INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Thursday, July 28, 2016

Riyama Ally Awaumbua Waliosema Hatafika Popote Na Leo Mysterio.

STAA wa filamu za Kibongo, Riyama Ally amewafunga midomo wote waliokuwa wakibeza uhusiano wake na msanii chipukizi wa muziki wa Bongo Fleva, Haji Mwalimu Mzee ‘Leo Mysterio’, baada ya kufunga naye ndoa hivi karibuni.
Minong’ono ilikuwa mingi mitaani na kwenye mitandao ya kijamii kuwa Riyama yupo kwenye uhusiano na Serengeti Boy kwa vile kijana huyo ni mdogo wake kiumri kwa miaka saba zaidi.

Akiondoa utata, Riyama alisema wanaojua kusugua midomo waendelee lakini wao tayari wameshakuwa mwili mmoja, yeye akiwa mali halali ya Leo Mysterio.
“Wamesema sana, lakini sasa limewashuka shuuu! Wengine walisema sijui tunatafuta kiki, mara ooh! Sijui nimemzidi umri… inawahusu nini? Tayari tumeshafunga ndoa, sasa watuache tulale. Kama vilimilimi tushawakata,” anasema Riyama.
Mysterio ana umri wa miaka 26 huku Riyama akiwa na miaka 33, miaka saba zaidi ya mume wake huyo anayetamba kupendana mpaka kifo kitakapowatenganisha.
Riyama anasema: “Mimi najiheshimu sana, ndiyo maana huwezi kunikuta kwenye skendo yoyote. Hata mavazi yangu siku zote huwa ya heshima. Najitambua sana.
“Sasa kama kupenda au kupendwa na mtu mliyezidiana umri ni skendo, nipo tayari kwa hiyo. Mimi nilichoangalia ni mapenzi ya kweli, siyo umri. Mume wangu tumeelewana na naona kila mmoja anakidhi haja za mwenzake, sasa tatizo nini?
“Nampenda na nitamheshimu mume wangu hadi kifo kitakapotutenganisha, wanaosema na waseme, sisi tumeziba masikio yetu. Wala hatufikirii kuachana. Sisi ni wa maisha.
Mtanzania

No comments:

Post a Comment