INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Tuesday, December 22, 2015

Aunty Ezekiel Na Moze Iyobo Kupata Mtoto Mwingine.

Staa maarufu wa filamu Bongo, Aunty Ezekiel amefungua kinywa chake na kusema kuwa kwa sasa yuko kwenye mchakato wa kumtafuta mdogo wake na Cookie kwa kuwa hataki kukaa muda mrefu ili kupata mtoto mwingine.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni Aunty,alisema kuwa ameamua kufanya hivyo kwa kuwa anaona kuzaa mapema na kumaliza ndiyo poa ili aweze kuendelea na kazi zake vizuri kuliko kukaa muda mrefu halafu ndiyo ubebe ujauzito tena.

“Sasa hivi mimi na baba Cookie tumeshaamua kufanya maamuzi mazuri kabisa ya kuongeza mtoto mwingine maana tumeona kwanza ndiyo furaha yetu kubwa na kitu kingine tukizaa haraka ni vizuri zaidi tunaweza kufanya kazi zetu kwa ajili ya kusomesha na si kufikiria kuzaa tena,” alisema Aunty.
Chanzo: GPL

No comments:

Post a Comment