INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Thursday, October 10, 2013

MZEE MAJUTO ATANGAZA KUGOMBEA UBUNGE 2015, NI WAPI NA KWA CHAMA GANI? BOFYA HAPA



MCHEKESHAJI mkongwe nchini, Amri Athuman 'King Majuto' ametangaza nia yake ya kujitosa kwenye siasa akitaka kuwania Ubunge katika Jimbo la Tanga Mjini katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015.
Akihojiwa na kituo cha Clouds FM, Mzee Majuto mwenye umri zaidi ya miaka 60, alisema Mungu akimjalia atajitosa kwenye ubunge jimboni humo kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), akidai kiu hiyo imechochewa na mafanikio ya wasanii waliojitosa kwenye siasa na kufanya vyema.

Mzee Majuto alisema, uzoefu alionao katika kuishi kwake mjini Tanga itamwezesha kuwatatulia kero na kuwaletea maendeleo ya kweli wananchi wenzake iwapo Mungu atamjalia katika kusudio lake.
Kadhalika Muigizaji, ambaye pia ni mtayarishaji na muongozaji wa filamu nchini, Yekonia Watson 'Amani' amesema matarajio yake miaka michache ijayo ni kujitosa kwenye siasa akitaka kuwania Ubunge kabla ya kuangalia nafasi ya juu zaidi kwa maana Rais.

Akizungumza na MICHARAZO jioni, Watson alisema anaamini ana uwezo na kipawa cha uongozi hivyo anaweka mambo sawa kabla ya kujitosa jumla kwenye duru hilo, japo yeye hakuweka bayana atajitosa kupitia chama gani.
"Kwa sasa ni mapema mno, ila nitaanzia Ubunge kisha kuangalia nafasi ya juu, ila muhimu Mungu anipe uhai na umri wa kufanikisha hilo," alisema mkali huyo anayejiandaa kuachia filamu yake mpya iitwayo 'Uwanja wa Vita' aliyoigiza na wasanii kadhaa nyota akiwamo Irene Uwoya.

Source: Vituko vya Mtaa

No comments:

Post a Comment