INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Monday, October 29, 2012

JACK WOLPER ATWAA TAJI LA IJUMAA SEXIEST GIRL






Jacqueline Wolper (kulia), akipokea cheti cha ushindi kutoka kwa DK. Cheni aliyekuwa jaji mkuu wa shindano hilo. Wolper akiwa ameshikiria cheti chake muda mfupi baada ya kutangazwa mshindi. Dok. Cheni akiwa kwenye pozi na Wolper juu ya jukwaa. Msanii wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz akiwajibika jukwaani na mnenguaji wake.
Chidy Benz akikamua jukwaani hapo.
Omm Dipoz akizungumza na mashabiki zake jukwaani.
Dogo Asley akiwajibika.
Awali jana mchana hawa ni baadhi ya watoto wakichezeshwa ukumbini hapo.
Watoto hawa wakijiandaa kushindanishwa moja ya mchezo wa kuzungucha rigi kiunoni jana mchana ukumbini hapo.
Mmoja wa watoto waliofika Dar Live mchana akikabidhiwa baiskeli baada ya kuibuka mshindi katika mchezo wa kuruka kamba.

Mchekeshaji maarufu Mtanga, akizungumza na mmoja wa watoto ndani ya Dar Live.
Sehemu ya umati uliyojitokeza ukumbini hapo.

MSANII wa chimbo la filamu Bongo, Jacqueline Wolper Masawe, usiku wa kuamkia leo ameibuka kidedea kwenye shindano lililokuwa likiwashirikisha mastaa wa kike Bongo la Ijumaa Sexiest Girl ndani ya Ukumbi wa Dar Live Mbagala jijini Dar es Salaam.

Wolper amejizolea heshima lukuki na kitita cha sh. milioni 2 ikiwemo na ofa ya kulipiwa saluni kujiremba kwa mwaka mzima. Usiku wa leo pia ndani ya ukumbi huo kulikuwa na burudani kibao kutoka kwa Ommy Dimpoz, Chidy Benz, Dogo Asley, TOT Taarab na michezo kibao ya watoto iliyosindikizwa na shindano la Mkali wa Mic.

BAADA YA KUCHUMBIWA, ‘JINI KABULA’ AWAPA MAKAVU WABAYA WAKE…!!


Msanii wa Bongo movie Jini Kabula, ameweka wazi kuwa tayari ameshaingia kwenye maisha mapya, kwani ameshachumbiwa na mwanaume aliyedai kuwa ni mfanyabishara ambaye mara nyingi husafiri kwenda nje, na kudai wabaya wake wanaochukia wameze sumu.

 Aliongeza kuwa “maisha yanabadilika na kama ameishi maisha ya kujiachia na starehe kwa muda mrefu sasa ni wakati wake wa kuishi ndani ya ndoa na kutulia” .

“Muda ukifika nitaolewa tu na wasiyotaka kazi kwao, unajua kuna wakati fulani huwa nawaza kwa nini nisiolewe na majibu yake yameshakuja kama hivyo uchumba tayari kilichobaki ni kuanza harakati za kumaliza kazi na mimi kuitwa mke,”.

SEND OFF YA AUNT EZEKIEL

PICHA 6 ZA SEND-OFF YA AUNT EZEKIEL ILIYO FANYIKA SERENA HOTEL








Tuesday, October 23, 2012

MSANII WA BONGO MOVIE 'MIRIAM' AKATAA KUOLEWA BAADA YA WAZAZI KULA MAALI




MSANII chipukizi kwenye tasnia ya filamu bongo, Miriam, ambaye ni mdogo wa msanii Jackine Wolper, amesema kuwa yupo kwenye wakati mgumu kwani wazazi wake wanamtaka aolewe kilazima na mtu ambaye hana mahusiano naye huku wakiwa tayari wameshachukua mahari.

Ishu hiyo awali kabisa ilidaiwa kuwa mwanaume ambaye amewekwa kwa ajili ya kumuoa ni mume wa mtu huku ndugu zake wakiwa wameshapokea nusu ya mahari tangu mwaka jana.

Mwandishi wa habari hizi, alimtafuta msanii huyo ili kuzungumza naye kwa kina juu ya hiyo, ndipo alipodai kuwa hawezi kusema lolote kwani haitaji kuolewa kwa sasa na kitu kikubwa kinachomtatiza ni kwamba mwanaume huyo tayari ni mume wa mtu.

Alidai baadhi ya ndugu zake wanadai kuwa nusu ya mahari imeshatolewa kwa ajili yake na endapo akikataa kufanya wanavyotaka hali itakuwa ngumu kwani hakuna kitu wanachoweza kurudisha kwa mwanaume huyo zaidi ya yeye kukubali kuolewa.

“Mimi siwezi kwa sababu sina mpango wa kuolewa kwa sasa lakini wazazi ndo kwanza wanataka mimi nifanye hivyo yani nashindwa kuelewa nifanye nini kwa hili, kila ndugu ninayemfuata kumbe anajua kila kitu juu ya hilo suala na walishindwa kunishirikisha mimi ili nitoe mawazo yangu,” alisema kwa unyonge.

WEMA SEPETU AFANYA KUFURU




KATIKA kuonesha jeuri ya fedha, Wema Isaac Sepetu amefanya kufuru kama kawaida yake baada ya kumlowanisha mwili mzima kwa pombe za bei mbaya mrembo aitwaye Rehema Kimbu.



Mrembo Wema Sepetu akimwogesha Rehema Kimbu kwa pombe. Tukio hilo lililoshuhudiwa na mwanahabari wetu lilijiri nyumbani kwa mwigizaji Aunt Ezekiel, Mwananyamala, Dar, Ijumaa iliyopita ambapo Wema na Aunt walimfanyia ‘sapraizi’ ya birthday Rehema ambaye ilikuwa siku yake ya kuzaliwa.

Katika hali ya kushangaza, Rehema ambaye ni shosti mkubwa wa Aunt alishtukia anamwagiwa pombe mfululizo aina ya Gordon’s na Jack Daniels huku mwigizaji Nice Chande akimmiminia chupa kubwa kadhaa za maji.


Muda mwingi Wema alikuwa akimmwagia Rehema pombe bila kushusha mkono. Kufuatia kitendo hicho kilichoambatana na kelele nyingi za mastaa hao, kilisababisha wapita njia kujazana getini kwa Aunt bila kujua kilichokuwa kikiendelea na kudhani Rehema alikuwa akipokea kipigo.

AUNT EZEKIEL ATOA SABABU ZA NDOA YAKE KUFANYIKA KABLA YA SEND OFF NA KITCHEN PART



Wiki iliyopita picha za muigizaji wa filamu nchini, Aunt Ezekiel akifunga ndoa zilisambaa kwa kasi kwenye mtandao na kuzua maswali mengi kama iwapo amefunga ndoa kweli ama ni usanii tu. Wengi waliamini kuwa amefunga ndoa na wengi pia walikuwa na mashaka.

Waliokuwa na mashaka walihisi si kweli kutokana na sababu zifuatazo.

1. Aunt Ezekiel alikuwa akiendelea kukusanya michango ya harusi iweje aamue kufunga ndoa wakati bado anachangisha?

2. Kwanini harusi yake isihudhuriwe na watu wake wa karibu hata kama ni ya kiislamu? (kutokana na picha hizo)

3. Aliwahi kuhojiwa na kudai kuwa angefunga ndoa mwezi November

Lakini ukweli kuwa picha hizo zilimaanisha kuwa tayari amefunga ndoa. Lakini kuna sababu za harusi yake kuwa hivyo.

“Ni mchumba wangu na hakika yeye ndiye mwenye maamuzi nikaamua nifanye hivyo,” ameiambia ‘Movie Leo’ ya Clouds FM.

“Naweza sema bado yaani siko sawa mpaka nihakikishe hivyo vitu vyote vimeenda vimepita salama manake unajua shughuli yoyote hata kama ndogo lakini lazima unajua yaani unakaa ni pressure yaani sijui itakuaje sijui itakuwa vipi?

Kwahiyo naweza kusema kwasababu ni mwanzo kwahiyo bado kiukweli naona yaani huko mbele kutakuaje.”

Kutokana na kufanya mchakato wake ‘kiflashback’ yaani kuanza na hatua ya mwisho ya harusi na kurudi nyuma, muigizaji huyo pia ameelezea jinsi Kitchen Party za Send-off zitakavyokuwa, “nataka nifanye vitu vya tofauti na kila kitu nataka kiwe tofauti na vile watu ambavyo wamezoea kuviona au wamewahi kwenda , kwahiyo mwisho wa siku nikisema niseme itakuaje, itakuwa hivi itakuwa hivi naweza nikawa nimezusha ugomvi.”

And by the way sasa jina lake ni Rahma baada ya kubadilisha dini na kuwa muislamu.

ELIZABETH MICHAEL AKA LULU ARUDISHWA RUMANDE






Msanii maarufu wa filamu nchini, Elizabeth 'Lulu' Michael pichani juu, akielekea kupanda basi la magereza kwenye viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkaazi Kisutu, baada ya kesi inayomkabili ya kutuhumiwa kumuua msanii mwenzake, Hayati Steven Kanumba, kuahirishwa tena na hivyo mwanadada huyo ambaye umri wake unaleta utata ataendelea kusota rumande hadi hapo kesi yake itakapotajwa tena

Thursday, October 18, 2012

JENNIFER KYAKA (ODAMA) ARUDI NCHINI TANZANIA NA VIFAA VIPYA VYA KISASA KWAAJILI YA MOVIE

 Mmeona mambo haya!!!
 Kazi imepamba moto katika kuchagua stand maridadi kwaajili ya camera
 Duh hii kiboko!!!
 Mama yangu kazi imeanza..ni balaaaa!!!!

 Mhh!!



 Baada ya kuchagua saaaaana , nikaamua kupumzisha akili kwanza...!!!
 Duh hizi silaha au stand????

 Kazi imeanza sasa kutafuta Boom Mic ya ukweli, si unajua mambo ya sauti kwenye movieeeeee!!!
 Nikikagua Stick ya Boom

 Mhh!! Kazi ipo!!!
 Bei gani kwani??
 Iko poa!!!

 What?

SIKU YA PILI KAZI ILIENDELEA YA KUTAFUTA VIFAA  VINGINE BORA VYA MOVIE.

 Leo kazi ipo!!!
Baada ya zoezi zima kumalizika ukafika wakati wa kupata snaps za kumbukumbu