INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Sunday, October 20, 2013

HEMEDY NDANI YA PENZI ZITO NA ZUHURA GORA ....


Hemedy na Zuhura Hemedy Suleiman ambaye ni star anayetamba Swahiliwood na pia katika muziki wa Bongofleva anatoka kimapenzi na Zuhura Gora ambaye ni model na pia mwigizaji wa filamu akiwa ameigiza filamu kama vile The Beauty Fools. Chanzo makini kilicho karibu na wawili hao kiliiambia Swahiliworldplanet juzi kuwa ni muda kidogo wawili hao wapo katika penzi zito ingawa wengi wakiwemo mashabiki wao hawajui."sikia nikuambie lakini usinitaje, Hemedy na Zuhura ni wapenzi na muda wowote wakitangaza ndoa msijemkashangaa" kilisema chanzo hicho

Hata hivyo mtoa habari huyo alisema kuwa Hemedy bado kama anajifichaficha kumuweka hadharani Zuhura ili kila mtu ajue kuwa ni wapenzi huku Zuhura akijisikia huru kuwa na Hemedy kama boyfriend wake. " but unajua bado Hemedy kama hajawa tayari kumuweka hadharani Zuhura kama mtu wake lakini Zuhura yuko peace sana na relationship yao" kilimwaga data chanzo hicho. Zuhura alipotafutwa leo na Swahiliworldplanet ili kudhibitisha habari hizo alikubali kuwa ni wapenzi yeye na Hemedy kwa kujibu kwa ufupi "Yeah ni boyfriend wangu"

Zuhura ambaye ni model mwenye vigezo vyote vya kuwika kimataifa katika tasnia hiyo tayari ameonekana kwenye video za wasanii wakubwa wa Bongofleva kama vile Kamili Gado ya Profesor Jay.


-CHANZO:Swahili wold Planet

No comments:

Post a Comment