INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, June 30, 2014

STEVE NYERERE ASIMIKWA UKAMANDA CCM TAWI LA BWAWANI

MWENYEKITI wa Bongo Movie Unity Steven Mangere ‘Steve Nyerere’ jana amesimikwa kama kamanda wa Tawi la Bwawani lilopo katika Kata ya Mwananyamala, hivyo msanii huyo kugeukia masuala ya siasa na kuahidi kuwapigani wasanii na wakazi wa eneo hilo.

Tukio hilo liloongozwa na Paul C. Makonda leo Mbunge wa Bunge maalum la Katiba, moja ya kazi aliyofanya kiongozi hiyo ni kufungua mashina ya wakereketwa (Wajasiliamali) na Kumsimika Kamanda wa Vijana wa Tawi la Bwawani Ndg. STEVEN MANGERE aka Steve Nyerere.

Katika kusherehesha sherehe hizo za Kumsimika kamanda huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bongo Movie Tanzania wasanii mbalimbali wa Bongo fleva na wasanii wa filamu walitoa burudani ya kufa mtu… Hakika sherehe zilifana kupita kiasi.

Baadhi ya wasanii na waigizaji wa filamu waliokuwepo hapo ni Jacob Stephen ‘JB’, Single Mtambalike ‘RICHIE RICHIE, Haji Adam ‘BABA HAJI’, Juma Chikoka ‘CHIKOKA’ Blandina Chagula ‘JOHARI’, KIM, Herieth, SANDRA, Jennifer Kyaka ‘ODAMA’,Rose Ndauka…MSAGASUMUkundi la MAKOMANDOO na wengineo kibao.

“Safari ya mafanikio ya mwaka 2014 tumeshaianza DSM,tutarudisha Majimbo,Kata na hata mitaa ukiwemo mtaa wa Bwawani ambao ulichukuliwa na wapinzani,”anasema Kamanda Steve Nyerere.

Sambamba na Mgeni Rasmi pia kulikuwepo na viongozi mbali mbali wa CCM na UVCCM, ambao ni Mjumbe wa Baraza kuu la UVCCM Taifa, William J. Malecela aka Le Mutuz Baharia,Mjumbe wa NEC Asha Baraka, Katibu wa UVCCM Mkoa DSM Kidando, Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi Mkoa wa DSM Komred Saady Khimji, Katibu wa UVCCM Wilaya ya Kinondoni, Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi Wilaya Kinondoni ndg Omar Omary Bomba, na viongozi mbalimbali wa Kata na Tawi, bila kumsahau Mwanamitindo Maarufu ndani na nje ya Tanzania Asia Idarous naye alikuwepo. PICHA KWA HISANI YA LE MUTUZ.


Steve Nyerere mwenyekiti wa Bongo Movie Unity.


Steve Nyerere akipitia katika matawi ya CCM

Steve Nyerere, Mike Sangu, Le Mutuz

Steve akisimikwa ukamanda na Mh. Paul Makonda

Bi. Mkubwa akifurahia kijana kuwa kamanda na kumtandika na gift ya likanga.



Steve Nyerere akivishwa ukamanda rasmi na Mh. Paul Makonda

Steve Nyerere tayari Kamanda kamili na ngao

No comments:

Post a Comment