INSIDE INAPATIKANA MADUKANI

FILAMU YA JADA ITAKUWA SOKONI 19.02.2015

JADA IPO SOKONI

JADA IPO SOKONI

Wednesday, August 22, 2012

SHILOLE: FLORA ASIJISHAUE



STAA wa filamu na muziki Bongo, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ amekanusha kupokelewa mjini na mwenzake Flora Mvungi na kumtaka  msanii huyo aache kujishaua kwani yeye ndiye aliyempokea mjini.
Shilole aliiambia Tollywod Newz juzikati jijini Dar kwamba, Flora aache kujishaua kwani wakati alipokuwa akiingia mjini yeye (Shilole) ndiye aliyempokea na kushangaa kusikia akijitapa tofauti.
“Mwambieni asijishaue, tena aache kujitafutia umaarufu usiokuwa na maana, miye ndiye niliyempokea mjini enzi hizo, iweje leo anigeuke?” alihoji Shilole ambaye hivi sasa anatamba na muziki wa mduara.
Hivi karibuni, Flora aliripotiwa akisema kuwa, yeye ndiye aliyempokea Shilole wakati alipokuwa akiingia jijini Dar.

No comments:

Post a Comment