INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, June 30, 2014

TICO WA BONGO MUVI NDANI YA KENYA..ANATISHA

Filamu ya Sio Riziki inatayarishwa na mtayarishaji Sabby Angel inaaminika kuwa ndio itakuwa kazi ya kipekee kulingana na muunganiko uliopo kutoka Kenya na Tanzania, sinema hiyo inarekodiwa na kampuni ya Coastal Film Production ya Kenya.

“Ni kazi ambayo kwangu imekuwa chachu ya mafanikio kuweza kuongoza filamu inayoshirikisha wasanii mastaa wan chi mbili za Afrika Mashariki ni hatua kubwa kwangu, pia nipo na Director msaidizi wangu Hassan Feisal anaheshimika sana Kenya,”anasema Tico.

Mzigo huu wa hatari unawakutanisha mastaa wanaong’ara katika tasnia ya filamu Bongo kama Amri Athuman ‘King Majuto’, Hisani Muya ‘Tino’, Kulwa Kikumba ‘Dude’, Sabby Angel na wasanii wakali kutoka Kenya, tunausubiri mzigo kwa hamu .

Wasanii wa filamu wa Swahiliwood na wasanii wa Kenya

DIRECTOR anayekuja kwa kasi Swahiliwood Timoth Conrad ‘Tico’ yupo nchini Kenya na wasanii nyota wa Bongo wakirekodi filamu kali nay a kusisimua ya SIO RIZIKI akiongea na FC live kutoka Mombasa amesema kuwa wasanii nyota wa Kenya wanashiriki katika filamu hiyo.

Tico akiongoza filamu ya Sio Riziki kwa umakini


mpiga picha


Wasanii wakiwa katika picha ya pamoja
Mwanadada akiwa na Camera onset
Tico akiwa kazini
Tino na Dude wakiwa location
Tino akiwa katika moja ya scene
Tino akirekodi katika moja ya maduka

No comments:

Post a Comment