INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Friday, October 25, 2013

MAMA KANUMBA ALIA NA MCHUNGAJI KAIRUKI KWA KUDAI KANUMBA YUKO HAI

Source: Vituko vya Mtaa

Baada ya hivi karibuni kuibuka tena kwa yule nabii na Mchungaji George Kaiuruki na kudai kuwa Marehemue Steven Kanumba bado yu hai, FROLA Mtegoa - mama mzazi wa aliyekuwa mwigizaji nyota filamu wa Bongo marehemu Steven Kanumba amesikitishwa na tabia ya mtu anayejiita Nabii George Kairuki kwa kutumia jina na kifo cha marehemu mwanaye kama njia ya kujitengenezea fedha na umaarufu, mama Kanumba anasema kuwa awali Kairuki alitumia msiba wa mwanaye katika kuongelea vitu ambavyo hata familia haivijui isipo kuwa yeye pekee yake.

Mama Kanumba anadai kuwa hivi karibuni Kairuki alijitokeza kwa kudai kuwa Kanumba hajafa na amemtumia fedha katika simu yake, na kusema kuwa karibu atamrudisha duniani na kuendelea na maisha yake jambo ambalo mama wa marehemu anapingana nalo kwa kusema kuwa yeye kwa imani yake anaamini kuwa mwanaye amefariki na hakuna miujiza mingine.

“Huyu mtu anayeitwa Nabii George Kairuki sijui anatafuta nini katika familia yangu, Kanumba alikuwa ni kipenzi cha watu na sisi sote tumeshuhudia hilo kama kweli yeye ana uwezo wa kumfufua amfufue watu wote watafurahi kipenzi chao kurudi kama anavyosema yeye, mimi simjui hata sura zaidi ya kumuona katika picha,”anasema mama Kanumba

Mama Kanumba anasema kuwa iwapo Kairuki ataendelea na tabia hiyo itabidi afanye utaratibu wa kumfungulia mashitaka na hata ikibidi kumfungulia mashitaka na kumfunga endapo ataendelea na tabia ya kutumia sana jina la Kanumba katika kujitafutia fedha na kutangaza maneno ya ajabu ajabu.

No comments:

Post a Comment