INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Thursday, October 11, 2012

MESEJI ZA MAPENZI ZA WAZIRI ZANASWA ZIKIWA NJIANI KWENDA KWA LULU MICHAEL


Meseji zenye maneno ya kimahaba za kumshawishi kimapenzi staa wa filam za kibongo Lulu Michael kutoka kwa waziri wa wizara moja nyeti serikalini zimezagaa mitaani....

Kwa sasa Lulu  yupo nyuma ya nondo katika gereza la segerea akikabiliwa na kesi ya mauaji ya Steven Kanumba....

Inaelezwa kuwa mawasiliano ya wawili hao yalianza miezi kadhaa kabla ya Lulu kukutwa na msaala huo....

Vyanzo vyetu vya habari vinaeleza kuwa meseji hizo zimetoka kwa aliyekuwa waziri wa wizara moja nyeti serikalini kabla ya Rais kikwete hajavunja baraza hilo.....

Waziri huyo ni mbunge kutoka katika jimbo moja lililopo katika mkoa wenye maji mengi na uoto wa asili ya kijani kibichi ingawa hakuna bahari......

Katika meseji hizo zilizosambazwa kwa kasi, mojawapo imeandikwa hivi:
"Wewe ni mtoto mdogo lakini nakupenda sana.Ukinikubalia tukutane Nairobi ili nikupe raha za maisha"

Baada ya kuzinasa meseji hizo, mwandishi wetu alimtafuta rafiki wa karibu wa Lulu ili kujua kama ni kweli alinasika na Waziri huyo.....

"Ni kweli Lulu alikwenda Nairobi kukutana na waziri huyo ila kilichofanyika huko siwezi kukisema".....Alieleza rafiki huyo

No comments:

Post a Comment