INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, October 15, 2012

WOLPER AKANUSHA KUURUDIA UKRISTO BAADA YA KUACHIKA

 
               Jacqueline Wolper.

MSANII wa filamu ambaye alisilimu, Jacqueline Wolper amesema licha ya kwamba ameachana na mchumba wake Ramadhani Mtoro ‘Dallas’ atabaki kuwa Muislam hadi mwisho wa maisha yake.
Wolper ambaye sasa anafahamika kwa jina la Ilham alisema, ni kweli alibadili dini baada ya kuchumbiwa na Dallas lakini atakuwa anamchezea Mungu kama ataamua kurudi kwenye Ukristo baada ya uchumba kuvunjika.
“Mimi nitabaki kuwa Muislam hadi kifo, siwezi kurudi kwenye Ukristo kwani nilikuwa nikiupenda Uislam.
Akitokea mwanaume Muislam akataka kunioa niko tayari na hata akija Mkristo pia ila nitaendelea kuwa Muislam,” alisema Wolper.
Wolper alibadili dini siku chache zilizopita baada ya kuingia kwenye uhusiano na Dallas lakini hivi karibuni kulikuwa na madai kwamba amerudi kwenye Ukristo, jambo ambalo amelikanusha.

No comments:

Post a Comment