INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, October 15, 2012

BABY MADAHA AKANUSHA JUU YA KIFO CHA MAMA YAKE MZAZI

SIKU chache baada ya kuenea kwa taarifa kuwa mkali wa ngoma ya Amour ambaye pia anafanya vyema kwenye filamu za Kibongo, Baby Madaha, ameondokewa na mama yake mzazi, staa huyo amefunguka na kuweka mambo sawa kuwa aliyekufa siyo mama yake mzazi kama watu walivyosikia bali ni mama yake mdogo aitwaye Maimuna.
Akichonga na Over The Weekend, Baby Madaha alisema mama yake mzazi yupo hai na hana tatizo lolote la kiafya hivyo watu wasielewe tofauti na kwamba mama yake mdogo ndiye aliyekuwa anaumwa kwa kipindi kirefu kabla ya kukutwa na mauti usiku wa Oktoba 9, mwaka huu na kusafirishwa hadi Musoma kwa mazishi.
“Nawashukuru watu wote walioguswa na kilichotokea lakini naomba kueleza kuwa aliyetutoka siyo mama mzazi kama ilivyoelezwa awali bali ni mdogo wake, mama yangu bado yupo hai na anaendelea na shughuli zake kama kawaida,” alisema Baby Madaha.

No comments:

Post a Comment