INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Wednesday, May 2, 2012


SIPENDI MAVAZI YANGU KUHUSISHWA NA ULOKOLE WANGU - DOKI
MSANII Ummy Wenceslaus, maarufu kama Dokii, ambaye awali alikuwa akiigiza kwa lafudhi ya Kikenya, amesema kuwa anashangazwa na watu ambao wamekuwa wakimsema au kumsengenya na kuwa na mashaka na wokovu wake. 

Anasema kuwa ulokole wake hauingiliani na mavazi au staili ya nywele alivyonyoa na kuzisuka. 

Watu wana maneno sana, kila Dokii akifanya kitu lazima waongee, wengine wanasema kwa nini Dokii akicheza anakata viuno sana wakati anajifanya mlokole? Mbona kanyoa vile! 

"Binafsi najiamini kama nimeokoka na kukata viuno ni utamaduni tu, kama msanii naweza kufanya jambo lolote kwa ajili ya kuelimisha na kuburudisha na hakuna cha ziada, anasema Dokii. 

Dokii anasema kuwa hajawahi kumkosoa Mungu kwa kujichubua ngozi yake kama walivyo baadhi ya waumini ambao pia nao wameokoka na kuhubiri, lakini watu wanamsema yeye kuhusu kucheza muziki, kuimba na kukataa viuno. 

Amesema anashanga watu kuingiwa na hisia za ajabu na akahoji ni sehemu gani katika Biblia imeandikwa mtu asiche muziki. 

Mimi sijali ya watu bali ndani ya nafsi yangu ndiyo najua wokovu wangu, kama unavyoniona, nimekuja na staili mpya kabisa ambayo nimeibuni mwenyewe na kuipa jina la 'Hakunaga kata ngebe man', najua watatesema

No comments:

Post a Comment