INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Tuesday, February 10, 2015

FROLA MVUNGI AHOFIA MTOTO WAKE KUTEKWA


Frola mvungi mwigizaji wa filamu Swahilihood.

MWIGIZAJI wa filamu na muziki Bongo Frola Mvungi yupo katika wakati mgumu baada ya kuhofia mtoto Tanzanite kuitekwa na watu wasiojulikana, msanii huyo amedai kuwa kuna watu ambao wamefika nyumbani kwake zaidi ya mara tatu kumtaka mfanyakazi wa awape mtoto huyo.

“Nimepatwa nahofu mtoto wangu sijui antaka kuibiwa na watu wasiojulikana mara ya kwanza walikuja watu wawili mwanamke na mwanaume wakamwambia dada wa kazi kuwa nimewaagiza wamchukue Tanzanite wampeleke shule, dada akawatalia,”anasema Frola.

Frola akiwa na mwanaye Tanzanite akiwa mdogo.

Frola amedai kuwa baada ya kukataliwa na mfanyakazi wake alikuja mtu mwingine mwanamke wa Kiarabu akijifanya ni rafiki yake akiomba kitana achane nywele dada alipoingia ndani bila kukaribishwa aliingia hadi seatingroom akidai aachewe mtoto lakini msichana alikataa, hivyo anahofu juu ya mtoto wake.





No comments:

Post a Comment