INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Friday, January 1, 2016

TV Zimeua Tamthilia Za Kitanzania: Mzee Chilo

Msanii wa filamu, Mzee Chilo amedai wamiliki wa runinga nchini ndio waliosababisha kupotea kwa tamthilia za nyumbani kwa kuzikwepa na kuonesha za kigeni.
Muigizaji huyo ambaye pia ni mmiliki wa kampuni ya Pilipili Entertainment, ameiambia Bongo5 kuwa hali hiyo imesababisha wazalishaji wa filamu nchini kukaa na kazi zao ndani bila kuwa na sehemu za kuzipeleka.

“Kilichopoteza tamthilia zetu ni runinga zetu, wakawa wanaamua kuonesha tamthilia za kigeni sijui kwao ndio zilikuwa rahisi?” amesema Chilo.
“Lakini sasa hivi naona wameanza kurudi na kutuona sisi ni wa muhimu, wanajali kazi zetu. Hii italeta makubwa katika tasnia yetu kwa sababu wasanii wanajengwa na tamthilia, hao wote wanaotajwa akina Ray, Kanumba na wengine wametokana na tamthilia kwa sababu tamthilia unaangalia nyumbani kwako na familia yako,” ameongeza.
Pia Mzee Chilo amesema baada ya kupata serikali inayowasikiliza wananchi wake ana imani kila kitu kitaenda sawa mwaka 2016.
Chanzo: Bongo5

No comments:

Post a Comment