INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Tuesday, February 17, 2015

DUDE, ESTER WAWAPANDISHA MORI LA SABA

Imelda mtema/Uwazi
STAA aliyewahi kuvuma na kundi lake la Bongo Dar es Salaam, Kulwa Kikumba ‘Dude’ juzikati aliambatana na msanii mwenzake wa filamu, Ester Kihama katika Shule ya Msingi Mgulani kwa ajili ya kuwahamasisha wanafunzi wa darasa la saba kufaulu katika mitihani yao.


Staa aliyewahi kuvuma na kundi lake la Bongo Dar es Salaam, Kulwa Kikumba ‘Dude.

po waliwapandisha mizuka wanafunzi hao baada ya kuwapa zawadi washindi waliofaulu vizuri mitihani ya kila wiki na kuwaahidi kuwa kila wiki watakuwa wakitoa zawadi kwa washindi.


Msanii wa filamu Bongo, Ester Kihama.

Tunataka wanafunzi muwe mnasoma kwa bidii kwa kuwa hakuna kitu kizuri kama kusoma na kutimiza ndoto zenu. Tutakuwa tunakuja kila wiki kuwatembelea na kujua maendeleo yenu, pia kuhakikisha mwaka huu mnafaulu wote,” alisema Dude.

No comments:

Post a Comment