INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Thursday, October 18, 2012

BURUDANI: KABURI LA KANUMBA LAJENGWA UPYA




Muonekano mpya wa kaburi la Steven Kanumba

 Kaburi la aliyekuwa msanii maarufu wa filamu Tanzania, Steven  Charles Kanumba limeanza kujengwa upya ikiwa ni baada ya wasanii wenzake kushushuliwa kuhusiana na muonekano wake ulivyokuwa.
Marehemu Steven Kanumba 'The great' enzi za uhai wake.

Hatua ya kulijenga upya kaburi hilo imechukuliwa na Mama yake mzazi, Flora Mtegoa na kampuni ya Steps kutokana na mauzo ya  kazi zake mbalimbali za filamu, hivyo  wameona ni vyema wakalijenga upya kwani lilikuwa ni gumzo kwa watu mbalimbali waliokuwa wakihoji hadhi ya kaburi hilo na umaarufu wa marehemu Kanumba.
Akizungumza na paparazi wetu, Mama Kanumba alisema kauli za kaburi  hilo kujengwa upya zilikuwa kama wimbo wa taifa  lakini  kuna mambo alikuwa akiyamalizia, hivyo kwa sasa ameshalijenga vizuri tofauti na lilivyokuwa mwanzo.
Mama mzazi wa marfehemu Steven Kanumba amesema kuwa Kaburi la Kanumba limejengwa upya japokuwa baba yake alisema hakuna haja ya kulijenga tena lakini lakini bado ana uchungu na mwanae japokuwa amemuacha huku bado anampenda na ataendelea kumkumbuka, kwa kushirikiana na kampuni ya Steps waumelijengea vizuri.
 Hivi karibuni wasanii mbalimbali wa filamu Bongo walilitembelea kaburi hilo na kupatwa na uchungu lakini walishushuliwa na mwenzao na kwa kuwaambia kuwa wamelisusa kaburi hilo.
 Imeonekana kuwa kaburi hilo halikuwa na hadhi ikilinganishwa  na umaarufu aliokuwa nao Kanumba, hakustahili kulala  kwenye kaburi lile, hivyo kuwataka kuchangishana fedha ili lijengwe vizuri lakini hakuna aliyeunga mkono badala yake waliishia kupeana manenoyasiyofaa

No comments:

Post a Comment