INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, October 12, 2015

Tatizo La Umeme Linasababisha Tasnia Ya Filamu Kuzorota: Dr.Cheni

Msanii wa filamu, Dr Cheni amesema kuwa biashara ya filamu kwa sasa imeshuka kutokana na tatizo la umeme linaloendelea.
Dr Cheni ameambia Bongo5 kuwa mawakala wanalalamika kushindwa kuuza kazi za filamu kama walivyotarajia kutokana na tatizo la umeme.

“Soko la filamu sasa hivi linasumbua kutokana na haya matatizo ya umeme,” amesema Cheni. “Umeme ukisumbua na soko la filamu linayumba kwa sababu sisi wateja wetu wanatumia umeme, sasa hata wazalishaji wa kazi zetu wanaogopa kuzalisha kazi nyingi kutokana na kutonunulika sokoni. Yaani kwa kifupi soko limesimama. Wewe nenda kwa mawakala pale Kariakoo watakwambia. Kwahiyo ukiona tatizo la umeme ujue na sasa kazi zetu zinasimama.”
Chanzo: GPL

No comments:

Post a Comment