INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Tuesday, July 31, 2012

AUNTY EZEKIEL KUFUNGA NDOA MWEZI OCTOBER



ILE kasumba kwamba hakuna msanii wa bongo muvi anayeweza kuolewa na kudumu ndani ya ndoa, inatarajia kufutwa na msanii Aunty Ezekiel, ambaye anatarajia kufunga ndoa mwezi October mwaka huu, na mpenzi wake anayeishi Dubai ambako ndiko atakoenda kuishi baada ya kufunga ndoa.

Mtandao
, ulifanya mazungumzo mafupi na msanii huyo juu ya maisha yake na filamu kwa ujumla ambapo, alisema kuwa ameamua kuchukua maamuzi hayo ya kutaka kufunga ndoa kwani anahitaji kuishi na mtu ambaye wataweza kupanga naye maisha.

Alidai kuwa mpenzi wake huyo ni Mtanzania ingawa anaishi nje, ambapo anaamini baada ya kufunga ndoa na yeye anataweza kwenda kufanya kazi huko.


“Nilikuwa kimya juu ishu hii lakini nachotaka kusema ni kwamba mambo yangu sasa yameanza na nimeamua kufunga ndoa, hivyo mashabiki wangu nahitaji nao waweze kujua kuwa sasa nimeamua kuchukua maamuzi hayo,”
alisema.

Ezekiel alisema kuwa vikao vya harusi na kupanga itakavyokuwa wameshaaza kukaa, kwani wameanza Jumapili.


Aliongeza kuwa mbali na mchakato huo mkubwa pia mwaka huu wa 2012 kampuni yake inatarajia kufunga mwaka kwa kutoa filamu mbili ambazo anaamini zitakuwa moto wa kuotea mbali.

Monday, July 30, 2012

WEMA KUMRUDIA MAMA YAKE TENA!

KATIKA kukamilisha mfungo wake wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ amekubali kupatanishwa na mama yake mzazi, Miriam Sepetu, hivyo kukamilisha usemi kuwa mtoto hakui kwa mzazi wake, Kwa mujibu wa chanzo cha karibu na Wema, baada ya staa huyo kutofautiana na mama yake kisa kikiwa ni mahojiano aliyofanya mzazi huyo runingani ambayo hayakumpendeza Wema, hivi karibuni wamekutanishwa na kurejesha amani iliyokuwa imetoweka kati yao.

“Mimi najua undani wa ishu nzima, tangu yale mahojiano na nyiye (Global) mkaandika kuwa mama Wema alimtia aibu mwanaye, hali ilikuwa mbaya hadi juzi walipopatanishwa ndiyo wamerudisha ushosti wao,” kilisema chanzo hicho.


WAZEE WAWAPATANISHA

Chanzo chetu kilidadavua kuwa pamoja na Wema kwenda kumwangukia mama’ke, kuna wazee ambao walitinga nyumbani kwa Wema, Kijitonyama ‘Hollywood’, Dar waliotoka upande wa mzazi huyo ambao walikwenda kumsihi afanye hivyo.

“Hazikuwa jitihada zake peke yake za kutaka kumaliza tofauti kati yake na mama’ke bali wale wazee takriban wanne walizungumza na Wema na kumwelekeza namna ya kumaliza tofauti zake na mzaa chema huyo,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:

“Hao wazee ndiyo waliwakutanisha kwa mama Wema, Sinza-Mori, Dar na kumaliza chokochoko zote na sasa Wema na mama’ke mambo ni ‘mswaano’.


HALI ILIKUWA MBAYA SANA
Chanzo hicho kiliendelea kushusha data kuwa kulikuwa na ulazima wa Wema kutinga kwa mama’ke na kumwangukia kwani suala hilo lilikuwa likimpasua kichwa na kusababisha hali kuwa mbaya kati ya wawili hao kwa sababu hakukuwa hata na salamu.


WEMA ASHINDA KWA MAMA’KE
Baada ya kusikiliza maelezo hayo kutoka kwa chanzo, Julai 23, mwaka huu saa 5 na sekunde 35 asubuhi, Ijumaa lilizungumza na Wema kutaka kujua alikuwa wapi wakati huo ambapo alijibu kuwa anaenda kwa dada yake kumchukua mtoto aliyemtaja kwa jina la Sasha kisha kwenda kushinda naye Sinza-Mori kwa mama yake.

Alipoulizwa kama ni kweli kuna wazee walimfuata na kumpatanisha na mama yake, staa huyo wa muvi ya Super Star itakayoingia sokoni Agosti alikiri kutokea kwa suala hilo.


HUKO NYUMA
Wiki kadhaa zilizopita, Wema na mama yake walitibuana baada ya mzazi huyo kuwatemea mbovu mashosti wa mwigizaji huyo alipokuwa akihojiwa runingani.

JACK PATRICK AACHIA PICHA NYINGINE MBAYA

MLIMBWENDE mtata Bongo, Jacqueline Patrick, kama kawa, amedondosha picha nyingine chafu kwenye ‘peji’ yake ya mtandao wa BBM.

Jack ambaye ni mke wa mfanyabiashara Abdulatif Fundikira alitupia picha hizo Julai 25, mwaka huu huku akizisindikizia na ujumbe usemao ‘sina tatizo na mtu na mwenye macho haambiwi tazama.’

Picha hizo zimezua maswali mengi kwa watu wake wa karibu ambao wengi ni waumini wa dini ya kisilam ambao kwa mwezi huu wapo ndani ya swaumu.

Wengi walihoji nini kilimfanya staa huyo kuweka picha hizo chafu sana zenye kumwonesha kila kitu huku akiwa ameolewa kwa ndoa! “Au yuko sokoni zaidi?” alihoji mdau wake mmoja.

Jack bila kujali hilo aliendelea kuanika picha hizo kwa kubadilisha moja baada ya nyingine kulingana na mapozi aliyotaka mwenyewe

ANGALIA ZAIDI. BOFYA HAPO CHINI

BILA MILIONI TATU HUJAMPATA SHILOLE


 
Ikiwa ni tofauti na wasanii wengine, mwanamuziki na muigizaji huyu amejiwekea kiwango chake cha shoo pamoja na uigizaji kwamba yeye anapatikana kwa kiwango cha juu cha milioni tatu.

"Mimi ni msanii ambaye ninajiamini na kile ninachokifanya, kwakuwa naamini nipo katika soko kwa sasa, mimi hunipati bila milioni tatu, ingawaje naweza kupunguza lakini hicho ndio kiwango kinachofahamika" anasema Shilole.

Anaongeza kuwa licha ya shoo nono anazozipata, katika kalenda yake ameshakuwa na shoo kadhaa ambazo anatarajia kuzifanya hapo baadaye "mpaka sasa nina shoo zaidi ya tatu kwa wiki hivyo kwa mwezi ninapata shoo zaidi ya 12 na wakati mwingine zinabebana shoo mbili kwa siku moja" anafafanua muigizaji huyo.

Licha ya kazi anazozifanya msanii huyu ambazo zipo machoni mwa mashabiki wake, Shilole ni mjasiliamali ambaye anafanya kazi mbalimbali ikiwemo kumiliki duka la nguo lililopo maeneo ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Ikiwa ni mwezi mtukufu wa ramadhani, Shilole hivi sasa amesimama kazi zingine na kwa sasa anauza duka na kurekodi kazi kazi zake za muziki mpaka hapo mfungo wa mwezi wa Ramadhani utakapokwisha.

"Katika kipindi hiki nipo bize na kazi zingine, kuna baadhi ya kazi zangu za ujasiriamali mbalimbali ambazo nimesimama kwa wakati huu, na sasa nauza duka na kazi za kurekodi za muziki na hivi karibuni watu watarajie kupata wimbo wangu mpya wa Dudu niliouimba nikiwa na Q Chief" anasema Shilole.

Shilole anasema katika maisha yake ana matarajio ya kuja kuwa msanii mkubwa na mwenye ubunifu kama ilivyo kwa wasanii wa nchi za ughaibuni.

"Unajua ukifika Hollywood unakutana na msanii ambaye ana fanya kazi zaidi ya moja, si kwamba anatumbukia tu ila kipaji kinazingatiwa zaidi na hivi ndivyo alivyo shilole" anajinadi huku akisisitiza kuwa sanaa pekee haitoshi katika maisha yake, ila ujasiriamali ndio nguzo anayoitegemea zaidi ili kuyafikia malengo yake.

Source: Vituko vya Mtaaa

Sunday, July 29, 2012

LIZZY ANJORINI - SITEMBEI NA MUME WA MTU

BINTI mrembo ambaye ni mwigizaji wa Nollywood, Lizzy Anjorin amekanusha habari zilizoenea kwamba ana uhusiano wa kimapenzi na mume wa staa mwenzie Funke Akindele.

Msanii huyo alidai kuwa tuhuma hizo zimemdhalilisha na anaangalia uwezekano wa kuyashtaki magazeti yaliyomtuhumu na kumshushia heshima. Habari hizo zilienezwa kwenye mitandao mingi ya kijamii nchini Nigeria na Ghana wiki moja iliyopita.

Msanii huyo aliyefungua Supamaketi mpya jijini Lagos, alisema; "Hii inanishangaza sana, nashangaa kwanini watu hawataki kuniacha na maisha yangu, simjui hata huyo mume wa Funke na wala sijawahi hata kumpitia karibu sehemu yoyote ile."

"Wala kwenye harusi yao sikwenda wala sina hata namba zake. Nimechoka sasa inabidi nichukue hatua za kisheria zaidi, nataka waniache na maisha yangu, wasieneze mambo ambayo si ya kweli kwa jamii," alicharuka Lizzy.

RAY AWAPA KWELI MA-MISS WANAOKIMBILIA KWENYE TASNIA YA UIGIZAJI

IDADI kubwa ya warembo wanaofanya filamu ndani ya bongo ni wale waliopita katika mashindano ya ulimbwende iwe wa vitongoji au Taifa, ambapo msanii nguli ndani ya tasnia hiyo Vicent Kigosi ‘Ray’, ametoa somo kwa warembo wengine kuwa wasifikilie tasnia hiyo ni kimbilio lao baada ya kutoka kwenye mashindano yao.

Ray alikaririwa na mwandishi wa DarTalk, akidai kuwa anaamini Tanzania inaweza kupata wanamitindo wazuri lakini anashindwa kuelewa ni kwanini wengi wanakimbilia kufanya filamu baada ya kutoka kwenye mashindano ya U-miss.

Alidai kuwa inawezekana tasnia hiyo ya filamu haina thamani kwani kila mrembo aliyepitia mashindano ya U-miss, baada ya kutoka huko basi anaingia kwenye filamu na kuachana na fani yake ambayo wenda ingeweza kuwa ndio fani yake.

Aliongeza kuwa kila mrembo anayeingia kwenye filamu anadai kuwa fani hiyo ya uigizaji ipo ndani ya damu, hapo ndipo anaposhindwa
kuelewa kwamba kama filamu ni fani inakuwaje aliingia kwenye kwenye ulimbwende on the first place.

“Nawaomba tu warembo wanaotokea kwenye fani hiyo, kama kweli wanahitaji kuliwakilisha vyema taifa letu basi wakaze buti kwenye fani hiyo kwani ni kitu cha aibu sana wanaposhindwa huko na kuja huku kwenye filamu, wanakosa muelekeo”. alisema

Ishu hiyo ndiyo inayofanya hadi tasnia ya filamu Tanzania ishindwe kupiga hatua kwani matatizo kibao yanayotokea ndani ya tasnia hiyo yanasababishwa na wasanii waliotokea kwenye U-miss.

Saturday, July 28, 2012

HEMED WA GONGO MOVIE: "NISHATEMBEA NA WANAWAKE MASTAA 32 HIVI"

Source: Bongo flava tz
Kwanza kwa kuanza ningependa kumshukuru Hemed suleiman kwa kuwa mmoja kati ya wavaaji wazuri wa Single buttons ninazozitengeza... picha zote unaziona ni amevalishwa na Martin kadinda..... turudi katika swala zima ambalo limenifanya kuandika Post hii.... Nilitaka kujua ni vijana wangapi watuamiji wazuri wa condoms hasa kwa vijana maarufu. Mtu wangu wa kwanza amekuwa Hemed Suleiman aliniambia: "we jamaa maswali gani hayo bana? mimi kondomu za nini? muda wote mimi nakwenda dry... anakaongezea kuwa alikuwa katika mahusiano na msichana mmoja ambaye hajataka kumtaja na anasema kwa sasa wameachana imepita miezi 3... anasema aliwa kupima nae virusi vya ukimwi na walipojikuta wako safi wakaamua kujilipua kavu kavu....

Alinichosha na majibu yake ikanibidi nihamie katika swali la pili: ambapo nilimuuliza kama amewahi kuwa katika mahusiano na wasichana wa Kitanzania maarufu?



SINA LA KUONGEZA HAPO.



HEMED: Marti Martin...... unauliza kengele kanisani??? unadhani kwanini naitwa Hemed PHD? nina taaluma ya kucheza na mioyo ya mabinti hawa wakibongo.... ila tatizo hawanivutii huwa napita tu kwakuwa nina hamu na wakati huo au ninakuwa sipo katika mahusiano na mtu yoyote....

MIMI: Duuh kwahiyo ushampitia nani hii..........?? na nanihiiii........??
HEMED: hilo sio swali... mpaka sasa nishawapitia 32... kwahiyo kuhusu majina katafute mwenyewe huko mtaani mbona stori zipo??

Thursday, July 26, 2012

MWEZI MTUKUFU WAMTEGA NISHA

 Salma Jabu ‘Nisha’.

MSANII kunako anga la sinema za Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ ameweka ‘plain’ kuwa yupo katika wakati mgumu kwani Mwezi Mtukufu wa Ramadhan umemtega kwa vile mapenzi yake na jamaa anayedaiwa kuwa ni mume wa mtu ndiyo kwanza yameanza.
Akijilipua kwa Motomoto Newz, Nisha alisema katika kipindi hiki cha swaumu analazimika kukaa mbali na mwanaume huyo kwa sababu si wanandoa.
“Huu ni mtihani jamani lakini sina jinsi, acha nifunge nisije nikaharibu swaumu yangu bure, ila nitamshauri tukimaliza mfungo anioe kabisa,” alisema Nisha.

Wednesday, July 25, 2012

ODAMA ASEMA, FILAMU YA HOUSE MAID IKO SOKONI. JIPANGE MDAU WANU

Filamu ya HOUSE MAID sasa iko sokoni.
Siku ya Ijumaa ndio siku ambayo filamu hii iliingia sokoni.
Hujachelewa, nenda kajipatie nakala yako na ikiwezekana mnunulie na ndugu yako au jamaa jako.  Na kama hutaweza kumnunulia upigie simu na umweleze kuwa Odama ametoa filamu nyingine. Ukifanya hivyo utakuwa umechangia kumuinua Odama na kampuni yake ya J-4 LIFE.

Ndani ya filamu hii utajifunza mengi na mbali na mafunzo itakuadibisha na kukuelimisha.
Huu ni ujio mwingine mpya wa Odama ambao hujawahi kuona katika filamu zilizopita.

Filamu hii inaandaliwa na kampuni yangu ya J-FILM 4 LIFE kwa viwango vya hali ya juu sana.

Ukitaka kuangalia Trailer bofya hapo juu na utaona utamu uliomo ndani ya filamu




NGOZI YANGU INANIPAAISHA NA KUPENDWA-AUNT EZEKIEL ASEMA


MSANII na mtayarishaji wa filamu za Swahiliwood, Aunty Ezekiel, amesema kuwa matokeo ya kuilinda ngozi yake kwa kutotumia ovyo vipodozi, yamekuwa na faida kubwa kwake.

Anasema kwa umakini huo, ngozi yake ina mwonekano wa kuvutia hivyo kumpa nafasi kubwa ya kupata kazi katika tasnia hiyo.

"Katika maisha yangu, ngozi ina thamani kubwa. Huwa nailinda isidhurike na kemikali, vipodozi vyangu ni vya kawaida kabisa," alisema baada ya kuchaguliwa kuwa balozi wa ZUKU.

"Situmii kemikali kabisa na sina gharama kama wengine, najivunia mwonekano wangu wenye kuvutia pamoja na kuwa na uwezo wa kuigiza, ndiyo maana nawashika wapenzi wa filamu.
"
Msanii huyo pamoja na Jacob Stephen walichaguliwa kuwa mabalozi wa Zuku Swahili Movie inayotarajia kuzinduliwa mwezi ujao.

Kwa ubalozi huo, wanatarajiwa kupata mikataba ya matangazo itakayohusu bidhaa za kampuni hiyo pia kushiriki katika kampeni mbalimbali za filamu

ZITTO AREJESHA PENZI LA WEMA, DIAMOND ???






MBUNGE wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, ametajwa kuwa kichocheo cha kurejea kwa penzi la vijana wenye umaarufu mkubwa nchini kwa sasa, Nasibu Abdu Juma ‘Diamond’ na Wema Isaac Sepetu.

Uwazi, lina mkanda wa video, unaowaonesha Diamond na Wema pamoja kwa mara ya kwanza, baada ya muda mrefu wa kutupiana maneno mengi ya kashfa, huku kila upande ukimshusha hadhi mwenzake.
Diamond na Wema, walinaswa kwenye Tamasha la Kigoma All Stars, lililoandaliwa na Zitto kisha kufanyika Julai 17, mwaka huu kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.
Shukurani kwa Zitto, kwani kupitia tamasha hilo, Diamond na Wema, waliweza kudhihirisha kwa kila mtu kwamba uhusiano wao sasa umerejea upya kwa kuambatana kimahaba ndani ya Mkoa wa Kigoma.
SAFARI ILIVYOKUWA TAMU
Watu wengi wakijua kwamba kuna uhasama mkubwa kati ya Wema na Diamond, Julai 17, mwaka huu, ilikuwa ni mshangao wa aina yake kwa waliokuwepo Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Kigoma, baada ya vijana hao kushuka wakiwa wameongozana.

Diamond akiwa amevaa shati jekundu na tai nyeusi, chini akiondokea suruali ya jeans rangi ya bluu iliyopaushwa kimodo, huku Wema akitokelezea kwa koti la rangi ya maziwa, ndani blauzi nyeusi, halafu wote wameyaficha macho yao kwa miwani nyeusi, waliwaka vilivyo ndani ya Ujiji, Kigoma.
Baada ya kuwasili Kigoma, Wema na Diamond walielekea Hoteli ya Tanganyika Beach (ipo ufukweni mwa Ziwa Tanganyika) ambako walipata pumziko walilohitaji kabla ya nyota huyo wa wimbo wa Mbagala, hajaelekea Uwanja wa Lake Tanganyika kwenye Tamasha la Kigoma All Stars a.k.a Leka Dutigite.
WEMA ALIFUATA NINI KIGOMA?
Minong’ono ilitawala kila kona ya Mkoa wa Kigoma kwamba Wema amekwenda kuwakilisha Leka Dutigite, hivyo wakataraji kumuona Uwanja wa Lake Tanganyika, akitoa sapoti yake kwenye tamasha hilo.
Wapo ambao waliacha shughuli zao kwa ajili ya kwenda kumuona Wema tu uwanjani lakini waliambulia patupu, kwani mrembo huyo hakuonekana kabisa.
Kutokana na hali hiyo, wale waliovumisha stori kwamba Wema amekwenda Kigoma a.k.a Lwama, walionekana wazushi wasiofaa kusikilizwa, bila kujua kwamba mtoto alijificha ndani ya Hoteli ya Lake Tanganyika Beach.
HAKIKA WANAPENDANA
Kama ukaribu wao ulisababishwa na tamasha lililoandaliwa na Zitto peke yake, basi wangekuwa na muonekano ‘feki’ sehemu chache wanazopita lakini kinyume chake wao walithibitisha wanapendana haswaa!

Diamond, alishindwa kujichanganya na wasanii wenzake aliokuwa nao kwenye shoo ya Kigoma kama akina Said Juma ‘Chegge’, Peter Msechu, Banana Zorro, Mwasiti Almasi na wengineo, badala yake muda mwingi aliutumia kuwa umbali wa mita sifuri kutoka alipo Wema.
‘Mtundu’ wa nyimbo mbili mpaka sasa, Nai Nai na Baadaye, Omar Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, ndiye pekee aliyekuwa jirani na vijana hao maarufu, walioamua kurejesha penzi lao kupitia mwavuli wa shoo hiyo.

Kwa upande mwingine, ni kama vile waliamua kwenda kufanya tambiko nyumbani asili kwa mume mtarajiwa, yaani Diamond kwa sababu chimbuko la Wema ni Mkoa wa Tabora, japo baba yake, Balozi Isaac Abraham Sepetu, amejichimbia Zanzibar kwa miaka mingi.
Mtu mmoja, mwenye hulka ya kutopitwa na mambo, akamueleza ripota wetu kuwa Julai 18, wasanii hao walikwenda Hifadhi za Gombe na Mahale, mkoani humo lakini jioni yake, Diamond aliongozana na Wema mpaka kwa babu yake, eneo la Ujiji Posta, mkoani humo ambako walisomewa dua na Babu Nasibu.
RAHA NDANI YA TILAPIA HOTEL
Safari ya furaha kwa Wema na Diamond, ilihamia ndani ya Jiji la Miamba ya Mawe, Mwanza ‘Rocky City’ kwenye Hoteli ya Tilapia, iliyopo ufukweni mwa Ziwa Victoria, eneo la Capri Point, hiyo ikiwa Julai 19, 2012.

Habari zinapasha kuwa wawili hao, walipumzika kwenye hoteli hiyo kwa muda mfupi, wakati wanasubiri saa ya ndege yao ya kuwatoa Mwanza hadi Dar es Salaam ifike.

Ndege waliyopanda Diamond na Wema kutoka Kigoma, ilitua Mwanza saa 9:30 alasiri, hivyo kuanzia muda huo, waliutumia Tilapia Hotel mpaka saa 2:30 usiku, wakaripoti Uwanja wa Ndege wa Jiji la Miamba ya Mawe, kabla ya saa 3:50 usiku, usafiri huo wa anga, uliitupa mkono ardhi ya Mwanza mpaka Dar es Salaam.
AIR PORT DAR ES SALAAM
Mama mzazi wa Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra Sammi’, alionekana Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, kuanzia saa 4:45 usiku (Julai 19), hivyo kwa jicho la ripota wetu, ikawa wazi kwamba amekwenda hapo kumpokea mwanaye kipenzi, Diamond ‘Sukari ya Warembo’.

Kutokana na safari hiyo kuwa mguu wa Diamond uliambatana na wa Wema, kwenda kwenye shoo ya kutoa shukurani nyumbani kwao Kigoma, ni wazi Mama Nasibu (Mama Diamond) alikuwa pale pia kwa minajili ya kumlaki mkwe a.k.a Mka Mwana.
PW 415 YAWASILI DAR
Diamond na Wema, walipanda ndege ya Kampuni ya Precision Air, PW415 na ilipotimia saa 5:30 usiku, ilitangazwa kuwa ndiyo inawasili kwenye uwanja huo wa ndege wenye jina la muasisi wa taifa huru la Tanganyika na baadaye Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ‘Baba wa Taifa’.
Milango ya saa 5:52, Diamond na Wema, walipita kwenye mlango wa wanaowasili (arrivals gate), wakiwa sambamba na Ommy Dimpoz, walipokelewa na Mama Nasibu hadi sehemu ya maegesho ya magari uwanjani hapo.

Timu nzima, ilijipakia kwenye gari la Diamond aina Toyota Land Cruiser Prado, rangi ya fedha, wakatoweka eneo la uwanja huo.
DIAMOND KWA WASIWASI
Saa 6:14 usiku (Julai 20), Diamond alimpigia simu ripota wetu, eti akahoji kilichompeleka uwanja wa ndege. Mahojiano yalikuwa hivi;
DIAMOND: Kiongozi nilikuona Air Port, pale ulikuwa unafanya nini?
RIPOTA: Aah, kumbe uliniona? Mlivyojikausha nikadhani hamkuniona. Kuna mzigo wangu nilikuwa naufuatilia pale.
DIAMOND: Mzigo wapi? Naomba uniambie ukweli.
RIPOTA: Acha hizo dogo, unafikiri mimi nilikufuata wewe? Tena ningejua unafika leo, halafu ujio wenyewe ni huo, ningetega kamera zangu na tuwapige picha za kutosha.
DIAMOND: Aah, usifanye hivyo kiongozi.
Baada ya mazungumzo hayo, Diamond kila alipopigiwa simu hakupokea mpaka gazeti hili linanyanyuka kwenda kiwandani.
UFAFANUZI WA WEMA
Wema alipopigiwa simu na ripota wetu, alijibu kuwa yeye na Diamond hawajarudisha mapenzi, isipokuwa hivi sasa wako karibu kama marafiki wazuri kwa ajili ya kusaidiana mambo mbalimbali.
“Kusema ukweli kwa sasa sijafikiria kurejesha mapenzi na Diamond ila tupo karibu kama marafiki,” alisema Wema.
ZITTO NAYE
Jitihada za kumpata Zitto aweze kuzungumzia kurejea kwa penzi la Wema na Diamond kwenye tamasha aliloliandaa, hazikuzaa matunda. Muda wote naibu huyo wa Kambi ya Upinzania Bungeni, simu yake ilikuwa imezimwa.
WANANCHI WAMPONGEZA
Fununu kuwa Wema na Diamond wamerudiana zilivuma kwa kasi ndani ya mitandao ya kijamii na maoni ya wengi yakaelekeza pongezi kwa Zitto, kwani kabla ya hapo, mastaa hao walikuwa na uhasama mkubwa.
UNAKUMBUKA?
Malumbano yao kwenye vyombo vya habari? Diamond alipomfedhehesha Wema baada ya kukataa kupokea fedha zake alizomtuza kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam Machi mwaka huu? Je, kauli nzito za Mama Wema, Mariam Sepetu kwamba Diamond ni kijana mbaya na hafai?
JIULIZE SASA
Mpaka hapo bado unabisha kwamba mapenzi ni upofu? Unaendelea kukataa kwamba mapenzi hayaulizwi kwa nini? Diamond alipoachana Wema, alitua kwa Miss Tanzania namba mbili 2006-07, Jokate Mwegelo, je, penzi lao limeyeyuka au bado lipo kwa sura gani?

KAJALA ATOA MACHOZI KATIKA BIRTHDAY YAKE SEGEREA GEREZANI



JUMAPILI ya Julai 22, mwaka huu ilikuwa ni siku ya kuzaliwa kwa msanii wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja (pichani), staa huyo alisheherekea siku yake hiyo kwa majonzi akiwa katika Gereza la Segerea jijini Dar  huku vilio vikitawala.
‘Bethdei’ hiyo ilifanyika Jumapili ambapo baadhi ya wasanii walifika katika gerezani  kwa ajili ya kumpelekea zawadi mbalimbali huku wakimwimbia Kajala wimbo maarufu wa ‘Happy Birthday’  wakati staa huyo akiwa nyuma ya nondo.
Baadhi ya watu waliofika gerezani hapo kwa ajili ya kuungana naye katika kusheherekea ni pamoja na mtoto wake Paula, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, Bilaly Mashauzi pamoja na Jeniffer Pemba.
JENIFFER AKABIDHI KEKI
Dada huyo ambaye ni rafiki wa karibu na Kajala ambaye pia ndiye mwenye jukumu la kumpelekea chakula kila siku, Jumapili iliyopita aliandaa keki ya nguvu pamoja na zawadi nyingine kwa ajili ya sherehe ya Kajala, bitu hivyo vilipokelewa na askari wa magereza na kukaguliwa kisha kufikishwa kwa mlengwa.
LULU AJUMUIKA
Baada ya muda mfupi staa mwingine anayetajwa kwenye kifo Steven Kanumba Elizabeth Michael ‘Lulu’ naye alijumuika na Kajala kusimama nyuma ya nondo kwa ajili ya kusheherekea bethdei hiyo pamoja na kuwasalimia watu waliofika ambapo wote walionekana kufarijika na ujio wao.
VILIO VYATAWALA
Hata hivyo, tofauti na ilivyotegemewa  kwani vilio vilichukua nafasi gerezani hapo kutokana hali ilivyokuwa kwani Kajala na Lulu hawakuweza kuungana na wapendwa wao kusheherekea pamoja kutokana na sheria za Jeshi la Magereza kutoruhusu tendo hilo.
SHILOLE ALALAMA
Kwa upande wake, Shilole mbali na kushiriki kuangusha kilio lakini alikuwa akilalamika kwamba yupo katika wakati mgumu na haoni raha ya  mwezi mtukufu wa Ramadhan kwa kuwa mwaka jana aliwaalika Kajala na Lulu wakala futari pamoja nyumbani kwake.
 “Sina budi kuwaombe dua katika mfungo huu wa Ramadhan ili Mungu awajalie waweze kutoka na tuungane tena kama zamani,” alisema.

SAJUKI APATA GONJWA BAYA LAMSHAMBULIA UTI WA MGONGO

 

Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’.
 
Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ akiwa na mkewe Wastara.

PAMOJA na kwamba afya ya staa wa filamu Bongo, Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ inaendelea vizuri, imegundulika kuwa ana ugonjwa mwingine tofauti na ule uliompeleka India kufanyiwa upasuaji,
Hivi karibuni, Sajuki alirejea kutoka nchini India alipokwenda kwa ajili ya matibabu ambapo alionekana kuwa na mabadiliko makubwa kiafya jambo lililowapa matumaini mashabiki wake.

HABARI MEZANI
Akizungumza na waandishi wetu, juzi, Jumapili nyumbani kwake, Tabata jijini Dar es Salaam, mke wa Sajuki, Wastara Juma alisema mumewe amegundulika kuwa na tatizo lingine walipokuwa nchini India kwa matibabu.
Alisema, hawakutaka kuweka hali hiyo mapema kwa Watanzania kwa kuhofia kusababisha simanzi, lakini sasa wanalazimika kufanya hivyo ili kuwafanya wajue kinachoendelea kwa staa wao.
“Kwa kweli mume wangu bado anaumwa na amegundulika kuwa na tatizo lingine ila tunamshukuru Mungu anaendelea vizuri,” alisema Wastara kwa huzuni nyingi.

NI UGONJWA GANI?
Kwa mujibu wa Wastara, walipokuwa India (katika Hospitali ya Apollo), Sajuki alifanyiwa vipimo mbalimbali ili kubaini matatizo yanayomsumbua ambapo aligundulika kuwa na tatizo kwenye uti wa mgongo na ngozi ya mwili mzima.
“Ana tatizo kwenye mfupa wa uti wa mgongo, lakini pia anasumbuliwa na tatizo jingine kwenye ngozi. Baada ya madaktari kugundua magonjwa hayo walimuanzishia dawa ya kutibu mgongo na mazoezi kwa ajili ya kumuweka sawa.
“Hizo dawa alianza kuzitumia tulipokuja huku, ambapo pia anaendelea na mazoezi. Tatizo lingine ni hilo la ngozi, ambalo pia anaendelea kutumia dawa,” alisema.

KWA NINI MGONGO?
Akifafanua kuhusu ugonjwa unaoshambulia sehemu ya mfupa wa uti wa mgongo, Wastara alisema madaktari walisema, tatizo hilo linasababishwa na kukaa kwa muda mrefu.
“Jambo hilo tulikubaliana nalo, kwa sababu ni kweli Sajuki huwa anakaa muda mrefu kwenye kompyuta kwa ajili ya kazi zake, lakini pia huwa anaendesha gari kwa muda mrefu. Tunaamini ndiyo chanzo cha ugonjwa huo kama madaktari walivyosema,” alisema na kuongeza:
“Lakini baada ya kupata dawa na ushauri  sasa anaendelea vizuri,  kwa sababu pia anafuata masharti aliyopewa vizuri. Huwa nahakikisha anapata muda mrefu wa kupumzika, hakai muda mwingi na haendeshi sana gari.
“Wamemwambia mambo mengi, hata kuinainama kila mara pia wamekataza. Kimsingi mwenzangu anahitaji uangalizi wa karibu sana. Hata hivyo anaweza kuendelea na filamu ila kwa kuzingatia na scene (onesho) yenyewe, ila kwa sasa anapumzika kwanza ili afya yake itengemae.”

KLINIKI KILA WIKI
Akiendelea kuzungumzia afya ya mumewe, Wastara alisema huwa wanalazimika kwenda Kliniki ya kila wiki katika hospitali moja jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuangaliwa maendeleo yake.
Aidha, alisema kila wiki tatu huwa wanatuma vipimo nchini India katika Hospitali ya Apollo aliyokuwa akitibiwa kwa lengo la kuchunguza maendeleo yake.

KUHUSU UGONJWA WA NGOZI
Wastara alisema, tatizo la ngozi alilonalo mumewe bado hajaanza kutumia dozi yake kwa sababu hawajapata fedha ya kutuma India ili waweze kutumiwa dawa zenyewe.
“Tupo kwenye mchakato wa kutafuta hizo fedha, lakini hali bado ni ngumu na anatakiwa kuanza dozi mapema kama madaktari walivyoshauri,” alisema na kuongeza:
“Mwezi Desemba (mwaka huu) anatakiwa kurudi tena ili aangaliwe tena maendeleo yake kwa ujumla. Yote hiyo ni gharama kubwa sana, lakini tunaamini Mungu atatusimamia.”

GHARAMA ZAMTOA CHOZI WASTARA
Alisema kwa namna mahitaji yalivyo mengi na yanayohitaji fedha, wapo kwenye wakati mgumu kuweza kuyakabili.
“Kiukweli bado tunahitaji msaada wa Watanzania wenzetu. Tunashukuru kwa wale waliojaliwa kutusaidia awali hadi kufanikisha safari yetu ya matibabu India lakini watakaoguswa wanaweza kuendelea kutusaidia.
“Mpaka sasa Sajuki hajaanza dozi ya ugonjwa wa ngozi na zipo nyingine anazotakiwa kuzitumia, lakini hazipatikani hapa...ni mpaka India.”

VIDUME VYAMTOKEA WASTARA
 Akizungumzia suala la usumbufu wa kimapenzi, Wastara alisema ni jambo la kawaida na ni kweli kuna baadhi ya wanaume wanatumia udhaifu wa ugonjwa wa mumewe kumshawishi kimapenzi.
“Kutongozwa ni jambo la kawaida kwa mwanamke, lakini mimi kama Wastara msimamo wangu ni kumheshimu mume wangu. Siwezi kushawishika kwa namna yoyote, kwanza hata hamu yenyewe sina.
“Ninachokiangalia kwa sasa ni afya ya mume wangu. Najua nina wajibu mkubwa wa kuhakikisha namhudumia mume wangu kwa mapenzi yote. Akili yangu haipo kwenye mapenzi kabisa, hali aliyonayo mume wangu inaniumiza sana.
“Kamwe sitamsaliti Sajuki wangu. Wema wake kwangu wakati nikiwa kwenye matatizo siwezi kuulipia kwa kumdhalilisha kwa kutoka na mwanaume mwingine eti kwa sababu anaumwa. Anayewaza kufanya hivyo, akajaribu kwingine, siyo kwangu.”

KALAMU YA MHARIRI
Kwa matatizo aliyonayo Sajuki ni wazi yeye na familia yake bado wanahitaji msaada wa hali na mali ili kuweza kukidhi mahitaji ya matibabu yanayomkabili kwa sasa.
Kama Mtanzania mwenzake, guswa na moyo wa utoaji na Mungu wa Mbinguni atakuongezea katika mifuko yako.
Ikiwa umeguswa, tafadhali tuma mchango wako kwenye akaunti namba 050000003047 yenye jina la Wastara Juma Issa iliyopo katika Benki ya Biashara ya Akiba (ACB) au tumia Tigopesa kwenda namba 0713 666113 yenye jina Wastara Juma.

MWIGIZAJI WA BONGO MOVIE- JACQUILINE WOLPER AWAFURAHISHA WAHEHE WA IRINGA

MWANADADA nyota katika tasnia ya filamu za Swahiliwood, Jaqueline Masawe Wolper, Jack Wolper, hivi karibuni alikuwa kivutio mjini Iringa kutokana na kuvaa gauni la heshima mithili ya mtawa

J Wolper

Watu wanaomfahamu msanii huyo, hawakuamini kuwa aliyevaa gauni hilo alikuwa Wolper ambaye mara nyingi huvaa nguo za kutatanisha na kujiachia.

Lakini siku hiyo alionekana kama mtawa au mama wa familia asiye na makuu.
Alikuwa katika Uwanja wa Samora mjini Iringa wakati wa uzinduzi wa muziki wa Injili kutoka kwa msanii Masanja Mkandamizaji.
"Ninajua kuwa mimi ni nyota kwa sasa, najaribu kwenda na matukio katika uvaaji wangu, siwezi kuvaa vazi la Disko au kuigizia katika sehemu inayohubiriwa neno la Mungu," alisema msanii huyo hukun akitabasamu.


Wolper (kulia) akiwa katika uzinduzi wa Masanja Iringa

"Ningefanya hivyo hapa, ningekuwa nashiriki kusikiliza neno la Injili au naigiza? Nipo kwenye uzinduzi wa albamu ya Masanja Mkandamizaji ambaye ni msanii mwenzetu nasi tumekuja kumsindikiza katika kazi ya kumtukuza Mungu.

"Nami namtukuza Mungu hata katika kuvaa kama unavyoniona nikiwa katika gauni safi tena la kiheshima."

Watu waliofika katika uwanja huo walishindwa kujizuia na kuanza kumsifia kwa nguo aliyovaa hata nywele zake alivyoziweka, hazikuwa za utata.

Tuesday, July 24, 2012

UNAMJUA VIZURI EDDIE MURPHY? HEBU MCHEKI



Eddie Murphy kwenye sherehe za Tribeca mnamo 2010
Amezaliwa
Edward Regan Murphy
3 Aprili 1961 (umri 51)
Brooklyn, New York, Marekani
Miaka ya kazi
1982 - hadi leo
Ndoa
Nicole Mitchell Murphy (1993-2006)
Edward "Eddie" Regan Murphy (amezaliwa tar. 3 Aprili, 1961, Brooklyn, New York City) ni mwigizaji wa filamu, mchekeshaji, na mwimbaji kutoka nchini Marekani. Eddie, pia amewahi kupata Tuzo ya Golden Globe mnamo mwaka wa 2006 na pia aliwahi kushindanishwa katika ugawaji wa Tuzo ya Academy mnamo mwaka wa 2001. Alikuwa mwanachama wa kawaidia kwenye kipindi cha TV cha Saturday Night Live kuanzia 1980 hadi 1984.
Filamu
Filamu
Mwaka
Filamu
Aliigiza kama
Maelezo
1982
48 Hrs.
Reggie Hammond

1983
Trading Places
Billy Ray Valentine

1983
Eddie Murphy Delirious
Himself

1984
Best Defense
Lieutenant T.M. Landry

Beverly Hills Cop
Det. Axel Foley

1986
The Golden Child
Chandler Jarrell

1987
Beverly Hills Cop II
Det. Axel Foley

Eddie Murphy Raw
Yeye mwenyewe

1988
Coming to America
Prince Akeem/Clarence/Randy Watson/Saul

1989
Quick (Real Name Vernest Brown)
Also Director and Writer
1990
Reggie Hammond

1992
Marcus Graham

Thomas Jefferson Johnson

1994

1995
Maximillian/Preacher Pauly/Guido
Also Producer
1996
Professor Sherman Klump/Buddy Love/
Lance Perkins/Cletus 'Papa' Klump/
Anna Pearl 'Mama' Jensen Klump/
Ida Mae 'Granny' Jensen/Ernie Klump, Sr.
Also Producer
1997
Insp. Scott Roper

1998
(voice)

G

1999
Rayford "Ray" Gibson
Also Producer
Kit Ramsey/Jeffernson 'Jiff' Ramsey

2000
Professor Sherman Klump/Buddy Love/
Lance Perkins/Cletus 'Papa' Klump/
Anna Pearl 'Mama' Jensen Klump/
Ida Mae 'Granny' Jensen/Ernie Klump
Also Producer
2001
(voice)

2002
Officer Trey Sellers

Pluto Nash

Kelly Robinson

2003
Charles "Charlie" Hinton

Jim Evers

2004
(voice)
2006

2007
Norbit Rice/Rasputia Latimore-Rice/Mr. Wong
Also Producer
(voice)
2008
Starship Dave (Spacecraft), Captain

2009
Evan Danielson

2010
(voice)
Frank Stanfred

2011
Leo "Slide" Dalphael

You might also like: