INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Wednesday, January 21, 2015

MAMBO AMBAYO HUKUYAJUA KUHUSU STAA WA NOLLYWOOD ALIYEFARIKI, MUNA OBIEKWE


KIFO cha staa wa Nollwood, Muna Obiekwe kimezua gumzo kwa watu wengi nchini Nigeria na wengine ambao wanafuatilia tasnia ya filamu nchini Nigeria, sasa kuna mambo kadhaa ambayo yawezekana ulikuwa huyajui kuhusu staa huyo aliyefariki kutokana na matatizo ya figo.

Staa wa Nollwood, Muna Obiekwe enzi za uhai wake.

Alikuwa muoga wa waandishi wa habari
Muna hakuwa tayari kujitokeza hadharani kuomba kuchangishiwa fedha kwa kuwa alikuwa muoga wa kuonekana kwa waandishi wa habari na alipenda maisha yake binafsi yasijulikane.

Muna alikuwa mlevi
Inaelezwa kuwa alikuwa akinywa pombe sana licha ya kuwa daktari alimkataza kufanya hivyo. Alikuwa akijihudumia mwenyewe bila msaada wa watu wengine, lakini baadaye siku za mwisho za uhai wake alipata msaada mkubwa kutoka kwa Patience Ozokwor na Kanayo O.

Alimfuata Ibinabo Fiberesima
Licha ya kuwa alikuwa mtu aaibu sana, siku za mwisho za uhai wake aliwasiliana na muigizaji wa kike wa Nollywood, Ibinabo Fiberesima lakini hakuwa na msaada kwa kuwa alifariki siku chache baadaye.

Muna alijua tatizo lake siku nyingi
Alijua tatizo hilo siku nyingi lakini inaelezwa kuwa alijua atalitatua kimya kimya, aliyapuuzia maumivu aliyokuwa akiyasikia.

Muna alikuwa na mke na watoto wawili
Wengi hawakujua lakini alikuwa ni baba wa familia na mwenye watoto wawili.

ANGALIA FILAMU HII ALIYOSHIRIKI


No comments:

Post a Comment