INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, October 15, 2012

SNURA AKIRI KUTAMANI NDOA

Snura Mushi akiwa ameweka pozi


MWIGIZAJI wa filamu za Kibongo ambaye pia ni msanii wa Bongo Fleva, Snura Mushi amefunguka kuwa anatamani ndoa kuliko kitu kingine chochote, japokuwa bado hajapata mwanaume anayemfaa,
Akichonga na safu hii, Snura alitiririka kuwa amekuwa akimwomba Mungu usiku na mchana ampatie mume mwema atakayekuwa na mapenzi ya dhati, mwenye heshima na mcha Mungu lakini wapi!
“Namuomba Mungu anipe mume mwema na hivi sasa nafanya kazi kwa bidii kwani ndiyo mkombozi wangu, najua siku ikifika Mungu atanipa mume mwema,” alisema Snura.

No comments:

Post a Comment