mtoto Wake Wa Kwanza.

Msanii wa filamu Aunt Ezekiel amefunguka na kueleza jinsi alivyopitia maumivu makali wakati wa kujifungua mtoto wake wa pekee ‘Cookie’ ambaye ametimiza moja mmoja hivi karibuni.
Kupitia ukurasa wake wa instagram, Aunt Ezekiel aliandika:

JB Azitolea Nje Ofa Za Filamu Za Kinageria, Ijue Sababu.

JB si msanii anayezuzuka na filamu za Kinaijeria ndio maana amesema ameshazitolea nje ofa tatu za kuigiza filamu za Kinaijeria.
“Natoboa siri ambayo watu hawaijui, nimekataa script zaidi ya tatu Nigeria kwenda kuact kwasababu hazinilipi,” muigizaji huyo aliiambia 255 kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

Martin Kadinda Azungumzia Ugomvi Wa Mirror Na Petit Man.

Martin Kadinda amefunguka juu ya ugomvi wa Mirror na Petiti Man. Akizungumza na Enewz Kadinda alisema kuwa ugomvi wa Mirror na Meneja wake anayesimamia kazi zake za muziki yaani Petit man ni utoto tu unawasumbua.

Sababu Ya Wolper Kumbwaga Mkongo Na Kuwa Na Harmonize Ni Hii Hapa.

Mwigizaji Jackline Wolper jana amefanya mahojiano na Zamaradi Mketema kwenye kipindi cha TakeOne na kuzungumzia mambo mengi kuhusu yeye na aliyekuwa mpenzi wake Putin ‘Mkongo’ aliyemvisha pete, na uhusiano wake na msanii Harmonize.
‘Ni kweli Raj (Harmonize) ni mpenzi wangu,ukweli nilimjua siku nyingi nilikuwa nikimchukulia kama mwanamuziki tu, tuna mwezi mmoja na wiki mbili sasa’’ alisema Jack.

Mimi Ni Zaidi Ya Ray: Gabo Zigamba

Msanii wa filamu nchini ambaye anafahamika kwa kuigiza kwa lafudhi ya Kimakonde Gambo Zigamba amefunguka na kusema kuwa yeye ni zaidi ya msanii Ray Kigosi kwenye kazi kwani yeye anafanya zaidi ya Ray.
Akizungumza kwenye kipindi cha eNewz Gambo Zigamba aliweka wazi kuwa kipindi ambacho wakina Ray na wasanii wengine wakongwe wanafanya kazi zao hizo kulikuwa hakuna wasanii wengine wachanga ndiyo maana walikuwa wanaonekani ni wazuri sana lakini hivi sasa tasnia imekuwa na vipaji vipya ambavyo vinafanya vizuri zaidi yao hao wakongwe.

Ali Kiba Amuombea Kura Diamond BET Awards.

Msanii Alikiba amefunguka na kusema kwa mafanikio aliyopata toka amerudi kwenye muziki tena ndani ya muda ni mfupi ni sawa na kuchana msamba kwake maana siyo hatua za kawaida.
Alikiba alisema haya kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio na kusisitiza kuwa yeye kusaini mkataba na kampuni ya ‘Sony Music’ jambo kubwa sana katika maisha yake ya muziki.
“Kiukweli toka nimerudi rasmi kwenye game na kutoa wimbo wa Mwana mashabiki walipokea vizuri sana Africa Mashariki, na kadili nilivyokuja kutoa wimbo mwingine wa Chekecha walizidi kuongezeka mashabiki na kujiona nina mashabiki wengi, hivyo kuja kusaini mkataba na ‘Sony Music’ ndani ya muda mfupi hivi kwangu mimi najiona ni kama nimepiga msamba maana siyo hatua za kawaida” alisema Alikiba.

Tuesday, May 24, 2016

Picha: Wema Sepetu Azindua Application Yake Ya Simu.

Jana Wema Sepetu Alizindua application yake ya simu kwa ajili ya kuwa karibu na amshabiki wake. uzinduzi huo ulihudhuriwa pia na waziri wa sanaaa, utamaduni na michezo Nape Nnauye. Hizi ni picha toka kwenye event hiyo...

Friday, May 20, 2016

Zari Na Mama Diamond Watifuana ?

Inadaiwa ilitokea lakini haikuandikwa! Kuna habari kuwa, ile safari ya familia ya nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kula bata kwenye nchi za Ulaya, ilikuwa na mambo mengi lakini kubwa ni madai ya kuwepo kwa mtifuano kati ya mama Diamond, Sanura Kasim na Zarinah Hassan ‘Zari’ ambaye ni mzazi mwenzake, Diamond.
Kwa mujibu wa chanzo, mtifuano kati ya Zari na mkwewe huyo ulitokea baada ya siku moja mkwe huyo kuteleza kwenye ngazi za umeme wakiwa wanapanda, Zari akamuwahi kwa kumshika mkono hali iliyomtibua mama huyo.

Rose Ndauka Aelezea Siri Ya Mafanikio Yake.

MKALI wa filamu Bongo, Rose Ndauka ametoa siri ya mambo yake kumnyookea kuwa imetokana na kumuhusisha Mungu kwa kila anachokifanya na wala si vinginevyo kama watu wanavyodhania.
Akizungumza na Amani, Rose ambaye kwa sasa anamiliki kampuni inayojishughulisha na kutengeneza Jarida la Rozzie, alisema kuwa Mungu ndiye aliyemtendea miujiza hiyo kwani asingemshirikisha asingekuwa hapo alipo.

Wema Sepetu Amfungukia Ali Kiba.

Msanii wa filamu nchini Wema Sepetu amefunguka na kusema kuwa msanii Alikiba ni mtu wa kumuacha kutokana na uwezo wake wa kuimba na namna ambavyo anaweza kuipangilia sauti yake kwenye muziki.
Wema Sepetu amezidi kuonyesha mapenzi aliyonayo kwenye kazi za msanii Alikiba na kusema huwa zinamkosha sana na kudai hajawahi kumuangusha siku zote

Monday, May 9, 2016

Harmonize Afunguka Baada Ya Kuzawadiwa Gari.

Msanii ambaye yupo chini ya Label ya WCB, Harmonize jana amezawadia gari aina ya Mark X na uongozi wake wa WCB kama motisha kwa kazi zake lakini pia kama njia ya kumrahisishia usafiri na kulinda jina lake na hadhi yake.
Baada ya kupewa zawadi hiyo ya gari msanii huyo alikuwa na maneno ya shukrani kwa uongozi wake huo na kusema kuwa kitendo hicho kimemfanya awe na furaha ambayo hajawahi kuwa nayo.

Diamond Ni Mshikaji Wangu Ila Simtegemei: Shetta

Msanii Shettah ambaye kwa sasa ameachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Namjua’ amefunguka na kusema kuwa yeye na msanii Diamond Platnumz ni washikaji sana na marafiki wa karibu sana ila inapokuja suala la kazi Shettah anasimama kama Shettah.
Shettah alifunguka hayo kupitia show ya Friday Night Live inayorushwa na EATV kila siku ya Ijumaa na kudai kuwa kwenye masuala ya muziki yeye anasimama kama yeye japo muda mwingine watu hao wamekuwa mchango katika kumbadilisha kutoka kwenye kuchana mpaka sasa anaimba ngoma kama hizo.
“Unajua Diamond Platnumz ni mshikaji sana na mtu wangu wa karibu sana ila inapokuja kwenye masuala ya kazi mimi kama Shettah nasimama mimi kama mimi na ndiyo maana unaona nina Management yangu tofauti na muda si mrefu huenda na mimi nikawa na wasanii nawasimamia kwani kwa sasa siwezi kushindwa kumfanyia msanii kazi na kumtolea pesa ya video lakini nataka nijipange zaidi na team yangu” alisema Shettah
Mbali na hilo Shettah amekiri wazi kuwa katika wimbo wake wa sasa ‘Namjua’ kuna michango ya watu mbalimbali katika kuifanya kazi hiyo isimame na kusema zipo hata melody za Diamond Platnumz ndani ya wimbo huo yaani alimuelekeza labda sehemu hii Shettah pita hivi hapa fanya hivi.
eatv.tv

Siwezi Kumhukumu Nay Wa Mitego: Shamsa Ford

STAA wa Bongo Muvi, Shamsa Ford kwa mara ya kwanza ameibuka na kuiongelea Ngoma ya Shika Adabu Yako iliyoimbwa na Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ kuwa kamwe hawezi kumhukumu Nay kwa maneno aliyoimba.

Ray Kucheza Filamu Nchini Rwanda.

Msanii wa filamu nchini Vicent Kigosi amefunguka na kusema kuwa yeye ni msanii pekee kutoka Tanzania ambaye amechaguliwa kushiriki katika filamu inayounganisha nchi mbili ya Rwanda na Tanzania.
Ray Kigosi kupitia mtandao wake wa kijamii aliandika kuwa kwa nafasi aliyopata hawezi kuwaangusha watanzania kwani yeye amekwenda kuwaonyesha kazi.

Tuesday, May 3, 2016

TID Afungukia Penzi Lake Na Wema Sepetu.

Msanii mkongwe wa muziki, TID amesema kipindi cha nyuma alikuwa anatoka kimapenzi na malkia wa filamu Wema Sepetu lakini baadae alitemwa hali ambayo ilimuumiza sana.
Akizungumza katika kipindi cha Clouds TV Ijumaa hii, TID amesema hali hiyo ilimfanya atoke na wasichana wengi.
“Nilikuwa ‘namdate’ Wema Sepetu akaniambia sikutaaki, tangu kipindi hicho nimekuwa na wasichana wengi. Ikitokea Wema anataka kurudi hakuna nafasi, I’m occupied,” alisema TID.

Sipendi Kuanika Mali Zangu Mitandaoni: Irene Uwoya

MSANII wa filamu za nchini, Irene Uwoya, amefunguka na kusema hapendi kuweka wazi mambo yake binafsi kama ilivyo wasanii wengine.
Msanii huyo alisema kuwa kuna baadhi ya wasanii ambao wanapenda kuweka kila kitu chake ambapo haina maana yoyote kwa jamii.

Mzee Majuto Atangaza Kuacha Kuigiza.

Mzee Majuto amesema kuwa kwa sasa anaamini anaweza kuishi bila kutumia kipaji chake hicho cha ugizaji na muda huu atatumia kumuomba Mungu amasamehe makosa aliyotenda na kudai kuwa anaamini itawezekana kwani Mungu ndiye anayetoa ridhiki kwa kila mtu.