INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Thursday, September 17, 2015

Odama Asema Yeye Si Wa Kuchezewa Hovyo Hovyo.

Jennifer Kyaka ‘Odama’ amesema miongoni mwa mambo ambayo kamwe hayafanyii mzaha ni pamoja na kuruhusu mwili wake ‘uguswe’ kwa urahisi na wanaume wakware.
‘Akibananishwa ukutani’ na ‘kisabengo’ wetu kwa maswali magumu juu ya kutoonekana hadharani au kumwanika mwandani wake hivi karibuni, Odama alisema yeye ni mwanamke thabiti aliyelelewa katika maadili halisi ya kiafrika, hivyo suala la kuwa na mwanaume halihitaji ‘promo’ kwani ni kawaida kwa mtu mzima aliyekamilika kuwa na mwenzi, huku akiweka bayana kuwa mwili wake si sadaka hivyo haguswi kirahisi.

“Kwani kuwa na mwanaume ni fasheni? Nimelelewa na familia yenye maadili ya kiafrika, suala la kuwa na mwandani si biashara wala matangazo, kwa hiyo nikiwa naye si lazima kila mtu ajue au amjue, kwanza mimi si mwanamke rahisi, mwili wangu hauguswi hovyo na wanaume wakware, unanionaje? Najielewa na kujitambua,” alisema Odama.
Chanzo: GPL

No comments:

Post a Comment