INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Saturday, February 21, 2015

GLOBAL WALIVYOFANYA MAHOJIANO NA ODAMA KUJUA KUCHANGIA WANAUME

Laurent Samatta
MAMBO yanazidi kunoga ndani ya safu hii ya Sindano 5 za moto, kutokana na maombi yenu, leo tumemleta kwenu mwigizaji Jeniffer Kyaka ‘Odama’, tiririka naye:

Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Jeniffer Kyaka ‘Odama’.

Paparazi: Mambo vipi Odama! Tuanze moja kwa moja na swali la kwanza, hivi kwa sasa una mpenzi? Mbona hatumjui?

Odama: Mambo poa! Mpenzi ninaye, nampenda muda bado wa kumuanika.

Paparazi: Ulishawahi kuchangia bwana na mwanamke mwingine katika maisha yako?

Odama: Hapana, sina kumbukumbu hiyo.

Paparazi: Hadi leo hii unaweza kukumbuka idadi ya wanaume ambao umewahi kutoka nao kimapenzi?

Odama: Nakumbuka, kama mtu hukumbuki idadi basi lazima utakuwa una kichaa. Nakumbuka kwa sababu idadi ni ndogo, ila hapa sitataja idadi yao.

Paparazi: Hivi baba mtoto wako ni nani hasa au ndiye uliyenaye hadi sasa?

Odama: Hilo liweke kapuni kwa sasa, nitalizungumza ‘next time’.Paparazi: Inasemekana wewe ni miongoni mwa warembo ambao wanaoongoza kwa kutongozwa Bongo Movies, ni kweli?

Odama: Hiyo kawaida kwa mtoto wa kike, nadhani sipo peke yangu.

No comments:

Post a Comment