INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Saturday, February 21, 2015

JINI KABULA ALIA NA CD ZA ‘MAGAIDI’

Stori: Gladness mallya
MSANII wa filamu Bongo, Miriamu Jolwa ‘Jini Kabula’ amefunguka kwamba anateseka na viashirio vya vita hasa baada ya CD zilizosambazwa na watu wasiojulikana wanaosema ni magaidi kudai kuwepo kwa vita nchini.


Msanii wa filamu Bongo, Miriamu Jolwa ‘Jini Kabula’.

Akipiga stori na gazeti hili, Jini Kabula alisema amekuwa akikesha akimuomba Mungu ailinde nchi ya Tanzania na aiepushe na vita kwani tangu amezaliwa mpaka alipofikia amekuzwa na amani na anajivunia kuwa Mtanzania na anafurahi hivyo Watanzania wote wanatakiwa kudumu katika maombi ili damu isimwagike kama hao magaidi wasiotakia mema nchi wanavyoahidi. “Namuomba Mungu usiku na mchana vita isitokee maana tumezoea amani sasa ikitokea ukweli sijui tutafanyaje na tutakimbilia wapi hivyo ni jukumu la kila Mtanzania kumuomba Mungu atuepushe na janga hilo,” alisema Jini Kabula.

No comments:

Post a Comment