INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Friday, August 19, 2016

Zari Awapa Za Uso Wabaya Wake.

Kuna tetesi nyingi sana zimevuma kwenye mitandao ya kijamii hivi karibuni zikiwahusu Diamond na Zari.
Huku tetesi hizo zikimhusisha Diamond kusaliti mahusiano yake kwa kutoka na warembo wengine akiwemo Hamisa Mobetto na mrembo aliyetumika kwenye video ya wimbo wa ‘Kwetu’, Irene.

Wema Sepetu Na Petit Man Wapatana.

Kwa miezi kadhaa sasa Wema Sepetu na Petit Man walikuwa wakichuniana hadi kuwafanya mashabiki waanze kuuliza maswali kupitia mitandao ya kijamii kutaka kujua kunani!

Mapenzi Yamtesa Fid Q

AGOSTI 13, mwaka huu ilikuwa ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Mwanahip Hop, Fid Q na kwa furaha aliyonayo kwa kutimiza miaka kadhaa, siku hiyo aliamua kuachia ngoma mbili kama zawadi kwa mashabiki wake.
Wimbo wa kwanza unaoitwa Sumu aliutoa usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita, baadaye jioni akaachia video ya ngoma nyingine ya Roho aliyomshirikisha Christian Bella.

Masanja Awaangukia Polisi Na Kuyamaliza.

Katika harusi ya Masanja Mkandamizaji iliyofanyika Agosti 14, wachekeshaji wenzake wa kundi la Orijino Komedi, walikuja wamevalia nguo zilizofanana na sare za jeshi la Polisi hali iliyowapelekea kukamatwa. Walifikishwa kituo cha Polisi kwa mahojiano na pia wakakaguliwa sehemu wanazoishi ili kuweza kufahamika kama kuna kitu kingine wanachomiliki tofauti na sare za Polisi.

Thursday, July 28, 2016

Riyama Ally Awaumbua Waliosema Hatafika Popote Na Leo Mysterio.

STAA wa filamu za Kibongo, Riyama Ally amewafunga midomo wote waliokuwa wakibeza uhusiano wake na msanii chipukizi wa muziki wa Bongo Fleva, Haji Mwalimu Mzee ‘Leo Mysterio’, baada ya kufunga naye ndoa hivi karibuni.
Minong’ono ilikuwa mingi mitaani na kwenye mitandao ya kijamii kuwa Riyama yupo kwenye uhusiano na Serengeti Boy kwa vile kijana huyo ni mdogo wake kiumri kwa miaka saba zaidi.

Gabo Aishauri Serikali Kuhusu Sanaa Na Kilimo.

Msanii Salim Ahmed alimaarufu kama ‘Gabo Zigamba’ ameishauri serikali ya awamu ya tano kutolea macho kwenye sekta ya kilimo Tanzania pamoja na vipaji na kusema kuwa hivyo ndivyo vyanzo vizuri vya mapato.

Jay Moe Afunguka Kuhusu Shilole.

Mwanamuziki rapa nchini anayetikisa kwa ngoma ya ‘Pesa Madafu’, Jay Moe amekuwa akionekana karibu sana na rapa Bilnass ambaye anatikisa na ngoma ya ‘Chafu Pozi’ kitu ambacho ni njia pekee ya Jay Moe kumpata mrembo Shilole.
Baada ya kuwepo kwa tetesi za wawili hao kutoka kimapenzi na zaidi kuonekana picha wako pamoja kwenye moja ya eneo za kula bata wakati wa usiku, ENewz ilimtafuta rapa Jay Moe avunje mzizi huo wa fitna kama ni kweli anaanguka kwa Shilole lakini alikanusha nakusema ndio mara ya kwanza yeye kusikia habari hizo.

BASATA Wamfungia Na Kumpiga Faini Nay Wa Mitego.

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limemfungia kwa kipindi kisichojulikana msanii wa muziki wa kizazi kipya Emmanuel Elibariki maarufu kwa jina la Nay wa Mitego.
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limemfungia kwa kipindi kisichojulikana msanii wa muziki wa kizazi kipya Emmanuel Elibariki maarufu kwa jina la Nay wa Mitego hadi hapo litakapojiridhisha kwamba ametekeleza maagizo yote aliyopewa na Baraza sambamba na yeye kubadilika katika kubuni kazi zenye maadili na zisizo dhalilisha watu wa kada mbalimbali.

Thursday, July 21, 2016

Wema Sepetu Achoshwa Na Wanaomfuatilia.

"Naomba niseme kitu na nieleweke tafadhal, Sijawahi hata siku moja kwenda kwa hata mmoja wenu na kumgongea kuomba hata hela ya chumvi…. My life concerns me…. Na hata siku nikifa nakufa mwenyewe, Majibu kwa Mungu naenda kujibu alone…. Niacheni Jamani…. Nimechoka……! Jus leave me Alone…!!! Kama nakukera na maisha yangu basi usiyafatilie… Sio lazima….. Nisiheme sasa…. Naomba tafadhal kama mapungufu ni ya kwangu mimi na mimi mwenyewe sasa midomo

Wema Sepetu Bado Anataka Kuzaa Na Idris.

LICHA ya madai kuwa wapenzi wawili, Idris Sultan na Wema Sepetu wamemwagana, muigizaji huyo nyota na Miss Tanzania 2006, amesema anataka kuzaa na mshindi huyo wa Big Brother Hotshots 2014 kutokana na jinsi anavyojali na mwenye huruma nyingi.

Ali Kiba Na Baraka Dah Prince Wavamiwa Na Majambazi South Afrika.

“Wote Alikiba na Barakah the Prince walikuwa pamoja na timu kwaajili ya mkutano wa utayarishaji kwenye ofisi zilizopo maeneo ya katikati za kampuni maarufu ya Afrika Kusini wanayofanya nayo kazi,” yamesema maelezo rasmi kutoka uongozi wa Rockstar4000.
“Wakati wakiendelea na mkutano, watu sita waliokuwa na bunduki walivunja kuta za jengo la ofisi hiyo na kuingia walipokuwa Alikiba, Barakah The Prince na wengine,” yamesema.

Thursday, July 14, 2016

Filamu 25 Za ZIFF Kutumika Kufundishia Mashule.

MKURUGENZI wa Tamasha la Ziff, Profesa Martin Mhando, amesema kwamba baadhi ya filamu katika tamasha la mwaka huu zitatumika kwa ajili ya kufundishia.

Shilole Ampata Mrithi Wa Nuh Mziwanda.

STAA anayebeba fani mbili kwa mpigo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, juzikati alimwanika bwana’ake mpya huku akijinadi kuwa ndiye mrithi halali wa aliyekuwa mpenzi wake wa kitambo, Naftari Mlawa ‘Nuh Mziwanda’

Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni baada ya kubambwa kwenye Ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga jijini Dar es Salaam ilipokuwa ikifanyika Shoo ya Black Tie, Shilole alisema ameamua kubadili upepo na kuachana na mapenzi ya vijanahivyo ameangukia kwa mwanaume huyo ambaye ni mtu wa rika lake.
“Kusema kweli leo sitaki hata kupaparika maana nimekuja na mheshimiwa hivyo sitaki tena kuonekana kama mtoto mdogo humu ukumbini, angalia hata meza niliyokaa utagundua kuwa hapa ishu zote ni za kiutu uzima, siwezi tena kupaparika, ifikie muda tuheshimiane kwani njia pekee ya kujiheshimu ni kutoka na watu wenye msimamo wao nawatu wazima kama huyu.

Roma Mkatoliki Asema Babu Tale Alimchimba Mkwara.

Msanii Roma Mkatoliki ambaye leo ameachia ngoma yake mpya ‘Kaa tayari’ amefunguka na kusema moja ya mstari uliopo kwenye wimbo wake huo unamuhusu meneja wa Diamond Platnumz ambapo unamchana kuwa saizi anamganda sana Diamond Platnumz mpka amelisahau kundi lake na Tip Top Connection.

Siasa Ipo Kwenye Damu Yangu: Irene Uwoya

STAA mkali Bongo Muvi, Irene Uwoya amefunguka kuwa bado hajakata tamaa ya kuwa mwanasiasa japokuwa mwaka jana alishindwa lakini hiyo imempa nguvu ya kujipanga zaidi na kwamba kwa sasa akili yake yote akilala, akiamka ni kuwaza siasa tu.

Saturday, July 9, 2016

Mose Iyobo Ataka Aunty Ezekiel Achore Tattoo Ya Jina Lake.

Moses Iyobo ‘Moze’ ambaye ni mzazi mwenza wa staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson, amemwambia mpenzi wake huyo kuwa na yeye ajichore ‘tatuu’ ya jina lake kama ilivyokuwa kwa msanii Zuwena Mohammed ‘Shilole’ kwa Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ kabla ya kumwagana.

Mr.Blue Aikubali Couple Ya Diamond Na Zari.

Mr Blue amesema Diamond na Zari ndiyo couple anayoikubali zaidi.
“Ukinitoa mimi na Wahyda couple ambayo naipenda, naielewa ni Zari na Diamond,” Blue alikiambia kipindi cha The Playlist cha Times FM.
“Yaani wanapendeza unajua eeh, na Mungu amewajaalia wamepata mtoto, wanashirikiana kama marafiki kwenye biashara, wanajua kucheza na akili za raia, wanaitengeneza couple yao ya kimapenzi, wanaifanya pia inakuwa kibiashara, yaani very nice,” aliongeza.

Mtitu Awachana Viongozi Wa Shirikisho La Filamu Tanzania.

DAIREKTA mwenye jina kubwa nchini, William Mtitu amefunguka kuwa kitu kinachoiangusha tasnia ya filamu Bongo ni uongozi wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), ambao umeshindwa kuwasimamia wasanii wake vizuri pamoja na kutengeneza mazingira mazuri ya kuwafanya wadau mbalimbali kuvutiwa na tasnia hiyo hata kuwekeza.

Bodi Ya Filamu Yahimiza Wasanii Wachanga Wasaidiwe.

Wito huo umetolewa na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Bi.Joyce Fissoo jijini Dar es Salaam wakati akimkabidhi Bi Wakonta Kapunda Shilingi laki tano kwa ajili ya Safari ya kwenda Zanzibar kushiriki mashindano ya uandishi wa Muswada (Script).
“ Napenda kutoa wito kwa wadau wa sanaa kusaidia wasanii wanaochipukia kwani ni nguzo muhimu kwa maendeleo ya sanaa nchini” Alisema Bi Joyce.

Sunday, July 3, 2016

Mimi Ni Dhahabu Kila Mtu Anataka Kuishika: Wema Sepetu

Wema  Sepetu, amesema yeye ni dhahabu inayogombewa na watu hivyo hajali hata kama atachafuliwa namna gani katika mitandao ya kijamii.

Wema aliliambia MTANZANIA kwamba, hana mpango wa kujibu vibaya vinavyoongelewa kuhusu yeye kwa kuwa yeye bado ni dhahabu inayotamaniwa kushikwa na kila mtu.

Jokate Na Ali Kiba Wadaiwa Kurudiana.

Wapenzi mastaa Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na Alikiba Saleh ‘King Kiba’ wameombwa chondechonde na baadhi ya mashabiki wao kuwa sasa wafunge ndoa kwani penzi lao lina baraka ya Mungu kutokana na kukumbwa na migogoro lakini bado likaibuka kwa staili nyingine.

Jini Kabula Asweka Lupango.

Kibano! Staa wa sinema za Kibongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ amejikuta kwenye mikono ya sheria na kuswekwa lupango baada ya  kumtukana shosti yake, Miss Kinondoni 2009, Stella Mbuge.
Kwa mujibu wa mtoa ubuyu wetu makini, Kabula alitaitiwa na polisi usiku wa Jumatano iliyopita mara baada ya kutendo kosa hilo walipokuwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar wakitazama mechi kati ya Yanga na TP Mazembe ya DR Congo.

Abdu Kiba Asema Wasanii Wa Label Ya WCB Wanabebwa Na Promo.

Abdu Kiba amesema kuwa promotion ndiyo inawabeba wasanii wa lebo ya WCB.
Muimbaji huyo amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM, “Sijafikiria kuimba na msanii kutoka WCB,
kwa sababu sijaona anayeimba type ya muziki wangu.”
“Hata kama wana promote kwa sababu ndiyo walipoona wao ndiyo wanaweza wakafanya na watu wakaweza kuelewa lakini siku zote ajuae hazami,” alisema Abdu Kiba.
Aidha aliongeza kuwa bado hajaona msanii anayeimba type ya muziki wake ndani ya lebo hiyo [WCB].
Hata hivyo mapema mwezi huu msanii huyo alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio kuwa yupo tayari kujiunga na lebo wa WCB kama watakubaliana na kuweka hela mezani kauli ambayo baadaye yeye mwenyewe aliipinga kuwa watu hawakumuelewa vizuri alichomaanisha.

Amanda Poshy Awachana Mastaa Wambwia Unga.

AMANDA Poshi, staa wa sinema za Kibongo, amewabwatukia baadhi ya mastaa wanaojitangaza kuwa wanatumia madawa ya kulevya baada ya kuathirika kuwa ni wanafiki.

Alisema angewaona wana hoja kama wangejitangaza kipindi walipoanza kuyatumia kuliko wakiona yanawashinda ndiyo wanakimbilia kwenye vyombo vya habari kuomba msaada.

Friday, June 3, 2016

Wema Alalama Kukosa Amani Sababu Ya Kuandamwa.

Msanii wa filamu na mjasiriamali Wema Sepetu amefunguka ya moyoni kutokana na namna mashabiki wake wa Instgram wanavyomchukulia na kumpa maneno ambayo muda mwingine yanamuumiza na kumkosesha amani na kumfanya ajione ni kama mkosaji mkubwa.

Rich Mavoko Asainishwa Rasmi Label Ya WCB

Msanii Diamond Platnumz, ameitambulisha rasmi label yake ya ‘WCB’ pamoja na kumsaini Rich Mavoko mbele ya waandishi wa habari.
Aidha, Diamond alimtambulisha dada yake, Queen Darleen kuwa mmoja kati ya wasanii wapya wa label hiyo.
Shughuli hiyo ilihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa Taifa, Godfrey Mngereza ambaye alizungumza na kumpongeza Diamond huku akiwataka wasanii wengine kushirikiana kwa namna hiyo.

Tuesday, May 31, 2016

Lazima Nimzalie Harmonize: Wolper

Jacqueline Wolper amenyanyua kinywa chake na kusema; “lazima nimzalie Harmonize (Rajabu Abdulhan, staa wa Bongo Fleva), kwa kuwa nimeridhika naye.”

Sijutii Kutembelea Bajaji: Wema Sepetu

STAA mwenye nyota ya kipekee Bongo, Wema Sepetu amewafungukia wanaomsema vibaya kuwa siku hizi kafulia mpaka anatembelea usafiri aina ya Bajaj na kudai kuwa hayo ni maisha yake binafsi ambayo hayamhusu mtu yeyote.
Akizungumza na gazeti hili juzikati, Wema alisema kuwa anashangazwa sana na watu ambao wanafuatilia maisha yake kila kona kwa kuwa yeye ni binadamu kama walivyo wengine na maisha yote anastahili kuishi.

Sikumuimbia Jokate Wimbo Wa Aje: Ali Kiba

Alikiba amesema Aje si wimbo aliomuimbia Jokate wala msichana yeyote bali aliimba kwaajili ya mashabiki wake.
“Sijamuimbia mtu yeyote kwa kweli, mi nimeimba kwa ajili ya mashabiki wangu, kwanza sijawahi kumuimbia mtu kabisa, sijawahi, so ni kwa ajili ya mashabiki wangu,” Kiba alikiambia kipindi cha Friday Night Live cha EATV.

Picha: Harmonize Amtambulisha Wolper Kwa Wazazi Wake Huko Mtwara.

Ijumaa iliyopita Harmonize alikuwa Mtwara kwenye show, hata hivyo alitumia nafasi hiyo kwenda kumtambulisha mpenzi wake mpya Jacqueleine Wolper kwa wazazi wake. Angalia picha...

Wednesday, May 25, 2016

Aunty Ezekiel Aelezea Maumivu Aliyopata Wakati Wa Kujifungua Mtoto Wake Wa Kwanza.

Msanii wa filamu Aunt Ezekiel amefunguka na kueleza jinsi alivyopitia maumivu makali wakati wa kujifungua mtoto wake wa pekee ‘Cookie’ ambaye ametimiza moja mmoja hivi karibuni.
Kupitia ukurasa wake wa instagram, Aunt Ezekiel aliandika:

JB Azitolea Nje Ofa Za Filamu Za Kinageria, Ijue Sababu.

JB si msanii anayezuzuka na filamu za Kinaijeria ndio maana amesema ameshazitolea nje ofa tatu za kuigiza filamu za Kinaijeria.
“Natoboa siri ambayo watu hawaijui, nimekataa script zaidi ya tatu Nigeria kwenda kuact kwasababu hazinilipi,” muigizaji huyo aliiambia 255 kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

Martin Kadinda Azungumzia Ugomvi Wa Mirror Na Petit Man.

Martin Kadinda amefunguka juu ya ugomvi wa Mirror na Petiti Man. Akizungumza na Enewz Kadinda alisema kuwa ugomvi wa Mirror na Meneja wake anayesimamia kazi zake za muziki yaani Petit man ni utoto tu unawasumbua.

Sababu Ya Wolper Kumbwaga Mkongo Na Kuwa Na Harmonize Ni Hii Hapa.

Mwigizaji Jackline Wolper jana amefanya mahojiano na Zamaradi Mketema kwenye kipindi cha TakeOne na kuzungumzia mambo mengi kuhusu yeye na aliyekuwa mpenzi wake Putin ‘Mkongo’ aliyemvisha pete, na uhusiano wake na msanii Harmonize.
‘Ni kweli Raj (Harmonize) ni mpenzi wangu,ukweli nilimjua siku nyingi nilikuwa nikimchukulia kama mwanamuziki tu, tuna mwezi mmoja na wiki mbili sasa’’ alisema Jack.

Mimi Ni Zaidi Ya Ray: Gabo Zigamba

Msanii wa filamu nchini ambaye anafahamika kwa kuigiza kwa lafudhi ya Kimakonde Gambo Zigamba amefunguka na kusema kuwa yeye ni zaidi ya msanii Ray Kigosi kwenye kazi kwani yeye anafanya zaidi ya Ray.
Akizungumza kwenye kipindi cha eNewz Gambo Zigamba aliweka wazi kuwa kipindi ambacho wakina Ray na wasanii wengine wakongwe wanafanya kazi zao hizo kulikuwa hakuna wasanii wengine wachanga ndiyo maana walikuwa wanaonekani ni wazuri sana lakini hivi sasa tasnia imekuwa na vipaji vipya ambavyo vinafanya vizuri zaidi yao hao wakongwe.

Ali Kiba Amuombea Kura Diamond BET Awards.

Msanii Alikiba amefunguka na kusema kwa mafanikio aliyopata toka amerudi kwenye muziki tena ndani ya muda ni mfupi ni sawa na kuchana msamba kwake maana siyo hatua za kawaida.
Alikiba alisema haya kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio na kusisitiza kuwa yeye kusaini mkataba na kampuni ya ‘Sony Music’ jambo kubwa sana katika maisha yake ya muziki.
“Kiukweli toka nimerudi rasmi kwenye game na kutoa wimbo wa Mwana mashabiki walipokea vizuri sana Africa Mashariki, na kadili nilivyokuja kutoa wimbo mwingine wa Chekecha walizidi kuongezeka mashabiki na kujiona nina mashabiki wengi, hivyo kuja kusaini mkataba na ‘Sony Music’ ndani ya muda mfupi hivi kwangu mimi najiona ni kama nimepiga msamba maana siyo hatua za kawaida” alisema Alikiba.

Tuesday, May 24, 2016

Picha: Wema Sepetu Azindua Application Yake Ya Simu.

Jana Wema Sepetu Alizindua application yake ya simu kwa ajili ya kuwa karibu na amshabiki wake. uzinduzi huo ulihudhuriwa pia na waziri wa sanaaa, utamaduni na michezo Nape Nnauye. Hizi ni picha toka kwenye event hiyo...

Friday, May 20, 2016

Zari Na Mama Diamond Watifuana ?

Inadaiwa ilitokea lakini haikuandikwa! Kuna habari kuwa, ile safari ya familia ya nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kula bata kwenye nchi za Ulaya, ilikuwa na mambo mengi lakini kubwa ni madai ya kuwepo kwa mtifuano kati ya mama Diamond, Sanura Kasim na Zarinah Hassan ‘Zari’ ambaye ni mzazi mwenzake, Diamond.
Kwa mujibu wa chanzo, mtifuano kati ya Zari na mkwewe huyo ulitokea baada ya siku moja mkwe huyo kuteleza kwenye ngazi za umeme wakiwa wanapanda, Zari akamuwahi kwa kumshika mkono hali iliyomtibua mama huyo.

Rose Ndauka Aelezea Siri Ya Mafanikio Yake.

MKALI wa filamu Bongo, Rose Ndauka ametoa siri ya mambo yake kumnyookea kuwa imetokana na kumuhusisha Mungu kwa kila anachokifanya na wala si vinginevyo kama watu wanavyodhania.
Akizungumza na Amani, Rose ambaye kwa sasa anamiliki kampuni inayojishughulisha na kutengeneza Jarida la Rozzie, alisema kuwa Mungu ndiye aliyemtendea miujiza hiyo kwani asingemshirikisha asingekuwa hapo alipo.

Wema Sepetu Amfungukia Ali Kiba.

Msanii wa filamu nchini Wema Sepetu amefunguka na kusema kuwa msanii Alikiba ni mtu wa kumuacha kutokana na uwezo wake wa kuimba na namna ambavyo anaweza kuipangilia sauti yake kwenye muziki.
Wema Sepetu amezidi kuonyesha mapenzi aliyonayo kwenye kazi za msanii Alikiba na kusema huwa zinamkosha sana na kudai hajawahi kumuangusha siku zote

Monday, May 9, 2016

Harmonize Afunguka Baada Ya Kuzawadiwa Gari.

Msanii ambaye yupo chini ya Label ya WCB, Harmonize jana amezawadia gari aina ya Mark X na uongozi wake wa WCB kama motisha kwa kazi zake lakini pia kama njia ya kumrahisishia usafiri na kulinda jina lake na hadhi yake.
Baada ya kupewa zawadi hiyo ya gari msanii huyo alikuwa na maneno ya shukrani kwa uongozi wake huo na kusema kuwa kitendo hicho kimemfanya awe na furaha ambayo hajawahi kuwa nayo.

Diamond Ni Mshikaji Wangu Ila Simtegemei: Shetta

Msanii Shettah ambaye kwa sasa ameachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Namjua’ amefunguka na kusema kuwa yeye na msanii Diamond Platnumz ni washikaji sana na marafiki wa karibu sana ila inapokuja suala la kazi Shettah anasimama kama Shettah.
Shettah alifunguka hayo kupitia show ya Friday Night Live inayorushwa na EATV kila siku ya Ijumaa na kudai kuwa kwenye masuala ya muziki yeye anasimama kama yeye japo muda mwingine watu hao wamekuwa mchango katika kumbadilisha kutoka kwenye kuchana mpaka sasa anaimba ngoma kama hizo.
“Unajua Diamond Platnumz ni mshikaji sana na mtu wangu wa karibu sana ila inapokuja kwenye masuala ya kazi mimi kama Shettah nasimama mimi kama mimi na ndiyo maana unaona nina Management yangu tofauti na muda si mrefu huenda na mimi nikawa na wasanii nawasimamia kwani kwa sasa siwezi kushindwa kumfanyia msanii kazi na kumtolea pesa ya video lakini nataka nijipange zaidi na team yangu” alisema Shettah
Mbali na hilo Shettah amekiri wazi kuwa katika wimbo wake wa sasa ‘Namjua’ kuna michango ya watu mbalimbali katika kuifanya kazi hiyo isimame na kusema zipo hata melody za Diamond Platnumz ndani ya wimbo huo yaani alimuelekeza labda sehemu hii Shettah pita hivi hapa fanya hivi.
eatv.tv

Siwezi Kumhukumu Nay Wa Mitego: Shamsa Ford

STAA wa Bongo Muvi, Shamsa Ford kwa mara ya kwanza ameibuka na kuiongelea Ngoma ya Shika Adabu Yako iliyoimbwa na Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ kuwa kamwe hawezi kumhukumu Nay kwa maneno aliyoimba.

Ray Kucheza Filamu Nchini Rwanda.

Msanii wa filamu nchini Vicent Kigosi amefunguka na kusema kuwa yeye ni msanii pekee kutoka Tanzania ambaye amechaguliwa kushiriki katika filamu inayounganisha nchi mbili ya Rwanda na Tanzania.
Ray Kigosi kupitia mtandao wake wa kijamii aliandika kuwa kwa nafasi aliyopata hawezi kuwaangusha watanzania kwani yeye amekwenda kuwaonyesha kazi.

Tuesday, May 3, 2016

TID Afungukia Penzi Lake Na Wema Sepetu.

Msanii mkongwe wa muziki, TID amesema kipindi cha nyuma alikuwa anatoka kimapenzi na malkia wa filamu Wema Sepetu lakini baadae alitemwa hali ambayo ilimuumiza sana.
Akizungumza katika kipindi cha Clouds TV Ijumaa hii, TID amesema hali hiyo ilimfanya atoke na wasichana wengi.
“Nilikuwa ‘namdate’ Wema Sepetu akaniambia sikutaaki, tangu kipindi hicho nimekuwa na wasichana wengi. Ikitokea Wema anataka kurudi hakuna nafasi, I’m occupied,” alisema TID.

Sipendi Kuanika Mali Zangu Mitandaoni: Irene Uwoya

MSANII wa filamu za nchini, Irene Uwoya, amefunguka na kusema hapendi kuweka wazi mambo yake binafsi kama ilivyo wasanii wengine.
Msanii huyo alisema kuwa kuna baadhi ya wasanii ambao wanapenda kuweka kila kitu chake ambapo haina maana yoyote kwa jamii.

Mzee Majuto Atangaza Kuacha Kuigiza.

Mzee Majuto amesema kuwa kwa sasa anaamini anaweza kuishi bila kutumia kipaji chake hicho cha ugizaji na muda huu atatumia kumuomba Mungu amasamehe makosa aliyotenda na kudai kuwa anaamini itawezekana kwani Mungu ndiye anayetoa ridhiki kwa kila mtu.

Saturday, April 23, 2016

Filamu Ya MKWE Yapokelewa Vizuri Sokoni.

Filamu ya MKWE toka kampuni ya J-Film 4 Life imeingia sokoni tayari humo ndani ikiwa na wasanii kama Odama na Hemedy. Nunua nakala yako halisi sasa.

Wezi Wa Kazii Za Wasanii Kufungwa jela Miaka 5

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) itaendelea na msako mkali kwa wafanyabiashara wote wanauza kazi za filamu na muziki bila kubandika stempu halali za kodi, ili kulinda kazi hizo kwa ajili ya kuwanufaisha wasanii pia kuhakikisha serikali inapata kodi kutoka na kazi za wasanii.

Rammy Galis Apata Shavu La Kuigiza Nigeria.

Muigizaji wa filamu nchini, Rammy Galis amepata shavu la kuigiza filamu mpya Nigeria iitwayo Her Shoes.
Rammy alienda Lagos kumalizia kurekodi video yake iitwayo Red Flag lakini imebidi aendelee kuwepo huko baada ya kupata shavu la Nollywood.