INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Friday, August 19, 2016

Wema Sepetu Na Petit Man Wapatana.

Kwa miezi kadhaa sasa Wema Sepetu na Petit Man walikuwa wakichuniana hadi kuwafanya mashabiki waanze kuuliza maswali kupitia mitandao ya kijamii kutaka kujua kunani!

Lakini usiku wa August 16, wawili hao walionekana wakijirekodi video fupi na Wema akaiweka katika account yake ya SnapChat. Baadaye kulivyokucha Wema alionekana kupost video clip ile ile ya SnapChat kwenye Instagram kuandika hivi: Yes…! He has a piece of me… @officialpetitman_wakuachetz”
Kwa miaka mingi Petit alikuwa akifanya kazi na Wema kama msaidizi wake. Hivi karibuni aliongea na Bongo5 kuelezea tetesi hizo za kukosana na Wema.
“Mimi sidhani kama nina tatizo na Wema. Ndiye aliyenifanya mimi nijulikane na Wema ndiye mtu ambaye mimi nimetoka naye mbali sana miaka tisa. Kwahiyo hata kama nikiwa nimegombana naye siwezi nikasema siongei naye, kwahiyo mimi nahesabia sina tatizo naye kama watu wanavyodhani,” alisema.
Bongo5

No comments:

Post a Comment