INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Thursday, June 14, 2012

TUZO ZA FILAMU KUANZA MWEZI UJAO
 
Na Mwandishi Wetu

TUZO za kwanza kabisa za waigizaji wa filamu zimepangwa kufanyika mwezi ujao. Mratibu wa tuzo hizo kutoka kampuni ya Bantu Film Award, Stuart Kambona, alisema kuwa hatua ya kuanzisha tuzo hizo inatokana na muitikio wa soko la filamu za Tanzania kwa hivi sasa tofauti na awali.

Alisema kuwa Watanzania wengi walikuwa wanapenda zaidi filamu za kigeni na kuzipuuza filam za wasanii wa Kibongo wa hapa nyumbani.

Alisema kuwa kutokana na mapinduzi yaliyofanywa na wasanii wa fani hiyo, filamu za Tanzania kwa sasa zina soko la hali ya juu na imtokana na tabia ya watanzania kubadili mwelekeo. Alisema kuwa ili kuhakikisha Tanzania inafikia hatua ya Hollywood, wameamua kutoa tuzo kwa wasanii waliofanya vizuri na kuifikisha fani hiyo katika hatua ya sasa.

“Tunaamini kuwa kupitia tuzo hizi, waigizaji au wasanii wa filamu watatengeneza filamu zenye ubora wa hali ya juu ili kuweza kutwaa tuzo na soko kwa ujumla, tunaamini tutafikia lengo letu japo tumebakisha muda mfupi mpaka tuzo zenyewe kufanyika,” alisema Kambona.

Alisema kuwa kwa kuanzia watashindanisha filamu zote za Tanzania ambazo kwa sasa zipo sokoni ili kutoa fursa kwa kila msanii wa fani hiyo kushindana. Jumla ya tuzo 28 zitashindaniwa kwa mwaka huu.

Baadhi ya tuzo hizo ni Filamu Bora, Muongozaji Bora, Muigizani Bora mkuu wa Kiume, Muigizaji Bora Mkuu wa Kike, Msaidizi Bora Mkuu msaidizi wa kike na wa kiume, msanii chipukizi bora, filamu ya asili, Mpiga picha bora, Best Sound Track, Best Make-Up artist, Best Costume Designer, Best Documentary, Best Visual effect, best Film editor, best script na Tuzo ya Heshima.

Tuzo nyingine ni Outstanding Pioneer, Best Comedian, Best Cover Design, Best producer, Best Distributor, Best Action Movie, Best African Film outside Tanzania, Best Ligting, Best Sound na Best Story.

Muigizaji nyota wa kike nchini, Irene Uwoya aliwapongeza waandaaji hao kwa kuanzisha tuzo hizo ambazo alisema zitawapa changamoto kwao kuandaa filamu za ushindani.

Alishukuru kampuni ya Bantu kwa kuanzisha tuzo hizo ambazo anaamini zitawafanya kuandaa filamu zenye ubora wa hali ya juu.

"Tuzo hizi zitatufanya tufanye kazi nzuri zaidi ili kuingia katika ushindani, natoa wito kwa waigizaji wenzangu kufanya kazi kwa umakini ili kuleta msisimko na ushindani zaidi," alisema Uwoya.

Muigizaji Mkongwe, Jacob Steven (JB) alisema kuwa anaamini tuzo hizo zitawafikisha pale ambao wao wamekusudia na vile vile kuibua vipaji vingine katika tasnia hiyo.

JB alisema kuwa tuzo hizo zitawafanya mashabiki wao kujua undani wa fani yao kwa kuwajua watunzi bora, wapiga picha bora na wengineo.

No comments:

Post a Comment