INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Wednesday, July 15, 2015

Kama Wewe Ni Kijana Chini Ya Miaka 40 Soma Alichoandika Ray.

"Watu wengi hawajui kwa nini wazungu huwa wanasema LIFE BEGINS AT 40. Yaani maisha yako ya kweli yataanza ukifika umri wa Miaka 40. Wakati ambapo unatakiwa uwe na elimu uliyoihitaji.. Uwe na familia yako tayari.. Uwe na kwako tayari siyo umepanga bado.. Uwe na usafiri binafsi.. Uwe na kitu chako cha kukuingizia pesa na si kutegemea ajira peke yake. At 40!

At 40 unatakiwa uwe umeshapata exposure kwa kusafiri huku na ule dunia hii kujua wengine walioendelea zaidi wanaishi vipi na wewe ufanyeje? Umekuwa mtumwa wa simu. Ikikosa network unalalamikia kampuni ya simu utafikiri hiyo network unafanyia kitu cha maana Zaidi ya kusubiri m2 akosee Kiingereza basi hiyo ndio inakuwa mada ya siku nzima mnachelewa wenzenu wanapiga pesa nyinyi kazi yenu kujifanya wazungu. Kama kiingereza ni dili kiambie kikupe Pesa.
Kwani wanasoka wangapi wako kama Beckham Wnamuziki wangapi wako kama Kirk Franklin Wacheza Tennis wangapu wako kama Roger Federer?
Unadhani amekuwa champion akiwa amekaa na simu chumbani ana comment kuhusu huyu hajui kiingereza? No. Alikuwa ana-hussle wakati wengine wanacoment ujinga.
Miezi hii 6 iliyobaki kumaliza mwaka huu 2015 umeweka mikakati gani kuweka msingi wa maisha tofauti sana na kuhakikisha ufikapo umri wa miaka 40? Au bado unategemea mshahara wa laki 8 (tena hapo kabla ya makato) uje ubadili maisha yako).
Microsoft ya Bill Gates inapunguza wafanyakazi 800. Kama ulikuwa hujui. Unadhani kampuni yako ndo utakaa hapo milele?Be Careful Bill Gates huyo huyo anasema "KAMA ULIZALIWA MASKINI HILO SI KOSA LAKO..LAKINI UKIFA MASKINI HILO NI KOSA LAKO" Ni Mtizamo 2.
Kijana Amka Wakati Ndio Huu Wa Kupambana Maisha Wacha Kufuatilia Maisha Ya Wa2 Yani Fanya Ya Kwako Umri Unakwenda Over."
Vicent Kigosi 'raythegreatest' on instagram

No comments:

Post a Comment