INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Sunday, December 28, 2014

Photos: Odama Ndani Ya S.Akifanya Yake.

Hizi ni picha zaidi zikimuonyesha star wa filamu Odama akiwa S.Afrika kwa mishe mishe zake mbali mbali zikiwemo za kikazi

Saturday, December 20, 2014

Picha: Odama Akiwa Ndani Ya S.Africa Kwa Ajili Ya Kikazi.

Odama yupo nchini S.Africa kwa mapumziko na shughuli nyingine za kibiashara. Angalia baadhi ya picha .............

Tuesday, December 16, 2014

Odama Aenda S.Africa Kisha Brazil Kwa Ajili Ya Holiday Na Masuala Ya Kikazi.

Odama Jennifer Kyaka mmoja wa waigizaji maarufu wa filamu nchini juzi alisafiri kwenda nchini S.Africa na baadaye ataekea nchini Brazil kwa ajili ya mapumziko na bia mambo mengine ya kibiashara. Angalia wakati akiwa Julius Nyerere international Aiport.......

Thursday, December 11, 2014

Nimeumizwa Sana Katika Mapenzi: Happy Nyatawe

Star wa filamu Tanzania Happy Nyatawe amesema kuwa Zamani mapenzi yalimtesa sana ila kwasasa amepata kujifunza hapendi kuweka focus kwa mtu asiyempenda kwa dhati na wala halazimishi mapenzi ila anakomaa na kazi zake kama kawaida.

Idris Kuwekeza Katika Tasnia Ya Filamu Nchini Sehemu Ya Pesa Alizoshinda Big Brother Africa.

Mshindi wa Big Brother Africa HotShot 2014 toka Tanzania Idris Sultan amesema kuwa sehemu ya pesa zake alizoshinda atawekeza katika tasnia ya filamu nchini Tanzania kwa kuwa anapenda kuwekeza katika sanaa hiyo inayokuwa nchini.

Monday, November 24, 2014

Uzinduzi Wa Tanzania Film Awards New Africa Hotel Wafana.

Uzinduzi wa tuzo za Tanzania film awards uliofanyika jana New Africa Hotel ulifana huku wasanii mbalimbali wa filamu wakijitokeza kwa wingi. Angali picha

Saturday, November 22, 2014

Batuli Kuolewa Siku Si Nyingi.

Batuli
Star wa filamu Tanzania Batuli Yobnesh Yusuph anatarajia kufunga ndoa siku si nyingi baada ya kupata mwandani wa maisha yake.

Huu Ndio Muonekano Mpya Wa Odama.

Huu ni muonekano mpya wa star wa filamu Odama jennifer Kyaka,

je umeuonaje?

Tuesday, September 30, 2014

MAZISHI YA KAKA YAKE NA CAMERAMAN WA KAPUNI YA J-FILM 4 LIFE BWANA MALICK SIKU YA JUMATATU 28.09.2014 MKOANI PWANI

Siku ya jana Cameraman wa J-Film 4 Life chini ya Mkurugenzi Jennifer Kyaka (Odama) Bwana Malick kwa masikitiko makubwa aliweza kushirikiana na ndugu na jamaa kumzika kaka yake aliyepata ajali kwa pikipiki na kupoteza uhai. Crew ya J-Film 4 Life iliweza kufika katika msiba huu mkubwa na kuungana na ndugu na marafiki kupumuzisha mwili wa marehemu mkoani Pwani.

Rumafrica iliungana na crew ya J-Film 4 Life katika safari ya mwisho ya kuaga mwili wa marehemu. Hakika tulisikitishwa sana na kifo cha kaka wa rafiki yaetu Malick na ndio maana hatukujizuia kuungana na wenzetu kwenda katika msiba huo mkubwa sana kwa Taifa la Tanzania.

Tukumbuke sote ndiko tunakuelekea, hakuna mwenye makazi ya kudumu hapa duniani
Kulia ni Bwana Malick akiwa na msanii wa Bongo Movie, mchekeshaji Kingwendu


Msanii wa Bongo Movi Kingwendu (kushoto) akiongea na mfiwa Malick mawili matatu..
 Mfiwa Malick
 Crew ya J-Film 4 Life- Kutoka kushoto ni Director Lamata, mzee wa boom Issa, msanii wa Bongo movie, Kupa, Make up Ashura, Light Abdul, cameraman Malick (mfiwa), mkurugenzi wa J-Film 4 Life Odama
 Crew ya J-Film 4 Life- Kutoka kushoto ni Director Lamata, still picture Rulea Sanga, msanii wa Bongo movie, Kupa, Make up Ashura, Light Abdul, cameraman Malick (mfiwa), mkurugenzi wa J-Film 4 Life Odama
 Wananchi wakielekea makaburini
 Mazishi yakiendelea. Msanii wa Bongo Movie Kupa (mwenye nyekundu) alikuwepo





 Issa (mbele) na Malick (nyuma)


Rulea Sanga wa pili kutoka kulia akitupia mchanga kaburini
 Kutoka kushoto ni Abdul, Malick na Rulea Sanga (waliovalia tshirts nyeusi)
 Rulea Sanga wa pili kutoka kushoto
 Rulea Sanga mwenye tshirts nyeusi akishirikiana na wakazi wa pwani wakati wa kuzika


 Odama
  Mkuugenzi Odama
 J-Film 4 Life Make Up, Ashura
  J-Film 4 Life Director Lamata
  J-Film 4 LifeCrew
  J-Film 4 Life
  J-Film 4 Life Crew
  J-Film 4 Life boss Odama


Odama and Malick

Monday, September 22, 2014

TAZAMA MASTAA WA BONGO WAKIOSHA MAGARI KUSAIDIA WAATHIRIKA WA AJALI!


Monalisa, Odama pamoja na Johari wakisubiria wateja.

Wasanii wa filamu wakiwemo Johari, Monalisa, Irene Uwoya, Odama, Richie pamoja na Jacob Stephan aka JB jana katika viwanja vya Biafra Kinondani jijini Dar es Salaam, wameendesha kampeni ya kuosha magari ili kuchangisha fedha itakayowasaidia waathirika wa ajali za barabarari waliolazwa kwenye wodi ya hospitali ya taifa yaMuhimbili.Akizungumza na Bongo5 kwenye banda la Jaffary Carwash ambapo shughuli hiyo ilipokuwa ikifanyika, JB alisema kama wasanii wana wajibu wa kufanya shughuli za kijamii ili kuisaidia.

Kajala Masanja akiosha gari

“Sisi kama wasanii tunaonyesha tunaweza kutumia nguvu zetu kuosha magari ili kupata pesa za kuwasaidia watu ambao wameathirika kwa ajali za gari. Kwahiyo hii ni sehemu ya wajibu wetu, tunawakaribisha watu waje waoshe magari yao,” alisema JB
JB akiwa na Irene Uwoya

Richie na Kajala wakiwa na mteja wao baada ya kuosha gari lake

Johari na Monalisa wakiosha gari

Richie akiosha gari

Saturday, September 20, 2014

ODAMA KUOSHA MAGARI BIAFRA LEO MCHANA


Jeniffer Kyaka (Odama)

Msanii wa Bongo Muvi anayeheshimika sana na jamii kwa kazi zake nzuri zinazofanywa na kampuni yake ya J-Film 4 Life dada Jennifer Kyaka (Odama) siku ya leo atakuwa akiosha magari yeye mwenyewe katika viwanja vya Biafra mchana wa leo. Ukitaka kumuona yeye na wasanii maarufu sana wa Bongo Muvi basi jisogeze pale Biafra uone mastaa hawa wakipiga kazi. Soma hilo tangazo


Friday, September 19, 2014

PICHA: ODAMA NDANI YA KITCHEN PARTY YA NDUGU YAKE NA DIRECTOR WA FILAMU TANZANIA LAMATA


Tunamshukuru Mungu siku hii ilikuwa ya kipekee sana kwa rafiki yangu Lamata katika Kitchen party ya ndugu yake. Tukiwa na baadhi ya wasanii wa Bongo Movie, tuliselebuka mpaka bhasiiii... tulimaza shughuli hii kwa amani na upendo...

Kutoka kulia ni Lamata, Kajala na Odama
 Jennifer Kyaka (Odama)
  Jennifer Kyaka (Odama)
  Jennifer Kyaka (Odama)
  Jennifer Kyaka (Odama)
  Jennifer Kyaka (Odama)
  Jennifer Kyaka (Odama)
  Jennifer Kyaka (Odama) na Kajala
 Jennifer Kyaka (Odama)