INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, March 21, 2016

Bongo Movie Wamtenga Lulu ?

Hali hiyo ya sintofahamu ilijidhirisha Jumanne iliyopita kwenye hafla ya kumpongeza Paul Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam iliyoandaliwa na wasanii wa Bongo Muvi chini ya uratibu wake, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ katika Hoteli ya Rodizio iliyopo Masaki, jijini Dar.

“Jamani! Mbona Lulu hajifunzi kutokana na makosa? Juzi alipokuwa akirudi na tuzo kutoka Nigeria, hatukwenda kumpokea kutokana na yeye kutokupenda kujumuika na wasanii wenzake, angalia sasa, hata leo hajaja kama kawaida yake.
“Nilidhani atabadilika kumbe wapi. Anapaswa kubadilika sababu sioni cha kumzuia, mbona akialikwa kwenye pati za rafiki zake huwa anakwenda lakini sehemu kama hizi haji? Kilichotokea Airport ni funzo tosha, Mungu alimpa na akiendelea hivi siku atakumbana na majanga mazito atakosa wa kumsaidia,” alisikika mmoja wa wasanii waliokuwepo katika hafla hiyo.
Mara baada ya kupokea malalamiko hayo, mwandishi wetu alimtafuta Lulu na kumsomea mashtaka yake ambapo alifunguka hivi:
“Sababu zangu kutohudhuria katika hafla zao wao wenyewe wanazijua na wakizijua wao inatosha siyo lazima nikwambie na wewe (mwandishi). Elewa tu hivyo.”

No comments:

Post a Comment