INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Friday, August 3, 2012

NDIKUMANA:'SIJAWAI VUNJA NDOA YANGU



Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krish’ akiwa  na mumewe Hamad Ndikumana ‘Kataut’.
Na Imelda Mtema
MUME wa Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krish’, Hamad Ndikumana ‘Kataut’ ambaye kwa sasa anasakata kabumbu kwenye Timu ya Rayon Sports ya nchini kwao Rwanda, kwa mara ya kwanza ameizungumzia ndoa yake iliyoingia gogoro mwaka jana akisema kuwa hajawahi kuivunja ndoa yake.
Akizungumza kwa njia ya simu akiwa Rwanda, Ndikumana maarufu Bongo kwa jina la Ndiku alisema kuwa kumekuwa na maneno mengi kuhusu ndoa yake kuvunjika lakini alithibitisha kuwa hajawahi kusema lolote kwani hakukuwa na jambo kama hilo.
“Nilijua na ninajua watu wengi waliongea na wanaongea kuhusu ndoa yangu kuvunjika lakini ndoa inavunjikaje kama wahusika wenyewe hawajasema kama imevunjika?”
Mwanasoka huyo aliendelea kutiririka kuwa kama alifunga ndoa yake kanisani basi ni lazima kanisa lingejua kuwa imevunjika kwa maana lazima angeenda kusema.
0 comments

No comments:

Post a Comment