INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, October 15, 2012

SHILOLE NA SAJENTI WAKWIDANA CHOONI!


WASANII wa filamu za Kibongo, Zuwena Muhammed ‘Shilole’ na Husna Idd ‘Sajent’ hivi karibuni walizinguana na kufikia hatua ya kukwidana katika choo kilichopo ndani ya viwanja vya Leaders Club jijini Dar.
Chanzo chetu kilichokuwa katika eneo la tukio kilidai kuwa, kisa cha wawili hao kukwidana kilianzia kwenye kikao cha kuchagua uongozi mpya wa Bongo Movies.

Zuwena Muhammed ‘Shilole’.
“Katika kikao hicho, walianza kujadili mwenendo wa wasanii ambapo ilifika wakati Shilole na Sajenti walitofautiana, Shilole alipokwenda chooni, Sajenti alimfuata na huko ndiko kuliibuka timbwili,” kilidai chanzo hicho.
Katika kujua ukweli wa tukio hilo, Ijumaa Wikienda liliwatafuta wahusika ambapo Shilole alipopatikana alisema: “Zile zilikuwa ni tofauti za kawaida tu kama mnavyoweza kutofautiana nyie kazini, kwa sasa tuko sawa.”

Husna Idd

No comments:

Post a Comment