INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Friday, June 29, 2012

MABADILIKO YA MUIGIZAJI WA FILAMU TANZANIA-WEMA SEPETU
Hizi ni picha tofauti za mcheza filamu nyota wa kike Tanzania, Wema Abrahamu Sepetu kuanzia anashiriki shindano la Miss Dar Indian Ocean mwaka 2006, Miss Kinondoni, Miss Tanzania na Miss World hadi sasa. Je, ni Wema wa wakati gani alikuvutia zaidi na kwa sababu gani? Toa maoni yako mdau.


Alivyo sasa














Monday, June 25, 2012

OMOSEXY-OMOTOLAH NA WEMA SEPETU NDANI YA GIRAFFE OCEAN VIEW HOTEL KATIKA UZINDUZI WA SUPERSTAR

Wema Sepetu akiwa na mgeni wake Omotolla Jalade ndani ya Hotel ya Giraffe katika uzinduzi wa Filamu yake ya SUPERSTAR.Omotolla ni mmoja kati ya maactress hatari ndani ya kiwanda cha NOLLYWOOD Nigeria.Hakika ujio wake ni chachu kubwa kwa wasanii wa filamu nchini haswa sisi kinadada,tunatakiwa tuige kutoka kwake nini wanafanya mpaka wanatajirika na kupata kazi nyingi mpaka kufika  HOLLYWOOD.Hakika kwa hili tunatakiwa kumpongeza WEMA kwa kumleta msanii huyu mkubwa nchini.

Nikiwa na OMOTOLLA,Hakika nafasi hii  niliipenda sana


Davina akiwa na OMOTOLLA
Nesh akiwa na Omotolla

Rachel akiwa na OMOTOLLA JARADE

Mtitu Bw Harusi mtarajiwa  hakuwa nyuma kupata picha na OMOTOLLA

Wasanii wa BONGO MOVIE hawakuwa nyuma katika kumsapoti msanii mwenzao

Rachel,Davina na Nesh wakiwa na WEMA ndani ya Giraffe Hotel baada ya uzinduzi wa Filamu ya SUPERSTAR

Nikiwa na Wema Sepetu

Omotolla akienda kupumzika baada ya uzinduzi wa filamu kuisha akisindikizwa na Manager wa Wema Martin Kadinda na Rachel na mdau wa filamu

Tukitoa Hiiiiiiiiiii

UZINDUZI WA FILAMU YA SUPER STAR HYATT KILIMANJARO KEMPINSKI

Uzinduzi wa Filamu ya SUPERSTAR uliofanyika ndani ya Hotel ya Hyatt Kilimanjaro hakika umetoa fundisho kwa wasanii nchini kuwa tukijitahidi tunaweza kufika kule tunapotaka.Hakika Wema Sepetu anastahili sifa kubwa sana kwa kufanya uzinduzi wa aina yake uliojaa wasanii wa filamu,bongo fleva,dansi na wafanyabiashala mbalimbali,Huu ni uzinduzi wa pili wa Filamu unaofanyika nchini na katika mahoteli makubwa,wa kwanza alifanya steve Nyerere ndani ya hotel ya Serena Hotel.Hakika wote hawa wawili wanahitaji pongezi kubwa.Sisi wasanii tupo pamoja na wewe katika kukupongeza kwa kazi kubwa uliyofanya.HAKIKA UMETHUBUTU NA UMEWEZA HONGERA SANA.

Nikihojiwa na television ya Clouds

Shostito wangu Rachel akiwa anatabasamu

Nikiwa na Mama Erieth

Steve Nyerere hakika alifunika sana maana alikuwa na mabaunsa kama watatu wanaomlinda,pembeni hapo ni mmoja kati ya walinzi wake

Nikipiga story na THE GREATEST

Richie akiwa na Zungu

Mimi Rachel na Ma Erieth

Chopa akiwa na Irine Uwoya

Charles Baba akiwa na Ommy Dimples

Mama Lollaa akiwa na Nyerere

Ebwanae cheki mapozi hayo

Barnaba akiwa na Ray wakipiga maneno

Shilole,alifunika sana kwa nyimbo zake

Izzo B,Akiwa na Quick Racka

Mapozi hayo

Muda wa kuangalia movie ulifika na hapa SUPERSTAR ilikuwa live

Wacha wewe mtoto mapozi hayo


JB akipata menu

Shaa akipiga mzigo

THT wakifanya kazi jukwaani

Saturday, June 16, 2012

MCHEZASINEMA MAARUFU TOKA MAREKANI KUKIMBIA MBIO ZA MT. KILI MARATHON


Mcheza sinema maarufu duniani kutoka nchini Marekani Deidre Lorenz atakimbia mbio za kila mwaka za Mount Kilimanjaro Marathon zinazoanza kutimua vumbi kuanzia tarehe 24 Juni mwaka huu kutoka Moshi Club mjini Moshi.
Mbio hizi zilizoanzishwa na mama Marie France kutoka katika mji wa Bethesda, Maryland nchini Marekani mwaka 1991 ni mbio zinazojulikana kama 7 continental Races na zimeshawahi kupata tuzo mbalimbali za kimataifa.

Ujio wa mcheza sinema huyu aliyecheza sinema nyingi kama vile Santorini Blue, Perfect Strangers, The Great Fight, na nyingine nyingi unaiweka Tanzania katika macho ya dunia na kuwavutia watalii wengi kutoka taifa hili tajiri duniani. Deidre Lorenz alizaliwa katika jiji la Oregon nchini Marekani lakini akahamia katika jiji la New York City linalijulikana kama "The Big Apple" nchini Marekani akiwa na kampuni yake ya kutengeneza sinema inayoitwa Thira Films LLS.

eidre Lorenz ameshawahi kuteuliwa zaidi ya mara tatu kugombe tuzo za wacheza sinema maarufu duniani zinazojulikana kama Grammy Awards. Mcheza sinema huyu ataambatana na Wamarekani wengine kuja nchini tarehe 21 Juni kukimbia mbio hizi ambazo zimetokea kuutangaza sana mji wa Moshi tangu mwaka 1991. Lorenz alipatikana katika bahati nasibu iliyochezwa wakati wa mbio za New York Marathon mwaka jana.

Naye mwanzilishi wa mbio hizi mama Marie Frances ana historia ya kuanzisha mbio na matamasha mbalimbali duniani. Alikuwa pia mwanzilishi wa mbio za Pyramid Marathon nchini Misri pamoja na Miss Universe Egypt matamasha yaliyojizolea sifa kemkem.Aliombwa kuja kuanzisha mbio za Marathon nchini Tanzania na balozi wa Tanzania wa wakati ule nchini Misri.Mbio za Mt. Kilimahjaro Marathon ni moja kati ya mbio tafauti za marathon zinazifanyika katika mji wa Moshi.

Mount Kilimanjaro Marathon zitaanzia Moshi Club mpaka Rau madukani na kurudi mara tatu ambazo zitakuwa kilimeta 42. Kutakuwa pia na mbio z akilometa 21, kilimeta 10 na kilometa 5 kwa watoto. Wakimbiaji hawahitaji kuwa na ujuzi wa kukimbia watu wote wanaweza kukimbia.

FIILAMU YA "HOUSE MAID" KUWA SOKONI SI MUDA MREFU KUANZIA SASA.
Jenifer Kyaka amesema filamu yake mpya ya "House Maid" itakuwa sokoni si muda mrefu kuanzia dakika hii, kwahiyo wapenzi wa filamu zake waanze kukusanya pesa kidokidogo ili siku ya kutoka hiyo filamu uwe wa kwanza kuiona. Utajifunza mengi kwa kupitia filamu hii ya "House Maid"

Wataarifu na jamaa zako ambao hawajabahatika kupata habari hizi kwa njia ya mitanda

NDOA YA H-BABA, FROLA HAIELEWEKI !!!!
Ndoa ya nyota wanaotamba kupitia fani ya muziki na filamu Bongo, Hamis Ramadhan Baba, ‘ H-Baba’ na Frola Mvungi, bado iko gizani kufuatia, kijana huyo kushindwa kufikia uamuzi.


Akizungumza ‘live’ na mtandao namba moja kwa stori za mastaa (Teentz.com) H-Baba amesema kuwa hana uhakika kama jambo hilo linaweza kupewa nafasi hivi sasa kwa kuwa kuna mambo mengi yanyomfanya kushindwa kufikia uamuzi wa kufunga ndoa na mwigizaji huyo

“Bado kuna utata, sijafikia uamuzi wa kufanya jambo hilo hivi sasa, sitaki kusema sana kwa sababu najua kuna watu ambao wanajaribu kuingilia uhusiano huu, ki ukweli sijafikia uamuzi kuna mambo madogo madogo bado nayachunguza kwa mwenzangu na wakati ukiwadia basi kila kitu kitakuwa wazi” alisema H-Baba aliyeingia kwenye uhusiano na Frola mwaka mmoja uliopita.







SOURCE: DJ Fetty

Thursday, June 14, 2012

BANTU FILM AWARDS

Kilio cha muda mrefu cha wasanii wa Tanzania sasa kimefika kikomo baada ya wadau kujitokeza na kuanzisha tuzo ambazo zinaitwa Bantu Film Awards zinategemewa kufanyika mwezi ujao katikati tarehe na siku tutawajuliisha kupitia blog yako ya The Greatest, leo kulifanyika mkutano na waandishi wa habari katika hotel ya Serena kuzungumzia tuzo hizo, embu twende tuone mambo yalivyokuwa.....






Wasanii wa Bongo Movie wakiwa tayari kuanza mkutano na waandishi wa habari.

The Greatest, Richie na Jb wakimfuatilia mratibu wa tuzo za Bantu Film awards bwana Stewart akifafanua jinsi tuzo zitakavyokuwa

Irene Uwoya naye alikuwepo amesema kuwa amepania kuzoa tuzo za mwaka huu..

Tukiwa makini kufatilia kikao na mambo yatakavyokuwa.
Stewart ndiye Mratibu wa Bantu Film Awards
Stewart akiendelea kutoa ufafanuzi jinsi tuzo za Bantu zitakavyokuwa kwa waandishi wa habari
Safi sana kwa kweli wasanii wa Tanzania tumekuwa na faraja kubwa juu ya tuzo hizi za Bantu
Mambo yakiendelea........
Jb mwenyekiti wa Bongo Movie
The Greatest
Irene Uwoya
Single Mtambalike
Ulifika muda wa Jb kuongea yake machache kuhusu tuzo za Bantu, Kubwa alisisitiza kuwa umefika muda sasa ya wasanii kufanya kazi zenye ubora wa Kimataifa maana hiki ndicho kilkuwa kilio chetu cha muda mrefu sana maana hata wanafunzi wanapokuwa wanasoma lazima mwisho wa mwaka ukifika wanafanya mitihani kama kipimo cha mwaka mzima alichosoma na ndio maana leo nasi tumekuwa na kitu kama hiki cha kujipima kuwa ndani ya mwaka mzima umefanya kitu gani.
Hayo yalikuwa ni maneno ya Jb akiwawakilisha wasanii wa Tanzania nzima..
Waandishi wa habari wakifanya kazi zao kama kawaida yao
Mambo yakiendelea kupamba moto
Irene Uwoya naye akiongea yake machache
Single Mtambalike (Richie) naye akiongea mambo ya msingi yanayotakiwa kuzingatiwa katika tuzo hizo
Ulifika muda wa maswali na majibu toka kwa waandishi wa habari
Nikisikiliza swali toka kwa mwaandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi...
Mratibu akilijibu swali ilo kwa ufasaha
Waandishi wa habari wakisiliza jibu kwa ufasaha
Maswali yakiendelea kuulizwa kikubwa waandishi walikuwa wanataka kujua ni vigezo vipi vitakavyotumika kuwachagua watakaokuwa bora kwa mwaka huu