INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, July 16, 2012

TAMASHA LA UZINDUZI WA ALBAM YA HAKUNA JIPYA YA MCHUNGAJI MTARAJIWA MASANJA MKANDAMIZAJI (EMMANUEL MGAYA) LAFANA IRINGA MJINI

Mungu alimtumia Emmanuel Mgaya (Masanja Mkandamizaji au Mchungaji Mtarajiwa) kuwakusanya watu katika Uwanja wa Samora mjini Iringa kushuhudia matendo makuu ya Mungu, ambapo msanii huyu alikuwa akizindua albamu yake ya "Hakuna Jipya" Masanja Mkandamizaji ni mkazi wa jijini Dar es Salaam ni mzawaliwa wa mkoa wa Iringa. Aliamua kufanya tamasha lake katika mkoa aliozaliwa.

Msanja Mkandamizaji aliwakusanya watu kutoka mikoa mbalimbali waliofika  kushuhudia uzinduzi huo. Wasanii wa filamu za kibongo kutoka Dar es Salaam walifika mahali pale kama. Odama, Ray, steve Nyerere, Davina, Chopa Mchopanga, Jacquline Wolper na wengine wengi walifika mahali pale.

Mbali na uimbaji masanja Mkandamizaji ni mchekeshaji katika kituo cha televisheni cha TBC1 "Orijino ze Commedy", kutokana na karama hiyo ya uchekeshaji amepata kibali cha kukubalika katika jamii.

Masanja kwa sasa anajiita "Mchungaji Mtarajiwa" anategemea kuwa mchungaji lakini anasema hajui itakuwa saa ngapi, siku gani na wapi ataanza huduma hiyo, ila anakuomba uzidi kumuombea.

Masanja akisindikizwa na waimbaji mbalimbali kutoka Iringa na mikoa mingine katika uwanja wa samora mjini Iringa

Masanja Makadamizaji akikagua gwaride lake





Masanja Mkandamizaji na gwaride lake wakiingia jukwaani

Waimbaji wakiwa pamoja na Masanja Mkandamizaji aliyeshika ubao kama alama ya bunduki
Diwani wa kata ya kitanzini Manispaa ya Iringa Jesca hakuwa nyuma kutoa support kwa kununua DVD ya album ya HAKUNA JIPYA


JB toka bongo movie akitoa support kwa kununua DVD na Audio Cd

Hapa Mgeni Rasmi akiongea baada ya kuzindua waliokaa ni baadhi ya wabunge wa viti maalum na mkuu wa mkoa wa Iringa.


Tayari hapa Mgeni rasmi Mulugo amsehazindua


Naibu Waziri wa Elimu Milubo akizindua DVD na VCD


Baadhi ya viongozi wa Elimu wakiwa na mgeni Rasmi

Kundi la Bongo Movie kutoka Dar es Salaam waliofika ku-support kazi ya Emmanuel Mgaya

JB wa Bongo Movie akiwa ameshika kibaza sauti pamoja na waigizaji wenzake

Jacquline Waolper akiwa na furaha kuona tamasha linaenda vizuri


Vicent Kigosi (Ray) akisalimia wakazi wa Iringa


Steve Nyerere akitambulisha wakazi wa Iringa kikundi cha Bongo Movie

Masanja Mkandamizaji akisoma risala




Mke wa blogger Fracis Godwin wa Iringa akiwa na mwanae Falavian

Martha Baraka akimzindikiza mwimbaji mwezake Masanja



Mwimbaji wa nyimbo za injili Martha Mwaipaja akimtumikia BWANA


Watu waliohudhuria tamasha hilo uwanja wa Samora mjini Iringa wakati wa tamasha la Emmanuel Mgaya










Hotel ya Blue View na Fan Lodge ndio wadhamini wa tamasha hili

NAKUSHUKURU FRANCIS GODWINI KWA PICHA ZAKO

No comments:

Post a Comment