INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Thursday, July 28, 2016

Jay Moe Afunguka Kuhusu Shilole.

Mwanamuziki rapa nchini anayetikisa kwa ngoma ya ‘Pesa Madafu’, Jay Moe amekuwa akionekana karibu sana na rapa Bilnass ambaye anatikisa na ngoma ya ‘Chafu Pozi’ kitu ambacho ni njia pekee ya Jay Moe kumpata mrembo Shilole.
Baada ya kuwepo kwa tetesi za wawili hao kutoka kimapenzi na zaidi kuonekana picha wako pamoja kwenye moja ya eneo za kula bata wakati wa usiku, ENewz ilimtafuta rapa Jay Moe avunje mzizi huo wa fitna kama ni kweli anaanguka kwa Shilole lakini alikanusha nakusema ndio mara ya kwanza yeye kusikia habari hizo.

“Ndio kwanza nasikia mambo hayo, sijui mamneno hayo yametoka wapi, ni mambo ya muziki tu na uvumi wa stori tofauti, kama picha mimi ni msanii na kama wasanii picha ni kawaida tu ila hakuna kinachoendelea kati yangu na Shilole”
Jay Moe anatajwa kuwa karibu na Shilole kutokana na urafiki wake na Billnas.
eatv.tv

No comments:

Post a Comment