INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, October 21, 2013

WARIDI ALIA NA MAADILI KATIKA FILIMU ZA KIBONGO..










Muigizaji wa siku nyingi Anna Costantine maarufu kama Waridi ambaye alitamba sana mwishoni mwa miaka ya tisini amesema kuwa maadili ya kitanzania na kiafrika yameshuka sana katika filamu zetu mpaka ni aibu kutokana na kuiga sana uzungu ambao hata wazungu wenyewe hawafanyi hasa kwa waigizaji wa kike. Akizungumza na Mwananchi Waridi alisema "maadili yameshuka, hatuendani na maadili ya mwafrika, wanaiga sana umagharibi, tunaiga mpaka inakuwa aibu, hata wazungu hawafanyi hivyo"

Waridi ambaye alitamba enzi hizo na kina Monalisa, JB, Bishanga na Aisha alipoulizwa kuwa anategemea kurudi lini katika filamu alisema "mwanzoni mwa mwaka ujao nitarejea, nimejipanga vilivyo, ni lazima nifanye vizuri, nina kipaji, nimesomea kazi hii(chuo cha sanaa Bagamoyo), pia nina karama ya uigizaji, nitarudi kwa kasi, nitatingisha kama awali"

No comments:

Post a Comment